Kukaa kimya pia ni jibu, lakini si jibu la kila kitu

RIGHT MARKER

Senior Member
Joined
Apr 30, 2018
Posts
129
Reaction score
473
📖Mhadhara wa 24:
Kadiri unavyokuwa mkimya ndivyo unazidi kujiongezea thamani na sifa nzuri. Hupaswi kujibu kila kitu, unashauriwa kukaa kimya kwenye baadhi ya mambo.

Kukaa kimya pia ni jibu, lakini si jibu la kila kitu. Unafika wakati unapaswa kuvunja ukimya na kuzungumza, kwa maana pia ukiacha kuzungumza watu wengine wanaweza kufasiri ukimya wako.

Unapoamua kuzungumza jitahidi usieleweke, wachanganye wasikilizaji wako. Swali moja lisikufanye utoe majibu ya maswali kumi ambayo hukuulizwa. Majibu yako mafupi au ukimya huwafanya watu wasikujue zaidi.

Soma Pia: Kukaa kimya ni mbinu wanayoitumia Watu wajinga kuficha udogo na ufinyu wa akili zao


Right Marker
Dar es salaam.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…