Pole sana ndugu yangu.
Kama shauri hilo lilianzia baraza la kata, muda wa kukata rufaa kwenye uamuzi ulitolewa na baraza la ardhi la wilaya, ni siku 60 tangu hukumu iliposomwa.
Kama shauri lilianzia moja kwa moja katika baraza la ardhi la wilaya (yaani mogogoro uliozidi tshs 3,000,000), sheria ya ardhi haikuweka muda wa kukata rufaa. Katika hali hiyo inabidi utumie sheria ya kikomo cha muda sura ya 89, jedwali la kwanza sehemu ya pili inayohusu sheria ya mwenendo wa mashauri ya madai, inayoonyessha kuwa iwapo sheria iliyaondikwa haikuweka kikoma cha muda wa kukata rufaa, basi muda utakuwa siku 90.
Muda huo huhesabiwa tangu siku ulipopewa nakala ya hukumu.
Mambo ya kuambatisha hutegemea pia shauri lilikoanzia. Kwa mfano kama lilianzia baraza la kata, basi inabidi sababu za rufaa zisajiliwe katika masjala ya baraza la wilaya nk.
Hivyo ndugu yangu sheria ina mzunguko mrefu. Inabidi tupate few details. kwa mfano shauri lilianzia wapi -kata? nini ilikuwa hukumu yao. je lilifikaje baraza la wilaya, nini hukumu ya baraza la wilaya nk.