DOKEZO Kukithiri kwa matendo ya rushwa kampuni ya ujenzi ya Shandog Luquiao Group Co.ltd mradi wa Mwendokasi

DOKEZO Kukithiri kwa matendo ya rushwa kampuni ya ujenzi ya Shandog Luquiao Group Co.ltd mradi wa Mwendokasi

  • Thread starter Thread starter Anonymous
  • Start date Start date
Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Fikiria unatafuta ajira ili upate pesa, mwingine anakwambia utoe pesa ili upate ajira.

Kwa wale wenzangu na mimi mtakuwa mnaelewa machungu ya kuambiwa hivyo ili hali mfukoni huna hata mia na hujui utapata wapi nauli ya kurudia geto wala msosi wa usiku.

Ndani ya mradi wa ujenzi wa barabara ya mwendokasi awamu ya nne loti 2 kutoka mwenge mpaka tegeta (dawasa) unao fadhiliwa na benki ya dunia kumekuwa na rushwa iliyokithiri.

Katika mradi huo kampuni ya ujenzi ya SHANDOG LUQUIAO GROUP CO.LTD kutoka china ndio mtekelezaji mkuu wa mradi huo, kempu yao ipo karibu na mataa ya kawe opposite na fremu za jeshi hapa Lugalo karibu na kituo cha daladala cha bondeni.​

Kumekuwa na vitendo vya rushwa ambavyo havivumiliki kutoka kwa HR wakibongo wa kampuni hiyo akiwataka waombaji wa nafasi za kazi kutoa rushwa ili wapate ajira bila hivyo utachelewa sana kupata kazi au usipate kabisa.

Ikiwa wewe ni kibarua au saidia fundi unatakiwa kutoa laki moja mafundi au dereva au operator wanatakiwa kutoa laki moja na hamsini mpaka laki mbili na hana huruma na sura ya mtu.

Hali hiyo ya kukithiri kwa rushwa imepelekea watu kutoka mikoa ya mbali kuajiriwa kwa wingi huku wakazi wengi wa maeneo hayo kukosa nafasi ili hali sera, sheria na kanuni za nchi zinataka wao kupewa kipaumbele zaidi.

Mbaya zaidi HR huyu anajenga chuki kubwa sana kati ya wale wanaotoa rushwa na wale waliokataa kutoa wakiamini kupata kazi bila hongo ni haki yao kama Watanzania.

Unaeza kuta mtu mmesota naye miezi mitatu au mitano mkiwa marafiki mkisubiri nafasi ya kazi.

Ila kwa bahati mbaya yeye akafanikiwa kuingia kabla yako kwa kutumia rushwa, aisee akitoka hapo sio rafiki yako tena na akikuona anakukimbia kama hakujui.

Ukimuuliza kwanini unafanya hiyo anakwambia ndio tulivyoambiwa na HR tusiongee na ninyi.

Hali kama hiyo ya rushwa iliwahi kutokea miezi minne iliyopita kwenye moja ya kempu iliyopo karibu na bar ya 360 ukitokea mwenge kuelekea tegeta hapa maeneo ya Lugalo.

Ambapo vibarua, madereva na mafundi walitaka kutolewa kazini kiujanja ujanja ili waingize watu wao waliotoa rushwa kwa HR.

Watu wakagoma, baadae baadhi ya wanajeshi kutoka Lugalo wakaingilia sakata hilo na kulizima kimya kimya kwa vitisho visivyokuwa na tija kwa vibarua, madereva na mafundi ambao ilikuwa haki yao kuwa kazini kwa wakati huo.​

Tunaomba wahusika waingilie kati swala hili, ili kila mwananchi apate haki yake kabla hali haijawa mbaya zaidi.

~SAIDIENI JAMII
 
Fikiria unatafuta ajira ili upate pesa, mwingine anakwambia utoe pesa ili upate ajira.

Kwa wale wenzangu na mimi mtakuwa mnaelewa machungu ya kuambiwa hivyo ili hali mfukoni huna hata mia na hujui utapata wapi nauli ya kurudia geto wala msosi wa usiku.

Ndani ya mradi wa ujenzi wa barabara ya mwendokasi awamu ya nne loti 2 kutoka mwenge mpaka tegeta (dawasa) unao fadhiliwa na benki ya dunia kumekuwa na rushwa iliyokithiri.

Katika mradi huo kampuni ya ujenzi ya SHANDOG LUQUIAO GROUP CO.LTD kutoka china ndio mtekelezaji mkuu wa mradi huo, kempu yao ipo karibu na mataa ya kawe opposite na fremu za jeshi hapa Lugalo karibu na kituo cha daladala cha bondeni.​

Kumekuwa na vitendo vya rushwa ambavyo havivumiliki kutoka kwa HR wakibongo wa kampuni hiyo akiwataka waombaji wa nafasi za kazi kutoa rushwa ili wapate ajira bila hivyo utachelewa sana kupata kazi au usipate kabisa.

Ikiwa wewe ni kibarua au saidia fundi unatakiwa kutoa laki moja mafundi au dereva au operator wanatakiwa kutoa laki moja na hamsini mpaka laki mbili na hana huruma na sura ya mtu.

Hali hiyo ya kukithiri kwa rushwa imepelekea watu kutoka mikoa ya mbali kuajiriwa kwa wingi huku wakazi wengi wa maeneo hayo kukosa nafasi ili hali sera, sheria na kanuni za nchi zinataka wao kupewa kipaumbele zaidi.

Mbaya zaidi HR huyu anajenga chuki kubwa sana kati ya wale wanaotoa rushwa na wale waliokataa kutoa wakiamini kupata kazi bila hongo ni haki yao kama Watanzania.

Unaeza kuta mtu mmesota naye miezi mitatu au mitano mkiwa marafiki mkisubiri nafasi ya kazi.

Ila kwa bahati mbaya yeye akafanikiwa kuingia kabla yako kwa kutumia rushwa, aisee akitoka hapo sio rafiki yako tena na akikuona anakukimbia kama hakujui.

Ukimuuliza kwanini unafanya hiyo anakwambia ndio tulivyoambiwa na HR tusiongee na ninyi.

Hali kama hiyo ya rushwa iliwahi kutokea miezi minne iliyopita kwenye moja ya kempu iliyopo karibu na bar ya 360 ukitokea mwenge kuelekea tegeta hapa maeneo ya Lugalo.

Ambapo vibarua, madereva na mafundi walitaka kutolewa kazini kiujanja ujanja ili waingize watu wao waliotoa rushwa kwa HR.

Watu wakagoma, baadae baadhi ya wanajeshi kutoka Lugalo wakaingilia sakata hilo na kulizima kimya kimya kwa vitisho visivyokuwa na tija kwa vibarua, madereva na mafundi ambao ilikuwa haki yao kuwa kazini kwa wakati huo.​

Tunaomba wahusika waingilie kati swala hili, ili kila mwananchi apate haki yake kabla hali haijawa mbaya zaidi.

~SAIDIENI JAMII
Duuh Hatari.
 
Duuh Hatari.
Usishangae uliza mkurugenzi wake mkuu MWENDO KASI NI NANI. ukiweza tafuta back ground yake.huyo jamaa ni mpigaji hakuna tena..kahamishwa hamishwa sehemu nyingi kisa kotofautiana na viongozi wenzake ..ni jizi .
 
Pole sana Kijana,usijali wahusika wakipita humu swala lako watalifanyia kazi,na kila kitu kitakaa sawa,mtangulize Mungu kwa kila jambo na usikate tamaa,wwe endelea kupambana one day yess!!
 
HAPO SIO pa kufanya kazi.
Unaanza kufanya kazi kuanzia saa 1 asubuhi mpaka saa 1 usiku.mchina muuaji.
Kuhusu rushwa ni kawaida.hata hao wachina wamepata hyo tenda kwa rushwa.nani amfunge paka kengele?.
Kwa tanzania bila rushwa ni ngumu kupata kazi tusidanganyane.kila mtu anapiga kazini kwake.
 
HAPO SIO pa kufanya kazi.
Unaanza kufanya kazi kuanzia saa 1 asubuhi mpaka saa 1 usiku.mchina muuaji.
Kuhusu rushwa ni kawaida.hata hao wachina wamepata hyo tenda kwa rushwa.nani amfunge paka kengele?.
Kwa tanzania bila rushwa ni ngumu kupata kazi tusidanganyane.kila mtu anapiga kazini kwake.
Rushwa ni tatizo Tz,malipo ya vibarua ni shingap?
 
Rushwa ni tatizo Tz,malipo ya vibarua ni shingap?
10,000 imezidi sana 15,000
haizidi hapo kwa tanganyika.
Ila zanzibar 20,000 mpaka 25,000.
Makazi yenyewe magumuu na bado hela ndogo,kula kwako nauli kwako.ila mimi sipo hapo.
 
HAPO SIO pa kufanya kazi.
Unaanza kufanya kazi kuanzia saa 1 asubuhi mpaka saa 1 usiku.mchina muuaji.
Kuhusu rushwa ni kawaida.hata hao wachina wamepata hyo tenda kwa rushwa.nani amfunge paka kengele?.
Kwa tanzania bila rushwa ni ngumu kupata kazi tusidanganyane.kila mtu anapiga kazini kwake.
What should be done..au tuache iviivi
 
10,000 imezidi sana 15,000
haizidi hapo kwa tanganyika.
Ila zanzibar 20,000 mpaka 25,000.
Makazi yenyewe magumuu na bado hela ndogo,kula kwako nauli kwako.ila mimi sipo hapo.
Duh inabd kukomaa tu amna jinsi.bora kuwa na kitu kuliko kukosa kitu
 
Duh inabd kukomaa tu amna jinsi.bora kuwa na kitu kuliko kukosa kitu
Ehee.kama unayo wape.utafanyaje na mfumo wa ajira binafsi upo hivyo.
Na sio huko tu koooote.ni sehemu chache sana ambazo unaweza kuingia bila kuhonga.
 
Fikiria unatafuta ajira ili upate pesa, mwingine anakwambia utoe pesa ili upate ajira.

Kwa wale wenzangu na mimi mtakuwa mnaelewa machungu ya kuambiwa hivyo ili hali mfukoni huna hata mia na hujui utapata wapi nauli ya kurudia geto wala msosi wa usiku.

Ndani ya mradi wa ujenzi wa barabara ya mwendokasi awamu ya nne loti 2 kutoka mwenge mpaka tegeta (dawasa) unao fadhiliwa na benki ya dunia kumekuwa na rushwa iliyokithiri.

Katika mradi huo kampuni ya ujenzi ya SHANDOG LUQUIAO GROUP CO.LTD kutoka china ndio mtekelezaji mkuu wa mradi huo, kempu yao ipo karibu na mataa ya kawe opposite na fremu za jeshi hapa Lugalo karibu na kituo cha daladala cha bondeni.​

Kumekuwa na vitendo vya rushwa ambavyo havivumiliki kutoka kwa HR wakibongo wa kampuni hiyo akiwataka waombaji wa nafasi za kazi kutoa rushwa ili wapate ajira bila hivyo utachelewa sana kupata kazi au usipate kabisa.

Ikiwa wewe ni kibarua au saidia fundi unatakiwa kutoa laki moja mafundi au dereva au operator wanatakiwa kutoa laki moja na hamsini mpaka laki mbili na hana huruma na sura ya mtu.

Hali hiyo ya kukithiri kwa rushwa imepelekea watu kutoka mikoa ya mbali kuajiriwa kwa wingi huku wakazi wengi wa maeneo hayo kukosa nafasi ili hali sera, sheria na kanuni za nchi zinataka wao kupewa kipaumbele zaidi.

Mbaya zaidi HR huyu anajenga chuki kubwa sana kati ya wale wanaotoa rushwa na wale waliokataa kutoa wakiamini kupata kazi bila hongo ni haki yao kama Watanzania.

Unaeza kuta mtu mmesota naye miezi mitatu au mitano mkiwa marafiki mkisubiri nafasi ya kazi.

Ila kwa bahati mbaya yeye akafanikiwa kuingia kabla yako kwa kutumia rushwa, aisee akitoka hapo sio rafiki yako tena na akikuona anakukimbia kama hakujui.

Ukimuuliza kwanini unafanya hiyo anakwambia ndio tulivyoambiwa na HR tusiongee na ninyi.

Hali kama hiyo ya rushwa iliwahi kutokea miezi minne iliyopita kwenye moja ya kempu iliyopo karibu na bar ya 360 ukitokea mwenge kuelekea tegeta hapa maeneo ya Lugalo.

Ambapo vibarua, madereva na mafundi walitaka kutolewa kazini kiujanja ujanja ili waingize watu wao waliotoa rushwa kwa HR.

Watu wakagoma, baadae baadhi ya wanajeshi kutoka Lugalo wakaingilia sakata hilo na kulizima kimya kimya kwa vitisho visivyokuwa na tija kwa vibarua, madereva na mafundi ambao ilikuwa haki yao kuwa kazini kwa wakati huo.​

Tunaomba wahusika waingilie kati swala hili, ili kila mwananchi apate haki yake kabla hali haijawa mbaya zaidi.

~SAIDIENI JAMII
Hali hiyo ya kukithiri kwa rushwa imepelekea watu kutoka mikoa ya mbali kuajiriwa kwa wingi huku wakazi wengi wa maeneo hayo kukosa nafasi ili hali sera, sheria na kanuni za nchi zinataka wao kupewa kipaumbele zaidi.🤔🥺
 
Back
Top Bottom