Kukomesha utekaji serikali ipige marufuku vikundi hivi vya kisiasa kama itaweza

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2013
Posts
21,741
Reaction score
26,735
Tumekua tukishuhudia utekaji wa watu nchini vikifanywa na eti wasiojulikana! Hawa wasiojulikana ni watanzania ambao huenda wamejiambatanisha na vyama vya siasa, hata hivyo ni CCM tu ndiyo ina vikundi vinavyojulikana kama Chawa, Uhamasishaji, Wadudu na Green Guard(Umoja wa vijana), hawa huenda wanaweza kuwa wanatumia kauli ya ukinizingua chawa wangu hawatakubali, na tukiangalia utekaji unawakumba mashabiki wa upinzani zaidi kuliko wa CCM.

Kutokana na nilivyoeleza ni vizuri Serikali ikapiga marufuku vikundi vyote hivi wakati huu tunaelekea kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa na wa Rais na Wabunge ambako kutazuka wimbi la vikundi vya ulinzi.
 
Thubutu!
 
Kwa mfano hawa panya road wanaosumbua mijini ni UVCCM
 
acha porojo, wanaoteka ni serikali
 
Moto unawaka inatakiwa siku moja , hawa watekaji wafanyiwe jambo la history ndo utekaji utakoma, wakipigwa matukio mawili au matatu Heshima itakuepo tu
 
I think mkoloni alikuwa bora kuliko sasa na uhuru wetu fake, i wish Mwalimu angewapa uraia na kuwafanya sehemu ya uongozi tungekuwa mbali sana
 
Moto unawaka inatakiwa siku moja , hawa watekaji wafanyiwe jambo la history ndo utekaji utakoma, wakipigwa matukio mawili au matatu Heshima itakuepo tu
Kuna klipu moja iliwahi kutoka huko Dodoma UV CCM wakipewa mafunzo na chombo cha usalama.
 
Ila kusema kweli CCM inaipeleka hii nchi pabaya sana sana!
Wanatakiwa watambue kuwa tuendako wao watakuja kugeuka kuwa wahanga wa haya matukio!
 
 
Kuvipiga marufuku ni ngumu kwa sababu inaonesha kuna faida wanaipata.Haiwezekani uhalifu utokee na kukaliwa kimya au kufanyiwa masihara.
 
Unankumbusha kuhusu kujitekenya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…