beneli
Member
- May 1, 2013
- 86
- 7
Habari wanajukwaa ,poleni kwa mahangaiko ya kupata elimu maana mwatimiza maagizo ya muumba yeye aliyesema uza mali ukapate ufahamu..moyo wangu wauma hasa kwa kuona wasomi wengi wakiumia kwa kukosa ufadhili wa bodi ya mikopo ,wengi wakiwa wamekata tamaa na elimu kwa ujumla., wengi tunajua elimu sio mteremko na tumepitia mengi hadi kufikia sasa, wasomi wengi wa maswala ya fedha ,uongozi na sera wamesoma kwa mikopo hii hii na ni aibu kwa wasomi ambao wanatakiwa kuishauri serikali wao pia kulalamika, natumai wengi tunapenda kuona wadogo zetu wakisoma kwa amani miaka ijayo na kwa hivyo ningewashauri wataalamu wa fani mbalimbali kama maswala ya fedha(finance) uongozi wa biashara(bba) takwimu na uchumi , wakae pamoja na kutengeneza mpango (financing plan) utakao wasilishwa serikalini utakao husu namna ya kugawa mikopo kwa usawa utakao wafaidisha wanafunzi wote wenye uhitaji ,kuanzia na ada za vyuo, malazi na makazi pamoja na vyakula vitu vinavyotutesa wanafunzi wengi. Naweza onekana kama mwanasiasa ila ninachojaribu kusema ni kuwa sijawahi ona wanafunzi waliohitimu wakijaribu kutatua tatizo hili zaidi ya kulaumu na kukimbia kulipa madeni yao.nadhani imefika wakati sisi sisi wenyewe tuwe sehemu ya kutatua tatizo..elimu yako haina maana kwetu kama haitatukomboa..Nawasilisha.