Kukosekana kwa msimamo wa Mtaala Mpya wa Masomo ulioagizwa kutekelezwa toka Julai 1, 2024

Kukosekana kwa msimamo wa Mtaala Mpya wa Masomo ulioagizwa kutekelezwa toka Julai 1, 2024

Qin

New Member
Joined
Feb 29, 2024
Posts
2
Reaction score
1
Shule za advance zilifunguliwa July 1 2024 na tukapewa maelekezo ya kutumia mtaala ulioboreshwa.

Tukapeenda na seminar zilizochukua takriban siku 3, kutoka mtaala uliopita kuna masomo yalifutwa kama General studies(GS), na kuna yaliyobadilishwa kama Commerce kwenda business studies, kuna yaliyoongezwa kama Historia ya Tz na maadili na Academic communication, na kuna combi ambazo awali hazikuwepo ila sasa zipo na kuna wanafunzi wamekuja mashuleni kwa masomo hayo.

Sasa ni mwisho wa mwezi, tunapokea taarifa za kurudi kwenye mtaala uliopita sababu zikiwa kukosekana kwa vitabu. Hawakuliona hili kabla ya agizo la kuutekeleza? Umepotea muda, na pesa nyingi sana kwenye zile seminar.

Kikubwa zaidi, jamani tunawachanganya sana wanafunzi. Na kuhusu hizi combi mpya, mbona hatupewi utaratibu?
 
Sasa wale wanafunzi waliofika shule tayari kwa hizo combi mpya watafanyaje?, mfano ipp huko mkoa mwingine,Combi nyingine zilizobalance hazipo kwenye shule hiyo?...Ujinga na upuuzi mtupu.
 
Waku laumiwa ni Prof. Mkenda pamoja na kuwa elimu Ndiyo kada yake, lakini wizara hii imemshinda. Juzi kati niliona anasema II mwalimu apate leseni ya kufundisha lazima ajitolee mwaka mmoja. Huo utaratibu ungeanza kwa wale wanaotoka vyuoni sasa. Sio wale wapo kazini tayari. Watafute njia nyingine ya kuwapa hizo leseni ambao tayari wameajiriwa aidha serikalini au binafsi.
 
Back
Top Bottom