Kukosekana kwa taarifa juu ya kinachojiri HESLB

Mbute na chai

JF-Expert Member
Joined
Jul 21, 2012
Posts
564
Reaction score
593
Ndugu, rafiki, na jamaa Jforums, poleni sana hasa wanafunzi wanaongoja kwa hamu kujua kama wamepata mikopo toka HESLB. Ukimwa wa HESLB ni dharau ambayo taasisi nyingi zenye dhamana za serikali huwa nayo. Ni wazi kuwa mgawanyo wa fedha huitaji umakini, lakini umakini huu pasina taarifa ya hatua zilizofikiwa ni umakini gani? Serikali iliyo wazi, uwazi wake hujidhihirisha kupitia upatikanaji wa taarifa sahihi juu ya kinachojiri katika utendaji kazi wake. Dharau hii imejidhihirisha pale wanafunzi wanapoomba taarifa toka HESLB, kwani ni haki yao, na kupewa majibu ambayo ni ya mtu kujisikia (discretionary), yanayopelekea baadhi ya wanachama wa jf kuweka mada juu ya HESLB zilizowafanya waonekane waongo. Kwasababu hii, bodi ya mikopo elimu ya juu imepewa madaraka ya kupitiliza, hivyo ni wakati sasa serikali ipitie upya madaraka haya na kuweka mda maalum wa wanafunzi kutuma na kupata taarifa ya maombi ya mikopo. Na hii huonesha umaskini wa utumiaji wa elimu tunayoipata kwa manufa yetu na vizazi vijavyo kwani wafanyayo haya ni wasomi tena wenye shahada za uzamivu n.k. Tafadhali bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu toeni taarifa mmefikia wapi kwani baadhi ya vyuo huanza usajili juma lijalo mwezi huu wa tisa.
 
tatizo serikali yetu ni kipofu na kiziwi, hawaoni wala kusikia
 
bora umenisaidia mkuu, coz nami nilidanganywa nikadanganyika na kujikuta nimepost nilichodanganywa. Watanganyika tumechoka kuwa Wadanganyika, HESLB semeni ukweli
 
Wenye mamlaka ya kuona,kuskia na kuwajbka kwa hil,watoto wao hawana KABSA mpango na boom coz kuskul wao n 100% uhakika!kayumbaz kaz 2nayo kwel!hil liserikal bovu lnantia hasira!aaaaaaaargh!
 
bora umenisaidia mkuu, coz nami nilidanganywa nikadanganyika na kujikuta nimepost nilichodanganywa. Watanganyika tumechoka kuwa Wadanganyika, HESLB semeni ukweli

pole mkuu!! I hope before Wednesday next week mambo yatakua mambo
 
Yaan 2meomba loan toka mwez wa5 alaf hao bod mwakajana niliwauliza pale nanenane dom kuhusu mkopo wakaniambia system ndo hua inagawa mkopo,sasa km system nikitendo cha kubonyeza k2 ambacho hakichukui hata wik.sio siri loan bord mna2boa kishenzi.
 
achen tu wapendwa maana tanzania walikua wanaiongoza kama watu vipofu lakini si watanzania wa sasa tuna macho nauelewa wakutambua haki zetu na sio wakupelekwa tu walipaswa kutoa taarifa walipo fikia sio kukaa kimya nakuacha watu bila kuelewa wamesimama wp haya ni madhaaarau
 
Viongozi wa hii bodi ni janga la elimu ya juu.

kwakweli wanakera sana.

Wanafikiri hizo pesa ni msaada wanatupa.

Ovyo kabisa hawa watu.
 
ivi mbona kila mtu HESLB HESLB HESLB HESLB amjiu kama bodi ya mikopo wanasubiri mpaka TCUwamalize kila kitu, sasa ni jana tu ndio ilikua dedline ya watu kuomba vyuo mi sioni kama HESLB wana tatizo ila tatizo langu lipo TCU
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…