Kuku wangu hawaponi mafua ni chotara msaada wadau tafadhali

Kuku wangu hawaponi mafua ni chotara msaada wadau tafadhali

ayunus

Member
Joined
Dec 29, 2014
Posts
6
Reaction score
0
Ninaomba msaada wenu wajasiriamali maana nimetumia kila sina ya dawa hata sijui tatizo Ni nn wanakufa kidogokidogo nimesoma topic nyingi na nimezifanyia kazi hapa lkn hata sijui tatizo Ni nn.
 
Kuna jirani yangu alikuja kuchuma Aloe Vera fresh kisha akaichanganya na maji akatwangatwanga akawapa kuku wake wakapona.
 
Dawa kila aina ndio zipi? Ungetaja baadhi tungekusaidia ila yaweza kuwa uliruka chanjo gumboro? Au fowl typhoid huwa haina sign zinazoeleweka. Nakushauri uliza broad spectrum antibiotic kama tylosin, ganadexil au keprocyl. Wakipona wachanje kama bado
 
pamoja na yote, kuna kitu unatakiwa kukijua. subiri nitakueleza hivi punde...
 
TUANZIE HAPA:
kwa magonjwa ya kuambukiza (infectious diseases): ili ugonjwa utokee au uendelee kuwepo kwa mnyama, ni LAZIMA mambo matatu yafuatayo yawepo kwa pamoja,
1. Vijidudu sababishi (infective causative agents) mfano bakteria, virusi au protozoa.
2. Mnyama athirika (susceptible host) hii inaeleza mnyama gani anaweza kuumwa ugonjwa gani, kwa maneno mengine ni kwamba hata iweje ng'ombe hawezi kuumwa malaria. (since it is not a susceptible host of plasmodium that causes malaria)
3. Mazingira murua ya ugonjwa kutokea au kuendelea kuwepo (favourable environment for a disease to occour or persist). Hii inajumuisha hali ya hewa, lishe, hali ya usafi, makazi, menejimenti n.k.
SASA BASI, inawezekana wewe unatibu kuku wako lakini bado hauwaondoi kwenye hayo "mazingira rafiki ya ugonjwa", (unajitibu tayphoid halafu unaenda kunywa maji machafu).
ZINGATIA: chanjo kwa wakati muafaka, tiba sahihi ya ugonjwa husika, lishe bora, banda bora, menejimenti nzuri ya kuku wako, n.k
ASANTE.
 
Back
Top Bottom