Kulala mchana

Runner

Member
Joined
Feb 7, 2011
Posts
85
Reaction score
13
Habari wana JF,Wapendwa naomba msaada wenu kwenye hili tatizo linalonitatiza,imekuwa ni wiki sasa huwa napatwa na usingizi mzito sana ifikapo saa nne asubuhi,yaani iwe nimewahi kulala usiku au nimechelewa lakini ikifika muda huo kwa kweli huwa napata shida sana hata kufanyakazi,na si saa nne tu bali na saa kumi jioni.Katika nyakati hizo mbili kweli jamani huwa nateseka sana na huo usingizi mzito,lakini ikishapita muda huo usingizi unapotea kabisa kama vile sikuwa na huo usingizi.Naomba mwenye ufahamu juu ya hili anipe elimu,ni tatizo gani?nateseka sana jamani
 
Pole Mkuu, Kwa saa nne asubuhi kupatwa na usingizi itakuwa ni sababu ya chai ya rangi unayokunywa nyingi tena ya moto halafu unasindikiziaga kitafunwa kigumu kama vile mkate, kwa saa kumi jioni hii inatokana na kwamba mchana unakuwa umekula chakula kingi sana na kama kawaida wewe ni mvivu sana kunywa maji. Hii ni kwa mjibu wa vipimo vyangu hapa.

Kulala mchana si TATIZO, mimi huwa napenda ikifika saa tisa hivi nipumzike japo nusu saa sema sasa nafanya biashara ya umachinga hivyo inashindikana maana la sivyo kesho yake nitakosa hela ya kununulia supu.

Jaribu hivi: Unapokujia tu usingizi muda si wenyewe, chukuwa maji kama lita moja hivi (Tahadhari angalia afya kama inaruhusu, usije ukaanguka bure), kunywa maji hayo kwa pamoja jitahidi yawe katika joto la kawaida/room temperature, ukishayanywa tembeatembea kidogo.

Jitahidi pia kupunguza vinywaji vyenye kaffeina; chai ya rangi, kahawa, soda, rdbull, malta, nk. Ongeza mazoezi ya mwili.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…