Kulazimisha kuwategemea Zimbwe na Kapombe/Kijiri wapige Cross kama Pre-assist au Assist vinachangia kuiporomosha Simba

Kulazimisha kuwategemea Zimbwe na Kapombe/Kijiri wapige Cross kama Pre-assist au Assist vinachangia kuiporomosha Simba

SankaraBoukaka

JF-Expert Member
Joined
Jul 2, 2019
Posts
1,213
Reaction score
1,918
Nimekuwa nikifuatilia huu mfumo unaochezwa na Simba sasa wa kuwategemea mabeki wa pembeni waje kutengeneza nafasi kwenye kufanikisha mashambulizi pale na kushuhudia unavyotufelisha kwa sasa. Kwasababu:

  1. Zimbwe tokea enzi hizo ni mbahatishaji kwenye kupiga cross sahihi na pasi za mwisho, na hizo cross mara nyingi anajibutulia tu mpira. Amechangia kupoteza mipira mingi ambayo kama ingetumika sahihi ingechangia Simba kufanya vizuri.
  2. Kapombe amepoteza ufanisi kwenye kusaidia timu kushambulia. Misimu iliyopita alipokuwa kwenye ubora wake aliifanya vizuri sana kutengeneza magoli kwa kupiga cross zenye macho haswa zile "V-PASS" na hata kufunga magoli mfano alipokuwa AZAM FC alifunga magoli mengi kupitia mfumo wa 3-5-2. Lakini kwa sasa Kapombe si yule tena, maana nguvu zinapungua kutokana na umri unavyoenda, ukizingatia kuwa mfumo huo wa kusaidia kwenye kushambulia na kukaba unahitaji utimamu mkubwa wa mwili na misuli yake katika kukimbia kufanikisha matukio yote hayo.
  3. Kijiri yeye atakupa mibio mingi sana ila kama kawaida yake pasi ya mwisho ni mgogoro mkubwa tena sana.
Kiukweli kulazimisha mabeki wa pembeni Simba kupanda kusaidia mashambulizi halafu viungo wa pembeni akina MUTALE na BALUA waingie ndani ni kulazimisha vitu ambavyo havitokuja leta faida yoyote.

Maana kuna muda unawakuta MUTALE, MUKWALA NA BALUA wanakimbia kuelekea kwa mpinzani lakini wamejikusanya sehemu moja na pembeni kwenye FLANKS hakuna mtu, kwahiyo washambuliaji wamejikusanya sehemu moja kiasi kwamba viungo wa kati akina AHOUA wanakosa option za kusambaza mpira na mwishowe tutawaona magalasa.. Na hata pasi zikienda huko pembeni zinaishia kupotezwa tu.

Kwanini kocha asiwaache MUTALE na BALUA wacheze kwenye mapana ya uwanja ambako ndo NAFASI ZAO ASILIA wafanye timu ifunguke iwe na uwanja mpana wa kusamba mpira halafu MUKWALA akae kati na nyuma yake wakae AHOUA kama na AWESU au FERNANDEZ???? Halafu akina ZIMBWE na KAPOMBE wakawa na jukumu kubwa haswa la kuzuia..

WACHEZAJI NDO WANATENGENEZA MFUMO KWA MUDA HUO ULIOPO NA SIYO KULAZIMISHA VITU AMBAVYO HAVIWEZEKANI...

MFANO WAKATI WA KUSHAMBULIA TIMU IKAWA NA MWONEKANO HUU HAPA CHINI SI TUTAUPIGA MWINGIIIII!!!!!

1723811513843.png
 
kapombe and hussein hadi alot of position loss due to crosses.

I thought people saw that.

also wingers are pointless in modern football unless they are far wide deeper and very fast in transition. other than that bora usiwe nao.
 
Msimu huu tunaweza tusiruhusu sana magoli kama msimu uliopita, lakn huenda tukafunga magoli machache sana. Yaan Droo zitakuwa za kutosha, maana safu ya ushambuliaji ni butu sana. Ku-defend ndo tupo vizuri.
 
Mimi pia nililiona hili siku nyingi,na nadhani hii ndio sababu kubwa ya simba kushindwa kupata magoli,mara nyingi cross zikipigwa pale mbele unakuta watu wamejikusanya kwenye box wanabana sana uwanja,hii muda mwingine hupelekea cross kupotea tu,au wapiga cross Kurudisha mpira nyuma.
 
Msimu huu tunaweza tusiruhusu sana magoli kama msimu uliopita, lakn huenda tukafunga magoli machache sana. Yaan Droo zitakuwa za kutosha, maana safu ya ushambuliaji ni butu sana. Ku-defend ndo tupo vizuri.
Hili naliona kabisa
 
Ni kweli bado simba haijatibu eneo la WINGBACKS ..bado naamiangakua KOCHA nini ameongeza SIMBA. ..timu na kocha nani anambeba mwenzake
 
Umechanbua vyema , Kijili kabla hahaha Simba mbovu kwenye basi za mwisho anaweza kutoka nduki vizuri akifika kwenye kufanya maamuzi yanakuwa ya hovyo asilimia kubwa .
 
Simba haichezi kutafuta kufunga bali ina possess tu Mpira, angalia pasi za Yanga kwenye goli waliloifunga Simba utajifunza tofauti ya timu hizi mbili na namna zinacheza!

Simba haina mido kama Aucho au Mudathir wanaopiga pasi za mwisho za mpenyezo.

Simba haina Boka au Yao wanaomwaga maji kwenye flanks

Simba haina Pacome au Max wanaopasua ngome ya wapinzani kutokea katikati.

Tatizo la Simba ni kubwa sana, haliishii kwenye upigaji wa krosi tu bali uwezo wa timu kutengeneza nafasi za kufunga kutokea pembeni na katikati. Timu nzima ya Simba ni mbovu , si sahihi kulaumu Zimbwe na Kapombe. Timu haina morali, na muunganiko ndo bado kabisaaaa!
 
Back
Top Bottom