Kulikoni Ofisi za ATCL Mwanza?

Kulikoni Ofisi za ATCL Mwanza?

Koryo2

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2016
Posts
2,056
Reaction score
2,519
Leo nimebahatika kufika Ofisi ya ATCL Mwanza kwa ajili ya booking. Niliyoyakuta pale haileti hadhi kuwa ile ni ofisi ya ATCL.

  1. Kihadhi kwa kweli ofisi imechoka mbaya. Ofisi haikupakwa rangi kwa kweli muonekano wa nje ni chafu.
  2. Nilipoingia ndani nimewakuta watumishi watatu. Nimewakuta hawana kazi kabisa mmoja alikuwa anaendelea tu kuchat kwa simu. Sijui ni hali siyo nzuri, wananchi hawana hela mfukoni.
  3. Mbaya zaidi hawakuwa na uniform inayomtambulisha kuwa huyu ni mtumishi wa ATCL. Kila mmoja alikuwa na sare iliyo tofauti na wenzake hii ina maana kila moja alivaa alivyopenda.
Kwa kawaida ATCL wanatakiwa watumishi wao wawe na sare na wawe wasafi na sifa za ziada kama yalivyo Mashirika mengine.

Uongozi fuatilieni na muimarishe ofisi ya Mwanza iwe na hadhi kama ofisi ya ATCL.
 
Wapo active pale airport. Nenda airport
 
Wa kufuatilia wameshachomolewa fuzi, Sasa hivi ni Bora liende😠!
 
Nidhani unaongelea bei ya tickets za ndege kutoka mwz hasi Dar, eti uniform eti ukuta hauna ragi, ujinga kabisa.
 
Kwa hapa bongo huduma zinazopatikana mtandaoni hua sijihangaishi kabisa kwenda kwenye maofisi yao.

Kwenye suala la huduma kwa mteja haswa kwenye masirika ya serikali bado tupo nyuma sina. Mhudumu anaweza kukupa majibu mpaka ukajiuliza wewe ni mteja au umeenda kuomba msaada.

Ni bora nipambane na maudhi ya mtandaoni kuliko kupambana na maudhi na dharau za wahudumu wa kibongo.
 
Kama na ndege huko ndani bado zilikua chafu basi tatizo litakuwa kubwa sana.
 
Nimeangalia hii review ya Sam Chui ambaye nadhani ameshapanda ndege za biashara karibu mashirka yote duniani. Ameipenda sana Rwandair, sijui lini atapanda ATCL.

 
Atcl pamoja na mengine yaliyofufuliwa yalizikwa. Mwaka Jana chato...
 
Kwani unifomu huvaliwa na nani na sare huvaliwa na nani? Watumishi watatu ni sawa na vyeo vitatu lazima watatofautiana kimavazi, mfagizi, mkata tikiti na meneja hawawezi kuvaa sawa.
 
Booking Fanya Online fasta, acha ushamba wa kupoteza mda
 
Back
Top Bottom