Kulingana na uzoefu wangu kwenye masuala ya mpira, Taifa Stars bado ina nafasi kubwa tu ya kufuzuKkombe la Dunia

Maghayo

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2014
Posts
20,307
Reaction score
47,210
Mzuka wanajamvi!

Ni hivi mechi ambayo inaendelea sasa hivi Benin na Madagascar ni 1-0 Benin wanaongiza na wako mapumziko.

Hapa kinachohitajika siyo kingine kila atakayesoma huu uzi ajikite kwenye maombi makali sana wakirudi kipindi cha pili Madagascar iifunge Benin magoli mawili ama watoke sare.

Endapo Madagascar itashinda basi Benin itabaki ya tatu kwenye table na point 7 na endapo Benin watadraw na Madagascar watakuwa na Point 8 ambayo siyo mbaya kivile kwetu.

Lakini Benin akishinda mechi ya leo inabidi taifa lote tuzidishe maombi makali sana miujiza itokee.

Mungu tusaidie Madagascar iifunge Benin leo. Halafu jumapili Congo watoke sare na Benin. Halafu timu yetu kipenzi taifa stars jumapili iifunge Madagascar kwa kushinda mechi.

Kulingana na uzoefu wangu wa mpira bado taifa stars ina nafasi kubwa sana ya kufuzu kombe la dunia. Kwasababu gani nasema hivi tuna Mungu. Tulianza na Mungu na tutamaliza na Mungu na jumapili jioni table itasomeka hivi

Timu Pointi
TAIFA STARS : 10
Congo. : 09
Benin. : 08
Madagascar : 06

Senior JF local and International sport correspondent and analysist.

Masters!
 
Unaota wewe
 
Vitu vizito vitatu vimetupiga kichwani tulipokuwa kwenye maombi tumechoka mtupumzishe sasa..😂
 
Watanzania wengi sisi ni mbumbumbu sana! Ina maana Mwenyezi Mungu hana kazi zingine anasubiriga maombi yenu tu! Basi tambueni alishawapuuza siku nyingi! Hamna mipango, na wachezaji wenu ni vil.aza wasiokuwa na ndoto kubwa maishani!
Nyie shabikieni Simba na Yanga na uchawi wenu wa kijinga ndo mnaweza!
Sehemu zinazohitaji akili,ushindani na ndoto kubwa kaeni pembeni!
 
This thread has been overtaken by events.
 

Pumba tupu
 
Aisee, madaktari wa Mirembe mgonjwa wenu mmemuachia Smart Phone anachart jf!
 
Yaani ili twende world cup tunashabikia hadi timu ya madagascar na congo?Aisee, madaktari wa Mirembe mgonjwa wenu mmemuachia Smart Phone anachart jf hahahahaha!
 
Sikuelewi!
Kitimoto nilipenda comment yako kwake nikakuunga mkono kuwa ametoroka,nimecheka hadi nimepaliwa!Samahani kwa kukuibia comment it is my best comment ever for a lunatic like Maghayo,na akiendelea kuachiwa azurure kama hivi lazima atadhuru mtu au atajidhuru!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…