Kumbe Kamati za Bunge zina nguvu sana. Hayati Magufuli alikuwa anasema kila anachofanya kimepitishwa na Bunge watu wakabisha. Ahsante Nape Nnauye!

Kumbe Kamati za Bunge zina nguvu sana. Hayati Magufuli alikuwa anasema kila anachofanya kimepitishwa na Bunge watu wakabisha. Ahsante Nape Nnauye!

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Jana baada ya kumsikiliza kwa makini Waziri Nape pale Clouds TV ndio nikaelewa kwanini hayati Magufuli alikuwa anasema mambo yote anayofanya bunge linayajua na limeyabariki.

Nape alisema kamati za bunge ndio hufanya kazi zote za msingi na mwisho hukubaliana na kutoa maoni ya pamoja.

Kwa mfano ununuzi wa ndege kamati husika ya bunge kama ilitaarifiwa na kuafiki hapo ni bunge limeafiki hata kama Chadema wabunge wao watajifanya kupinga pinga baadae.

Kwa Tanzania ni ngumu sana serikali kujiamulia kufanya jambo lolote bila baraka za bunge na hii ni tangu enzi za mfumo wa chama kimoja.

Yaani Serikali inunue ndege zaidi ya 10 bila akina Tundu Lisu kujua na kupitisha pale bungeni? Isingewezekana kabisa bwashee.

Maendeleo hayana vyama!
 
aache uongo kamati ya bunge ikifanyia kazi kitu lazima kiwasilishwe bungeni ,bunge likiafiki ndio inakuwa hiyo ishu imepitishwa
 
Jana baada ya kumsikiliza kwa makini Waziri Nape pale Clouds tv ndio nikaelewa kwanini hayati Magufuli alikuwa anasema mambo yote anayofanya bunge linayajua na limeyabariki...!
ameanza kuharisha kama kawaida yake. Nape ni wa hovyo sana. Ndiyo maana hata jpm alimtimua serikalini
 
aache uongo kamati ya bunge ikifanyia kazi kitu lazima kiwasilishwe bungeni ,bunge likiafiki ndio inakuwa hiyo ishu imepitishwa
Hujiulizi kwanini kikifikishwa bungeni wanaopewa fursa ya kuchangia karibia 90% ni wajumbe wa kamati husika?

Kwa mfano Msukuma juzi alivyojifanya anamchana Waziri Makamba jr kumbe ulikuwa usanii mtupu kwenye kikao cha kamati aliunga mkono!
 
Huyu waziri ameanza kudemka kama kawa yake!
Ameshasahau alikotoka sababu ya uwaziri tena!
 
Magufuli was the best.

Ni propaganda tu za mabeberu na vibaraka wao pamoja na Watanzania wapigaji ili kumchafua.

Hata hivyo wazalendo tupo naye kwenye uhai na kifo. Apumzike kwa amani mbinguni.
 
Magufuli was the best.

Ni propaganda tu za mabeberu na vibaraka wao pamoja na Watanzania wapigaji ili kumchafua.

Hata hivyo wazalendo tupo naye kwenye uhai na kifo. Apumzike kwa amani mbinguni.
Amina!
 
Naanza kumpenda magufuli Bila sababu yoyote nikitizam clipu zake bas naingiwa na huruma San kwamba tumempoteza kiongozi mahiri San San kwamba itatuchukua muda sna aje mtu Kama magufuli tena kwa ukali na ubabe wake Bila kujali Sheria yoyote ile kila mtu alifyta mkia kipindi hcho .Nchi nzima ilitulia tuli.

Siyo jaji ,siyo spika ,siyo wanajeshi hata mkuu wa jeshi alitulia kimyaa .kila mtu alitulia kimyaa dadeki walai hakuna aliweza kupandisha kichwa juu kipindi hcho akabakia salama

Alitumia hii kauli ya Paulo kagame
Kwamba "uwezi kudharau rwanda ukabakiaa salama "hivyo hvyo magu naye aka apply hiyo staili na ilimsaidia snaa tu
 
Jana baada ya kumsikiliza kwa makini Waziri Nape pale Clouds TV ndio nikaelewa kwanini hayati Magufuli alikuwa anasema mambo yote anayofanya bunge linayajua na limeyabariki.

Nape alisema kamati za bunge ndio hufanya kazi zote za msingi na mwisho hukubaliana na kutoa maoni ya pamoja.

Kwa mfano ununuzi wa ndege kamati husika ya bunge kama ilitaarifiwa na kuafiki hapo ni bunge limeafiki hata kama Chadema wabunge wao watajifanya kupinga pinga baadae.

Kwa Tanzania ni ngumu sana serikali kujiamulia kufanya jambo lolote bila baraka za bunge na hii ni tangu enzi za mfumo wa chama kimoja.

Yaani Serikali inunue ndege zaidi ya 10 bila akina Tundu Lisu kujua na kupitisha pale bungeni? Isingewezekana kabisa bwashee.

Maendeleo hayana vyama!
Shida ni kuwa kuna maamuzi ambayo hata Spika alijiuliza kama kweli yalipita kwenye Bunge lake!

Amandla...
 
Kwa mfano ununuzi wa ndege kamati husika ya bunge kama ilitaarifiwa na kuafiki hapo ni bunge limeafiki hata kama Chadema wabunge wao watajifanya kupinga pinga baadae.

Kwa Tanzania ni ngumu sana serikali kujiamulia kufanya jambo lolote bila baraka za bunge na hii ni tangu enzi za mfumo wa chama kimoja.
Je hao wabunge huwa wanawasilisha mawazo waliyotumwa na wananchi kweli au huwa ni mawazo yao binafsi? Wananchi wanasema wanahitaji barabara nzuri, shule nzuri, vituo vya afya na dawa, maji salama, lakini Kamati inasema wananchi wanahitaji ndege
 
Back
Top Bottom