Kumbe Kuna Ofisi Maalum ya Serekali Ambayo Huchapisha Ripoti za bajeti Ilivyotumika !?

Kafrican

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2015
Posts
7,251
Reaction score
7,037
Mara nyingi hua naisikiza na Kuisoma Hotuba ya Wizara ya Fedha, lakini hua nashindwa kuchambua haswa vipi pesa zitatumika, manake katika ile hotuba hua ni wizara kadhaa tu zinatajwa na kutangazwa kama zimepewa pesa ngapi lakini hata hawasemi hizo pesa zitatumika kufanya nini haswa.
Yani hua sina budi ila kusikiza tu hotuba na kutoka hapo unapata mawili matatu kuhusu wizara mbili tatu..... Nilikua sijui kumbe kuna ofisi ambayo imepewa malaka ya kikatiba kutoa ripoti ya vipi bajeti ilivyotumika. Yani wizara ya Fedha inatoa hela na mpango wa matumizi, lakini hii ofisi ndo inapima hio bajeti kama ilitumika au la na mwisho wa kila miezi mitatu inatoa ripoti kuhusu maatumizi ya bajeti katika serekali kuu na za county.




Mamlaka ya kikatiba
Article 228.


Katika ripoti ya 2018/19 nitaanza na matokeo yake hapo mwisho wa hio ripoti, Hio ripoti inaonyesha ni asilimia 7.6% ya bajeti ya maendeleo ilitumika kwa miezi mitatu ya kwanza, na 38.8% kwa miezi sita ya kwanza... Yaani kwa kifupi, hii pesa ilikua imekaa kwa benki ya Wizara ya Fedha, Wizara zengine na County zilikua zinakula mishahara tu lakini hakuna kazi yeyote ya kimaendeleo walikua wanafanya.




















Walimu wanakula mishahara duh!




Hapa tunaona Wizara ya elimu ilipewa bajeti ya $4.6B lakini mwisho wa mwaka ilikua imetumia $4.38, Wizara ya Afya ilibajetiwa $920 million lakini ilitumia $760m pekee na hizo zengine zikarudi kwa benki badala ya kufanyiwa kazi!
Alafu wizara ya kilimo nayo inapewa pesa kidogo sana, Hapo inafaa wizaratatu zinazopokea hela nyingi ianze na Elimu, ifwatwe na miundombinu alafu biashara kilimo....






Madeni ya mwaka 2018/19 nayo yalikuwa $8.26B lakini Serekali ililipa $8.2B ikiwa ni asilimia 95%








Huko kwengine wanaenda kiundani zaidi na kuchambua ofisi moja moja kwa undani... kama mtu anataka kujisomea nimeiweka PDF hapo chini na pia link ndo hii
 

Attachments

1/2 of Budget Money (Over Ksh 1.4Trn) comes from Loans/Grants while 90% of the total budget is spent on Recurrent exp & salaries.
SIMPLY: Kenya is borrowing to pay salaries, buy office office supplies & Office tea
 
Dah! Jamaa wewe huwa mkali sana kwenye kufuatilia na kudadavua haya mavitu, hapa umenipa elimu pia, asante. Wacha niendelee kubambua hizi nondo, japo kitu hunisikitisha ni kwa serikali yetu kuendelea kutumia MTEF budgeting ambayo ni dhaifu kiufanisi, japo pia kuna taasisi na wizara ambazo zimefaulu kuanza kutumia PBB.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…