Nimebaini kuna idadi ya walimu wanaofanya kazi ya kuendesha pikipiki(boda boda) ili kuingiza kipato. Ayo nimeyabaini wiki iliyopita musoma baada ya kukodi pikipiki na kubaini dreva wangu ni mwalimu by proffesional.Baada ya kumdadisi kwa undani akanieleza wapo si chini ya walimu 9(primary na sekondari) wanaofanya kazi ya bodaboda, na sababu kubwa ni kipato kidogo wanachopata kwenye mishahara yao.
Na sgughuli iyo imekuwa ikifanyika ata muda wanaokatakiwa kuwepo madarasani.
Je kuna mwanaJF mwenye kujua kuhusu lolote kwenye mikoa mingine?
Maskini waalimu wamekuwa
yatima sana hii nchi,alafu mnakaa mnapiga hesabu waalimu watoe div1,2,3?
..kalagabao bwana.
ishu siyo kumiliki boda boda,ni kuwa dreva wa iyo boda boda kuendesha biashara ata wakati wanatakiwa kuwa madarasani kufundisha,NB rudia kusoma thread line by line utaelewa.kwani n dhambi huyo mwalimu kumilk Bodaboda?
Nimebaini kuna idadi ya walimu wanaofanya kazi ya kuendesha pikipiki(boda boda) ili kuingiza kipato. Ayo nimeyabaini wiki iliyopita musoma baada ya kukodi pikipiki na kubaini dreva wangu ni mwalimu by proffesional.Baada ya kumdadisi kwa undani akanieleza wapo si chini ya walimu 9(primary na sekondari) wanaofanya kazi ya bodaboda, na sababu kubwa ni kipato kidogo wanachopata kwenye mishahara yao.
Na sgughuli iyo imekuwa ikifanyika ata muda wanaokatakiwa kuwepo madarasani.
Je kuna mwanaJF mwenye kujua kuhusu lolote kwenye mikoa mingine?
sasa hapo kuna masomo tena?Kiongozi upo sahihi kabisa, baada ya Serikali kuwawezesha mishahara yao ipitie NMB basi wakawa wanakopesheka, wengi wao walipokopa wakaingia kwenye hiyo biashara inawalipa kwa kweli ingawa upande wa pili unaathirika
Afadhali ya hawa walimu mi naona wana a kili sana.Kuna watendaji wengi wa serikali muda wa kazi utawakuta bar au madanguro ofisini hawpatikani. Mi kwa mtizamo wangu jamii na serikali isitafute namna ya kuwabana walimu ili wafundishe bali iifanye kada ya ualimu kuwa kada ya kukimbiliwa badala ya kukimbiwa.
Kwenye mkoa wetu mimi kuna shule waalimu wote 11 ni boda boda
sahihi kabisa.usiwe mwizi tu.kila kitu kimepanda bei kwa kasi kubwaMm pia ni shahidi wa hilo, mwaka jana nlkuwa mkoa wa mbeya, wilaya ya rungwe maeneo ya kiwira, dereva bodaboda nilyopanda ni mwl wa shule moja ya kata palekiwira, nilipobain kuwa driver ni ticha nikahoji kulikon saa 7 mchana upo hapa badala ya shulen? majibu yake yalikuwa hivi.
1: mimi ni mwl sawa lakin si muda wote natakiwa kuwepo darasani, kuna muda wawanafunz kujisomea.
2: kwa siku nina vipindi 2-3 nachofanya nafundisha asubuh kimoja au viwili na baada ya break(saa 6) nakuja kujishughulsha na bodaboda, maisha haya bila shughuli za pembeni hutoki, kila kitu bei juu laki nne haitoshi.
KWA HILI nawaunga mkono kwan ukipiga hesabu ya bidhaa za ndan kama sukari, unga,bili ya umeme, bili ya nyumba, mavazi, matibabu nk. laki nne mizinguo wanapiga na issue zingine kwa sababu serikali haina uwezo wa kuwaongeza mishara basi acheni wajiongezee wenyewe.
ishu siyo kumiliki boda boda,ni kuwa dreva wa iyo boda boda kuendesha biashara ata wakati wanatakiwa kuwa madarasani kufundisha,NB rudia kusoma thread line by line utaelewa.
sasa hapo kuna masomo tena?
Ndo maana watoto sasa wanafeli, serikali ingewajali si nao wangejali kazi yao