Kumbe Michuzi Photopoint sio ya kwake!!!

Wabongo bwana.....keroooo
Someni MICHUZI
BTW Michuzi nampa 5 na anazidi kupiga bao tu mixa makitu kama haya
 

Attachments

  • 111.jpg
    31.6 KB · Views: 291
...wabongo bwana, ukute wengine walikuwa hata hawajazaliwa mjasiriamali huyu alipokuwa anabangaiza,


...Kama Mzee Vicent Urio (R.I.P) aliweza miaka hiyo kwanini michuzi asiweze? au wenye uwezo wa kuwa na studio ni kina Hassan mpiga picha tu?
 
Sio Michuzi tu,wako wengi wengine.Anza na IPP ,vituo vya radio,sijui Clouds nk.,Radio Free Africa,Star TV,Channel 10 na biashara nyingine nyingi.Unao waona ni day waka tu.Wenyewe wapo,nchi za magharibi.Na ina wezekana hata hao waliokabidhiwa hizo biashara hawajui zipo kwa ajili gani,wao wanapata maslahi yao basi wameridhika!Ni kama mtu aliyepanda gari kwenda Dar lakini hajui anakwenda kufanya nini,nawahurumia sana.
Ndugu yetu amekuwa akisema yeye ni mmoja wa wamiliki wa zile sehemu za kupigia picha na mpaka gari lake lina "poster za photo point" inasemekana yeye wala hausiki kabisa na photopoint, yeye ni kama deiwaka vile. Kama yumo humu atueleze basi
 



Mkuu hii thread ingeanzishwa na superstars wa kuchangia kashfa na maneno ya kejeli usinge yaona ungeona tu data zinamwagwa tu.
Ila kwa vile jamaa amegusa penyewe watu wamekuwa mbogo humu ''MKuki kwa .............''Jamaa ana washabiki wengi sana humu JF mmegusa sio penyewe.
 
Sio kwamba jamaa ana washabiki wengi humu bali Michuzi anakubalika. Sio lazima kuwa mshabiki kumtetea mtu ila its just appreciation of what he does and not what he has.
 
Akueleze wewe na nani?
Sasa yeye akiwa deiwaka au mmiliki inakuhusu nini?
Alishawahi kukwambia ni ya kwake?
Huu ndio upashkuna, acha kujadili vitu vya watu, jifunze utu kidogo....

Great minds discuss ideas simple minds discuss people!!!
 
Photo Point sio ya Michuzi yeye ni kama technical manager na ameajiriwa. PP ni ya mtoto wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Usalama wa taifa A. Mwangond'a aitwaye Samuel Apson. Michuzi ni paparazi tuu.
 
sijui Clouds nk.,

- Hii ya Clouds haihusiki na hizi nyepesi nyepesi maana ni ngoma kubwa mno, tumemuona Joe akianzia na vyombo vya nyumbani pale Motel Agip, mpaka kununua vyombo vya kweli na kuhamia Leaders Club, baada ya kupanuka sana ukaja mchezo wa kisasa wa wawekezaji kina Ruge, lakini ukweli uko pale pale kwamba Joe is the man.

- Michuzi ni Michuzi tu kumiliki au kutomiliki kwake anything hakumfanyi awe less au more of Michuzi, toka day one nimemjua mjini yuko vile vile, Michuzi ninamkumbuka akianzia YMCA Disco Toto anatupiga picha bure, jina Michuzi halijawahi kuwa associated na materialism au what the man owns, kama kina RIP Marcochella, Wandiba, Joe Holera Johnson, Gerry Kotto, Chris Faby, JPP, Choggy, Kali Kali, Super Deo na wengine, Michuzi comes from this line ya ubaharia wa nchi kavu na he deserves a big respect kwa kuweza kusimama kidete hadi leo na besides the man is got to do what the man he got to do. Michuzi ni survival pia ni mfano wa kuigwa na wengine, maana hata bila ya hiyo PP bado Michuzi atakuwa ni Michuzi tu, kumbuka kuishi mjini sio lelemama.

Tuwe na wivu wa kimaendeleo wakuu, sio kushushana shushana hata sisi masikini haifai!

Mungu Ambariki na Kumzidishia Mkulu Michuzi na aendele kuwa mfano kwa wengine.
 
Mod, nashauri uifunge hii thread maana muulizwa swali keshapata jibu. Michuzi ataendelea kuwa Michuzi, kazi yake rasmi ni photographer, wadhifa wake ndiye mpiga picha mkuu wa magazeti ya serikali ya Daily News na Habari leo. Extra Caricular yake ni host wa one of the most popular blog ya kibong
Pia ni mmiliki wa gazeti la Kita Ngoma. Amiliki asimiliki PP sio issue, heshima ya balozi huyu bado iko pale pale. Kama lengo lilikuwa kumshusha itapobainika PP siyo yake, jamaa bado yuko
Juu.
 
Ndugu yetu amekuwa akisema yeye ni mmoja wa wamiliki wa zile sehemu za kupigia picha na mpaka gari lake lina "poster za photo point" inasemekana yeye wala hausiki kabisa na photopoint, yeye ni kama deiwaka vile. Kama yumo humu atueleze basi


Jamani Michuzi ni celebrity wa bongo yetu hii. Ndo maana watu watafuatilia mpaka the so called personal issues. Mi nadhani mnaoishi majuu you know better. Ukishakuwa celebrity hata shati utakalolivaa watu watajadili rangi yake, hata simu ya kiganjani unayoitumia watu wataijadili.

Kwa hiyo sioni ubaya na hii thread ni ile tuu ya kujadili celebrities wetu. Ofcourse wengi watasema ni mambo binafsi..lakini..ukishaingia kwenye maisha ya kuwa attraction ya umma..basi ujue kabisa, umeaga maisha ya binafsi (private life)...people will follow you from where you sleep to where you play golf (if you do)

Mtu kama Michuzi ana the most popular blog Tanzania nzima (ofcourse JF being an exception)..sasa kweli unataka watu wasimjadili?

Sidhani kama jamaa aliyeianzisha hii thread alikuwa na chuki binafsi dhidi ya Muungwana Michuzi. Michuzi ni celebrity bana..ohh....au mnataka tuwajadili akina Puff Daddy, Oprah na wengineo wa majuu tuu? Hata Michuzi anastahili bwana...Infact inabidi mtuambie michuzi anaendesha gari gani na anatumia simu gani.. ;-)
 
...MICHUZI is a brand,

...brand is a tangible product, jamaa alianzia kupiga picha mitaani leo hii ukisikia MICHUZI huulizi product zotokanazo na brand MICHUZI, kuanzia picha kwenye blog yake, mpaka picha zinazopigwa kwenye studio zake, hata kama yeye hakuhusika...

hata kama photopoint si ya michuzi, brand MICHUZI inaendelea kuwa associated na photopoint, kwa mtaji huu anacholipwa/anachojilipa ibakie ni siri yake!
 

mkuu ulitaka kusema intangible au?
naamini kitaalamu brand ni intangible asset
na kwa hali ilivyo michuzi angeenda kwa wataalamu wa
brela aombe ushauri wa kulifanya hilo jina a trademark
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…