Kumbuka Rais Samia kabla hujawa Rais hukuwa na chawa hata mmoja

Kumbuka Rais Samia kabla hujawa Rais hukuwa na chawa hata mmoja

AbuuMaryam

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2015
Posts
2,577
Reaction score
4,637
Laiti ningepata nafasi ya kukutana na wewe, ningekupa nasaha zangu kama 3 ila sina uwezo huo nimeona niliseme hapa huwenda litakufikia na Utakumbuka ulikotoka. Ila bado naomba nafasi ya kukufikishia mengine yanayokuhusu wewe tu Rais wetu.

Mama yetu Rais wetu kipenzi... kumbuka ulipotoka mpaka Allaah akakupa hiyo nafasi sidhani kama uliwahi kufikiria kwamba ipo siku itakuwa rahisi wewe kuwa Rais wa nchi hii.

Ila Allaah kalifanya hilo likawa jepesi kwako na akakupa huu Urais...kipindi hiko ulikuwa huna hata CHAWA MMOJA.

Hakuna hata mmoja aliyekuwa anakutaja vizuri kama wanavyokutaja leo...na wengine walikuwa wanakudharau na kukupuuza na kukuweka mwisho mwisho.

Ila Allaah akakunyanyua na akakupa hii nafasi bila kutarajia...huyo ndio Mola wako.

Rudi kwa Mola wako Rais wetu tafuta Muongozo wa Mola wako msikilize aliyekupa hii dhamana akikusifu yeye inatosha.

Hawa chawa na wanaokupamba hivi leo wamedhihiri kipindi tayari Allaah amekupa haya madaraka walikuwa wapi kabla hujapewa.

Kama ambavyo hukuwa na chawa kabla hujawa Rais...na vilevile ukitoka kwenye urais watakukimbia wote...KUMBUKA HILI.

MWISHO KUMBUKA: ALIYEKUPA URAIS NI MOLA WAKO. NA ATAKAYEUFANYA URAIS WAKO UENDELEE KUWEPO NI HUYO HUYO MOLA WAKO...NA ATAKAYECHUKUA URAIS WAKO NI HUYO HUYO MOLA WAKO...HATA KAMA CHAWA WASIPENDE.

NAKUPENDA RAIS WETU MAMA...NAKUOMBEA DUA ALLAAH AKUHIFADHI NA AKULINDE NA KILA SHARI...ALLAAH AKUONGOZE...MAANA UKIONGOKA WEWE NCHI YETU PIA ITAONGOKA...
 
Yani hadi Maostaaadh wanakerwa na hii hali Mapadri pia baadhi yao wanakerwa na hii hali tunaenda wapi kama Taifa? Inakera na kuumiza sana ,maadili ya Nchi yanakufa sababu ya uchawa
 
Chawa kila mahali, hata mimi kazini nina chawa wangu.
 
Ujumbe mzuri sana natamani sana ungemfikia.

Hii hali iyopo leo sijui kama wanao husika na mustakabali wa nchi hii weridhia , kama wameridhia basi kama taifa safari ni ndefu mno .
 
Back
Top Bottom