Kumbukizi: Leo ni Miaka 21 tangu Marc Vivien Foe adondoke uwanjani na kufariki Dunia

Kumbukizi: Leo ni Miaka 21 tangu Marc Vivien Foe adondoke uwanjani na kufariki Dunia

Mchochezi

JF-Expert Member
Joined
Feb 29, 2012
Posts
10,962
Reaction score
7,830
Tarehe kama ya leo miaka 21 iliyopita Dunia ilimpoteza kiungo mahiri wa Man City na timu ya Taifa ya Cameroun, Marc-Vivien Foe.

Foe alidondoka uwanjani dakika ya 72 wakati wa mchezo wa Kombe la Mabara, kati ya Cameorun dhidi ya Colombia katika hatia ya nusu fainali ambapo michuano hiyo ilikuwa inafanyika Ufaransa.

Wakati Foe anadondoka hakuwa na mtu karibu yake alikuwa mwenyewe katikati ya uwanja. Chanzo ilikiwa ni tatizo la moyo. Watu wa matibabu waliingia uwanjani na kutumia karibia dakika 45 kujaribu kuokoa uhai wake lakini ikashindikana. Akapoteza maisha.

Kwa heshima ya Foe, Klabu ya Manchester City aliyokuwa Foe anacheza kwa mkopo, ikastaafisha jezi namba 23 na haitumiki tena klabuni hapo.

Marc-Vivien Foe akazikwa kitaifa huko kwao Cameroun katika mazishi ya kitaifa yaliyoandaliwa na serikali.

Marc-Vivien Foe ni miongoni mwa mashujaa kule kwao Cameroun.
 
Aisee nakumbuka niliangalia hii mechi kwa TV....R.I.P Champion.
 
Siku ya final ufaransa ilishinda dakika za jioni muda wa nyongeza kwa goli la aliyekuwa mshambiliaji machachali kwa wakati huo Henry na Rais wa fifa akaamuru kuwa kumbe lile like kameruni miezi sita kwani nao ni mabingwa wamecheza mechi ndani ya maombolezo
 
Tarehe kama ya leo miaka 21 iliyopita Dunia ilimpoteza kiungo mahiri wa Man City na timu ya Taifa ya Cameroun, Marc-Vivien Foe.

Foe alidondoka uwanjani dakika ya 72 wakati wa mchezo wa Kombe la Mabara, kati ya Cameorun dhidi ya Colombia katika hatia ya nusu fainali ambapo michuano hiyo ilikuwa inafanyika Ufaransa.

Wakati Foe anadondoka hakuwa na mtu karibu yake alikuwa mwenyewe katikati ya uwanja. Chanzo ilikiwa ni tatizo la moyo. Watu wa matibabu waliingia uwanjani na kutumia karibia dakika 45 kujaribu kuokoa uhai wake lakini ikashindikana. Akapoteza maisha.

Kwa heshima ya Foe, Klabu ya Manchester City aliyokuwa Foe anacheza kwa mkopo, ikastaafisha jezi namba 23 na haitumiki tena klabuni hapo.

Marc-Vivien Foe akazikwa kitaifa huko kwao Cameroun katika mazishi ya kitaifa yaliyoandaliwa na serikali.

Marc-Vivien Foe ni miongoni mwa mashujaa kule kwao Cameroun.
tulioina hii mechi LIVE hakika tumezeeka sasa...21yrs!!!
 
Back
Top Bottom