Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
KUMBUKUMBU YA MIAKA 50 YA KIFO CHA ABDUL SYKES
Ile kamati ndani ya kamati katika TAA ya Abdul Sykes, Ally Sykes John Rupia na Dossa Aziz walikuwa wameshakubaliana kuwa Nyerere lazima achukue ile nafasi ya rais na mwaka unaokuja 1954 wanaunda TANU. (Kamati kubwa ni ile TAA Political Subcommittee ya Sheikh Hassan bin Ameir iliyoundwa 1950).
Hii ni baada ya Abdul kutoka Nansio kwa Hamza Mwapachu na Hamza kumpa kauli yake kuwa Nyerere apewe uongozi na TANU iundwe 1954 udaiwe uhuru. Unajua Hamza kwa Abdul na Nyerere alikuwa ni mkubwa kwa kuzaliwa. Hamza kazaliwa 1913 na Nyerere 1922 na Abdul 1924. Angalia tofauti ya umri kati ya watu hawa. Kisha Hamza mambo haya kayajua mwanzo. Alikuwa kawazidi kwa kila hali. Inasikitisha sana kuwa historia imewaruka watu muhimu sana katika historia ya TANU na harakati za kupigania uhuru. Lakini jambo hili la kumwingiza Nyerere halikuwa la kutangazwa kila mwanachama akalijua kuwa sasa akina Abdul wanaunda chama cha siasa. Ilikuwa siri. Juu ya haya Denis Phombeah yeye hakuwa katika ile duru ya ndani kwa hiyo yeye akawa anamfanyia Nyerere kampeni amuangushe Abdul na Abdul akawa anamtazama tu hafanyi lolote kwani hicho ndicho kilichotakiwa. Juu ya haya Nyerere alishinda kwa kura chache sana katika uchaguzi ule. Tena uchaguzi huu ulikuwa wakionyesha mikono. Jambo la kusikitisha historia hii ni kama vile inatisha hata Nyerere mwenyewe hajapata kusema vipi alijuana na Abdul nini walikuwa wakipanga katika kuunda TANU nk. nk.
Kuna kitu kimoja muhimu sana. Unajua Abdul yeye alitaka Chief Kidaha Makwaia wa Siha aje TAA wamchague rais na kisha waunde TANU na mazungumzo haya yao hayakuwa na mafanikio ikawa kama vile Abdul amepwelewa ndipo Hamza akaja na jina la Nyerere. Lakini kama mwaka ule 1953 hii Inner Circle ya TAA ya akina Abdul wangefanya khiyana ya kumkataa Nyerere kwa sababu yoyote ile wangekuwa wamefanya kosa kubwa sana. Uhuru usingepatikana 1961. Abdul alikuwa amekifikisha chama pale alipolifikisha na hakuweza kukipeleka mbele zaidi ya hapo yeye akiwa kiongozi wa juu. Huu ndiyo wakati Earle Seaton akimsukuma sana Abdul aende Princeton University, New Jersey kusoma na admission letter alikuwa tayari anayo mkononi. Ukisoma Nyaraka za Sykes za 1953 utaona mambo yalikuwa mengi sana na hiki ndicho kipindi serikali ikitoa circular za kutisha. Huu ndiyo mwaka Kamati ya Saadan Abdu Kandoro, Japhet Kirilo na Abbas Sykes ilikuwa inazunguka Tanganyika kueleza dhulma za Ardhi ya Wameru. Abdul alikuwa karibu apoteze kazi yake ya Market Master Kariakoo Market.
Abdul alikuwa amekifikisha chama pale alipolifikisha na hakuweza kukipeleka mbele zaidi ya hapo yeye akiwa kiongozi wa juu. Huu ndiyo wakati Earle Seaton akimsukuma sana Abdul aende Princeton University, New Jersey kusoma na admission letter alikuwa tayari anayo mkononi. Nadhani unaona TAA ilikuwa kwenye stalemate.Hamza Mwapachu alikuwa mwamba unajua hapo alikuwa keshasoma medicine na kaacha kutibia akaenda University of Wales, Cardiff kusoma Social Science. Huyu ndiyo alikuwa hirizi yao hawawezi kumpinga walikuwa wanamuamini sana. Hamza wakati ule yeye anaandika makala katika gazeti la Sentinel za Fabian Society. Hawa Fabian ndiyo walikuwa siasa kali katika Labour Party ya Uingereza. Ninazo nakala za barua za miaka ya 1940 mwishoni Mwapachu akiandikiana na viongozi wa Fabian Society. Inasikitisha kuwa historia hii tulitaka kuicha ipotee bure.
Ile kamati ndani ya kamati katika TAA ya Abdul Sykes, Ally Sykes John Rupia na Dossa Aziz walikuwa wameshakubaliana kuwa Nyerere lazima achukue ile nafasi ya rais na mwaka unaokuja 1954 wanaunda TANU. (Kamati kubwa ni ile TAA Political Subcommittee ya Sheikh Hassan bin Ameir iliyoundwa 1950).
Hii ni baada ya Abdul kutoka Nansio kwa Hamza Mwapachu na Hamza kumpa kauli yake kuwa Nyerere apewe uongozi na TANU iundwe 1954 udaiwe uhuru. Unajua Hamza kwa Abdul na Nyerere alikuwa ni mkubwa kwa kuzaliwa. Hamza kazaliwa 1913 na Nyerere 1922 na Abdul 1924. Angalia tofauti ya umri kati ya watu hawa. Kisha Hamza mambo haya kayajua mwanzo. Alikuwa kawazidi kwa kila hali. Inasikitisha sana kuwa historia imewaruka watu muhimu sana katika historia ya TANU na harakati za kupigania uhuru. Lakini jambo hili la kumwingiza Nyerere halikuwa la kutangazwa kila mwanachama akalijua kuwa sasa akina Abdul wanaunda chama cha siasa. Ilikuwa siri. Juu ya haya Denis Phombeah yeye hakuwa katika ile duru ya ndani kwa hiyo yeye akawa anamfanyia Nyerere kampeni amuangushe Abdul na Abdul akawa anamtazama tu hafanyi lolote kwani hicho ndicho kilichotakiwa. Juu ya haya Nyerere alishinda kwa kura chache sana katika uchaguzi ule. Tena uchaguzi huu ulikuwa wakionyesha mikono. Jambo la kusikitisha historia hii ni kama vile inatisha hata Nyerere mwenyewe hajapata kusema vipi alijuana na Abdul nini walikuwa wakipanga katika kuunda TANU nk. nk.
Kuna kitu kimoja muhimu sana. Unajua Abdul yeye alitaka Chief Kidaha Makwaia wa Siha aje TAA wamchague rais na kisha waunde TANU na mazungumzo haya yao hayakuwa na mafanikio ikawa kama vile Abdul amepwelewa ndipo Hamza akaja na jina la Nyerere. Lakini kama mwaka ule 1953 hii Inner Circle ya TAA ya akina Abdul wangefanya khiyana ya kumkataa Nyerere kwa sababu yoyote ile wangekuwa wamefanya kosa kubwa sana. Uhuru usingepatikana 1961. Abdul alikuwa amekifikisha chama pale alipolifikisha na hakuweza kukipeleka mbele zaidi ya hapo yeye akiwa kiongozi wa juu. Huu ndiyo wakati Earle Seaton akimsukuma sana Abdul aende Princeton University, New Jersey kusoma na admission letter alikuwa tayari anayo mkononi. Ukisoma Nyaraka za Sykes za 1953 utaona mambo yalikuwa mengi sana na hiki ndicho kipindi serikali ikitoa circular za kutisha. Huu ndiyo mwaka Kamati ya Saadan Abdu Kandoro, Japhet Kirilo na Abbas Sykes ilikuwa inazunguka Tanganyika kueleza dhulma za Ardhi ya Wameru. Abdul alikuwa karibu apoteze kazi yake ya Market Master Kariakoo Market.
Abdul alikuwa amekifikisha chama pale alipolifikisha na hakuweza kukipeleka mbele zaidi ya hapo yeye akiwa kiongozi wa juu. Huu ndiyo wakati Earle Seaton akimsukuma sana Abdul aende Princeton University, New Jersey kusoma na admission letter alikuwa tayari anayo mkononi. Nadhani unaona TAA ilikuwa kwenye stalemate.Hamza Mwapachu alikuwa mwamba unajua hapo alikuwa keshasoma medicine na kaacha kutibia akaenda University of Wales, Cardiff kusoma Social Science. Huyu ndiyo alikuwa hirizi yao hawawezi kumpinga walikuwa wanamuamini sana. Hamza wakati ule yeye anaandika makala katika gazeti la Sentinel za Fabian Society. Hawa Fabian ndiyo walikuwa siasa kali katika Labour Party ya Uingereza. Ninazo nakala za barua za miaka ya 1940 mwishoni Mwapachu akiandikiana na viongozi wa Fabian Society. Inasikitisha kuwa historia hii tulitaka kuicha ipotee bure.