Kumbukumbu ya safari ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere UNO 1955

Kumbukumbu ya safari ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere UNO 1955

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
1564977969400.png

Safari ya kwanza ya Nyerere UNO 1955 katika picha hizo hapo juu ndiyo waliomsindikiza uwanja wa ndege kulia picha ya juu ni Bi. Tatu bint Mzee, Bi. Titi Mohamed, kulia ni Bi. Chiku bint Said Kisusa (mke wa Shariff Abdallah Attas), Julius Nyerere na picha ya chini wa kwanza ni Rashid Sisso, Robert Makange, Zuberi Mtemvu, Iddi Faizi Mafungo, Julius Nyerere, John Rupia na Bi. Titi Mohamed.

Historia ya safari ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere UNO
ina visa vingi sana vya kusisimua kuanzia kuhangaika kupata cheti
cha chanjo cha Mwalimu, kuvamiwa kwa Rashid Ali Meli ofisini
kwake kukamatwa kwa Iddi Faizi Mafungo na makachero, Turiani
akitokea Tanga kuchukua mchango wa fedha za safari kutoka kwa
Mwalimu Kihere hadi siku aliporejea Dar es Salaam na mapokezi
makubwa aliyopata.

Siku ya safari kuelekea UNO Mwalimu Nyerere alisindikizwa na
hao wanachama wa TANU wanaoonelana katika hizo picha mbili
hapo juu.

Siku ya kurudi UNO mji mzima wa Dar es Salaam ulitoka kumpokea.

Kutokana na hao wazalendo hapo juu mtu anaweza kuandika kitabu
kizima cha historia ya TANU.

Jambo la kusikitisha sana ni kuwa picha hizi hazikuwapo popote katika
ofisi za TANU.

Kwa nini iwe hivi hadi sasa?
CCM ifanye juhudi kuenzi historia hii.
 
Kusindikikiza mtu airport tu ndio wawekwe kwenye kumbukumbu za chama?

Amakweli maajabu hayaishi duniani

Historia yetu tunapaswa kuienzi na kuitunza

Haikuwa safari ya kawaida.....

Nisafari Maalum na muhimu sana kwa Taifa letu

Mzee katoa ushauri mzuri sana.
 
Kusindikikiza mtu airport tu ndio wawekwe kwenye kumbukumbu za chama?

Amakweli maajabu hayaishi duniani
Mikocheni...
Umeuliza swali zuri kuwa kumsindikiza Baba wa Taifa uwanja wa ndege ndiyo
wawe kwenye kumbukumbu za Chama?

Hakuna wa kukulaumu kwa sababu wewe hao wote hujui michango yao kwa
Baba wa Taifa binafsi, kwa TANU na harakati za kupigani uhuru.

Nitakueleza kwa mukhtasari tu na nitajaribu kukuwekea na links ili usome
zaidi na uelimike katika historia ya kupigania uhuru.

Katika picha juu ya hao akina mama wa kwanza kulia ni Bi. Tatu bint Mzee
yeye ni katika akina mama wa kwanza kuingia TANU na kuitangaza nyumba
kwa nyumba na alikuwa mjumbe wa Halmashauri Kuu ya TANU mwaka wa
1955 na alikuwapo katika mkutano wa kujadili kujiuzulu Mwalimu Nyerere
kazi ili ajishughulishe na TANU.

Mkutano huu ulifanyika nyumbani kwa Clement Mohamed Mtamila Mtaa
wa Kipata na Sikukuu.

Mwenyekiti wa TANU (miaka ile TANU ilikuwa na Rais na Mwenyekiti).

Bi. Titi Mohamed naamini unaijua historia yake.

Aliyeko kulia wa kwanza kwenye picha ni Bi. Chiku bint Said Kikusa au
Mama Sakina kama wengi walivyomwita.

Bi. Chiku yeye ni katika jamaa zake Abdul Sykes na walimjua Mwalimu
Nyerere
kipindi kile alipojuana na Abdul mwaka wa 1952 na alikuwa shoga
mkubwa wa Mama Maria Nyerere na yeye ndiye aliyewahimiza wanawake
wa Dar es Salaam kujiunga na TANU na kushiriki katika mikutano ili mikutano
ile ishamiri na kunawiri.

Huyu alikuwa mke wa Shariff Abdallah Attas.
Nani Shariff Abdallah Attas?

Shariff Abdallah alikuwa mwanamji na katika watu wa kwanza kufahamiana
na Nyerere pale sokoni Kariakoo alikokuwa akifanyakazi kama Mkusanyi
Ushuru wa Nafaka chini ya ofisi ya Market Master, Abdul Sykes.

Hawa watu ndiyo waliomjengea Baba wa Taifa msingi wa kufahamika na
kukubalika Dar es Salaam.

Shariff Abdallah Attas alikuwa mkubwa kwa umri kumzidi Abdul Sykes
na Abdul alimheshimu sana.

Kuna habari wamenieleza wajukuu wa Bi. Chiku kuwa Mwalimu katika
safari ile ya UNO aliondokea nyumbani kwa Shariff Attas na Bi. Chiku
Mtaa wa Mchikichi na New Street kuelekea Uwanja wa Ndege kwa ajili
ya kufanya dua kabla ya safari lakini nimeshindwa kupata uthibitisho
huru wa hili.

Itoshe tu kuwa Bi. Chiku Kisusa alikuwapo katika msafara wa kumsindikiza
Baba wa Taifa katika safari hii muhimu sana katika historia ya Mwalimu na
katika historia ya TANU.

Mwalimu aliporudi UNO mjukuu wa Bi. Chiku, Jamila ndiye aliyemvisha Baba
wa Taifa
shada la maua.

Tuje kwenye picha hiyo ya chini kuna Rashid Sisso huyu alikuwa bingwa wa
propaganda wa TANU akisimama nyuma ya Nyerere katika mikutano yote ya
hadhara.

Robert Makange mmoja wa waandishi wa gazeti la TANU yeye na Rashid
Kheri Bagdelleh.

Iddi Faizi Mafungo
alikuwa Mwekahazina wa TANU na Al Jamiatul Islamiyya na
ndiye alikuwa mkusanyaji wa fedha za safari ya UNO.

Iddi Faizi alihudhuria mkutano wa kwanza wa TANU Arnautoglo Hall mwezi
Agosti, 1955 mkutano ambao haukuzidi watu 20.

Kadi yake ya TANU na nduguye Iddi Tosiri zinaongozana ni no. 24 na 25.
Hawa ndiyo waliomtambulisha Nyerere kwa kaka yao Sheikh Mohamed Ramia
wa Bagamoyo na TANU ikapata nguzo kubwa huko.

Yuko Zubeir Mtemvu historia yake inafahamika.
Tusimame hapa ingawa yako mengi ya kueleza
 
Mikocheniiiiiiiiii 😂😂😂
Khaligraph...
Unaweza sasa kuisoma historia hii kwa urefu na kuangalia video kwa utulivu hapo chini:





 
Historia yetu tunapaswa kuienzi na kuitunza

Haikuwa safari ya kawaida.....

Nisafari Maalum na muhimu sana kwa Taifa letu

Mzee katoa ushauri mzuri sana.
Adolay,
Mikocheni kasema hayo kwa kutokujua historia ya uhuru wa Tanganyika.

Naamini baada ya leo na kusoma niliyomwandikia na kuingia katika links
nilizoweka hapo atakuwa kaelimika na atachangia kwa adabu zaidi.
 
Adolay,
Mikocheni kasema hayo kwa kutokujua historia ya uhuru wa Tanganyika.

Naamini baada ya leo na kusoma niliyomwandikia na kuingia katika links
nilizoweka hapo atakuwa kaelimika na atachangia kwa adabu zaidi.

Asante sana kwa hizo link nikitoka kazin lazima nisome

Nimuhimu kwetu kutambuwa mambo muhimu yanayohusu Taifa letu.
 
Gagnija,
Angalia nembo nyingine ya East African Airways,,,

View attachment 1173408
Kulia Juluus Nyerere, Kamuzu Banda, Kaluta Amri Abeid na Kanyama Chiume nyuma
Abbas Sykes
Nashukuru mkuu, naamini tupo wengi tuliodhani haya mashirika yalianzishwa na viongozi wetu baada ya uhuru. Lilikuwa kosa kubwa sana kwa hawa viongozi wetu kuyavunja mashirika ambayo wao wenyewe waliyakuta. Pengine kama si ile mifarakano shirika kama hilo lingekuwa leo hii linashindana na kina Ethiopian Airlines.

Hivi Amri Abeid alikuwa na wadhifa gani TANU?
 
Adolay,
Mikocheni kasema hayo kwa kutokujua historia ya uhuru wa Tanganyika.

Naamini baada ya leo na kusoma niliyomwandikia na kuingia katika links
nilizoweka hapo atakuwa kaelimika na atachangia kwa adabu zaidi.
Nimesoma thread iliyoanzishwa na Yeriko Nyerere humu kuhusu harakati za kisiasa kabla ya uhuru nikapatwa na mshangao. Yeriko anadai Ofisi ya AA ilipo ofisi ndogo ya makao makuu CCM Lumumba lilitolewa na gavana wa kikoloni kwa AA. Nijuavyo mimi nyumba ile ilikuwa ya mmoja wa wazalendo waliojitoa kupigania ukombozi wa nchi hii. Lakini kilichonishtua zaidi ni madai yake kuwa Abdul Sykes alitwaa uongozi mwaka 1948 kwa mapinduzi ya vurugu maarufu, "Ondoa wazee" ikiwa pamoja na kuwapiga viongozi wa wakati huo.

Katika hali ya kupokea taarifa zinazokanganya kama hizi za kina Yericko, ni vema wenye taarifa sahihi mkaendelea kuandika kila mnapopata fursa ili kutuondolea huu mkanganyiko tunaoletewa na hawa wanao-promote vitabu vyao vilivyododa kwa kukosa wanunuzi.

Sitazungumzia clip aliyoambatanisha Yericko kwa ukatoliki wangu nisije nikamkosea Mungu kwa kumtukana Padri yule tapeli aliyekuwa akiwarubuni waumini wake mbumbumbu wasiojua lolote.
 
Historia nyingi haifahamiki sababu wengi waliomsaidia Mwalimu ni waislam #Kwaheri Ukoloni kwaheri Uhuru
 
Back
Top Bottom