Kumbusho: Kula kingi kuliko kinachozalishwa ni janga la baadaye

TZ-1

JF-Expert Member
Joined
Sep 28, 2020
Posts
4,321
Reaction score
7,501
Bajeti Kuu ya Serikali ya Tanzania mwaka wa fedha 2024/25 Jumla ya bajeti ya viburudisho, tafrija na kubadilisha samani (furniture) ofisi na nyumba za DCs, RCs, Mawaziri katika Serikali ni TZS 1.9 trilioni.

Bajeti ya Wizara ya Kilimo 2024/2025 ni TZS 1.2 trilioni na Bajeti ya Wizara ya Afya kwa mwaka 2024/25 ni TZS 1.3 trilioni. Wizara mbili zinazogusa maisha ya watanzania, zinazidiwa na bajeti ya viburudisho.

Serikali imetenga bajeti ya vitafunwa na viburudisho kubwa kuliko bajeti ya wizara ya Kilimo ambayo imechangia 16.1% ya pato la taifa, ambayo 2023 imekua kwa 4.2% mwaka 2023 kutoka 2.7% mwaka 2022.

Imetolewa
Twitter

Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan imetenga bajeti ya viburudisho, tafrija na kubadilisha samani (furniture) katika ofisi na nyumba za viongozi kubwa kuliko bajeti ya Wizara ya Afya [Sh1.3 trilioni]. Inasikitisha.

Serikali yenu imetenga karibu trilioni mbili [2] kwa ajili kutafuna visambusa, pipi, bagia, korosho, kahawa. Ok! Wewe mwananchi, ukitembelea hizo ofisi zao, umewahi kupewa hata kitumbua utafune? Tupe ushuhuda.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…