Elections 2010 Kumekucha Nzega! Selelii azomewa mwanzo mwisho!

Elections 2010 Kumekucha Nzega! Selelii azomewa mwanzo mwisho!

Joined
Feb 3, 2010
Posts
19
Reaction score
0
Kinyang'anyilo cha uchaguzi wa kura za maoni mwaka huu katika jimbo la Nzega kimeanza kwa vibweka baada ya mbunge wa jimbo anayemalizia muda wake Lucas L selelii kuzomewa mwanzo hadi mwisho alipopewa nafasi ya kujieleza huku wananchi wakimzomea kuanzia mwanzo hadi mwisho wa mkutano huku wakipaza sauti Asulubiwe! Asulubiwe! hatumtaki hali ilyopelekea hatari ya mkutano kuharibika . kibaya zaidi ni pale alipopanda Husen Bashe yeye alishangiliwa kiasi cha kushindwa kujieleza kwani kelele za wananchi zilikuwa kubwa mno na baadae wananchi wakakumbusha enzi za mrema kwa kulisukuma gari la Bashe hadi pale vyombo vya usalama vilipoingilia kati kwa kuuzuia umati huo wa watu
 
Tupe chanzo cha habari. Au wewe mwenyewe ulikuwepo pale?
 
pamoja na upambe nilikuwepo kwenye mkutano, ni kata ya Ndala baada ya kutoka Budushi na sasa hivi tumefika kata ya puge kata aliyozaliwa selelii watu wamelizunguka gari la Bashe kila mtu anataka kumpa mkono, hadi sasa selelii bado hajashuka ndani ya Gari nadhani anaongea na simu
 
huyu jamaa hana uhakika kwani mimi nipo nzega na hali hiyo haipo acheni uongo
 
Kama hawamtaki kuna siku ya kupiga kura..zomea ya nini?
Seleli nae asome alama za nyakati atakiwi tena huko..tafuta tumaini jipya..
Achana na hao wasiotaka kukosolewa hata 'wanapokula wakasahau kunawa'...
 
Mbinu za EL na RA?

Hiyo inajulikana wazi kwani, huyo EL huwa anakuja hapa mara kwa mara na kufanya vikao vya siri kwa lengo la kummaliza Selelii,
hivyo sintomshangaa huyu ajiitaye Diwani kwa kauli yake hiyo. Tunajua ni mwaka wa uchaguzi tutaona/sikia mengi, kuanzia:
Same Mashariki hadi Kyela, Nzega hadi Urambo, Kahama hadi Sikonge, Vunjo hadi Kwa Dr. Slaa n.k n.k kisa tu Waheshimiwa hawa walikuwa against Richmond, EL, RA, n.k.

Hatuhitaji hekaya za Abunuwasi hapa yatupasa kusubiri kura za maoni. Vp wewe Diwani kwa upande wako Huzomewiiiii!:shut-mouth:
 
Hiyo inajulikana wazi kwani, huyo EL huwa anakuja hapa mara kwa mara na kufanya vikao vya siri kwa lengo la kummaliza Selelii,
hivyo sintomshangaa huyu ajiitaye Diwani kwa kauli yake hiyo. Tunajua ni mwaka wa uchaguzi tutaona/sikia mengi, kuanzia:
Same Mashariki hadi Kyela, Nzega hadi Urambo, Kahama hadi Sikonge, Vunjo hadi Kwa Dr. Slaa n.k n.k kisa tu Waheshimiwa hawa walikuwa against Richmond, EL, RA, n.k.

Hatuhitaji hekaya za Abunuwasi hapa yatupasa kusubiri kura za maoni. Vp wewe Diwani kwa upande wako Huzomewiiiii!:shut-mouth:

Mhnnn!!Mwaka huu lazima pachimbike siutani hii ndo itatupa pcha halisi ya 2015 patakuwaje sbiri wachache warudi idodomya!!subiri!!:blah:
 
Asijali, ajipange tu maana wengi wamepangwa kuwaangusha wapiganaji wa ufisadi . CCM wang'oeni mapema tuwapeleke kwa Dr wa Demokrasia na Maendeleo ya kweli SLAA
 
Diwani usitake kuanza kuaminisha watu kuwa selelii hatakiwi jimboni, si tusubiri kura za maoni! umesema watu awalikumbusha enzi za mrema kwa kulisukuma gari la Bashe, je unakumbuka pia pamoja na mrema kusukumwa ni mkapa ndie aliyeshinda! kusukumwa gari si hoja, huenda Bashe na kundi lake walikodi watu kufanya hivyo ili kum frustrate Selelii, angalia sana Diwani na Bashe wako msije zimia baada ya kura za maoni! kumbuka " ajidhanie amesimama aangalie asije akaanguka"
 
pamoja na upambe nilikuwepo kwenye mkutano, ni kata ya Ndala baada ya kutoka Budushi na sasa hivi tumefika kata ya puge kata aliyozaliwa selelii watu wamelizunguka gari la Bashe kila mtu anataka kumpa mkono, hadi sasa selelii bado hajashuka ndani ya Gari nadhani anaongea na simu

pesa kiasi gani za ufisadi zimetumika hapo .. kikao chenu na RA kitakuwa saa ngapi?
 
huyu jamaa hana uhakika kwani mimi nipo nzega na hali hiyo haipo acheni uongo
Nimefatilia post zake zote yeye ni sifa kwa Bashe na shutuma kwa Seleli. Watu wa aina hii hawatufai hapa JF maana wanatupotezea muda wetu kwa habari za kishabiki kwa makundi yao. Naye anapoteza muda kwenye keyboard, akasukume gari la Bashe roho yake ipate burudani.
 
Jamani hatupaswi kuwa na hasira hapa bali nimepost kuwapa taarifa no matter nimetumwa au la! the issue is ni lichokisema ni kweli au nimetoa wrong habari? niwape habari zaidi ni kuwa baada ya selelii kuzomewa sana jana katika kikao cha tathmini jioni selelii amelalamika kwa viongozi juu ya hali hiyo hivyo yakatoka maamuzi kuwa ni marufuku kwa wananchi kumshangilia mgombea mmoja na yametoka maamuzi kuwa kuanzia leo mikutano isifanyike sehemu zenye mikusanyiko mikubwa ya watu, kwa maana hiyo mkutano wa kwanza wa leo umefanyika kata ya puge lakini nje kabisa ya kitongoji cha puge japo haijasaidia kwani watu wamekodi baiskeli( gana gana) kuufuata mkutano na hali iliyojitokeza jana imejitokeza leo pia japo kidogo imedhibitiwa na viongozi wa msafara kwa kumfanya Bashe awe mzungumzaji wa mwisho. huyo aliyesema yupo Nzega sina hakika sana na taarifa zake kwani kwa sasa tuna malizia mkutano wa Mwisho kata ya Magengati inayopakana na wilaya ya Uyui na watu wamemshangilia sana Bashe nipo kwenye msafara! mwenye swali aulize
 
Back
Top Bottom