Kumuendeleza binti aliyefeli kidato cha nne

FLAVOR

Senior Member
Joined
Jun 13, 2012
Posts
138
Reaction score
49
Wakuu nina mtoto wa marehemu kaka yangu msichana amefeli kidato cha nne, amepata zero. Nataka nimuendeleze kuanzia certificate naomba maoni yenu, kozi ipi itamfaa, yeye anapendelea nursing na utalii
 

Amepata Zero Arudi Tu Shule Hakuna Njia Nyingine Hapo Mkuu !

Asijaribu ku lazimisha ! Mafanikio hayaji kirahisi hivyo ! Utampeleka Certificate bila Cheti?

Mana hiyo zero hata cheti hapati !
Ebu acha masyala
 
Kwenye Utalii sahau Kaka! Huko ni kumpeleka kusomea "U-baamedi" tu hakuna lolote za ziada! Wazazi na Watoto wangi wanapotezwa na Matangazo mengi na Mazuri ya Vyuo vya Utalii ambavyo vingi ni feki tu, hakuna lolote. Wiki mbili tu ndani ya Masomo katika Vyuo hivyo, Watoto, hasa wa Kike, ni "twisheni" za uhakika za ngono na mengineyo. Achana nayo!

Kuna maswali mengi ya kujiuliza kabla ya ushauri wa kama arudie Shule au la. Cha msingi, haya ni maamuzi ya "future" yake. Kaa chini fanya tafakari ya kutosha na ufanye maamuzi sahihi. Kama mambo yote yako sawa, basi arudie Shule katika mazingira tofauti.
 
Ushauri wangu kama mwalimu. hebu huyo kijana mrudishe FORM TWO kabisa akaanze 1.
zero maana yake ni std 7 liver.
 
Wakuu nina mtoto wa marehemu kaka yangu msichana amefeli kidato cha nne, amepata zero. Nataka nimuendeleze kuanzia certificate naomba maoni yenu, kozi ipi itamfaa, yeye anapendelea nursing na utalii

Kwa vitu vingi vya kufanya mfano kujifunza kazi ya upambaji, ufundi cherehani, utalii (kama lugha inapanda) hata office practice; cheti ni karatasi tuu wala siyo hakikisho la mafanikio kimaisha
 
Pia
Nami naomba msaada.

Nina mdogo wangu wa Kike alipata FOUR ya 35 ana C za English & Kiswahili na Hakusoma Sayansi.

Msaada,
Kozi gani itamfaa?.....
 
Pia
Nami naomba msaada.

Nina mdogo wangu wa Kike alipata FOUR ya 35 ana C za English & Kiswahili na Hakusoma Sayansi.

Msaada,
Kozi gani itamfaa?.....



Aende UALIMU mkuu !
!

:msela:
 
Mkuu SAMAHANI,
Serikali imetoa mwongozo kuwa UALIMU mwisho four ya 34.

Hapo vp?.......
 
Wakuu nina mtoto wa marehemu kaka yangu msichana amefeli kidato cha nne, amepata zero. Nataka nimuendeleze kuanzia certificate naomba maoni yenu, kozi ipi itamfaa, yeye anapendelea nursing na utalii

nursing? Mpaka arudie kidato hapo mtafutie kors nzuri kama utalii
 
Pia Nami naomba msaada. Nina mdogo wangu wa Kike alipata FOUR ya 35 ana C za English & Kiswahili na Hakusoma Sayansi. Msaada, Kozi gani itamfaa?.....
changia kwanza mada iliyopo mezani, kama ulikuwa unahitaji msaada ungefungua uzi wako, usibandike tangazo juu ya lingine
 
changia kwanza mada iliyopo mezani, kama ulikuwa unahitaji msaada ungefungua uzi wako, usibandike tangazo juu ya lingine

Ndani ya mada kunaweza kuibuka mada nyingine mkuu ! Hiyo haina tatizo ! Tukisema kila mtu afungue thread kwa maswala madogo some times kama haya ni shida ! 2

Ahsante Mkuu

Naomba radhi kwa hilo.


Ukiishi hivyo unavyoishi kwa upole upole kama huu !

Utanyanyaswa sana ndani humu !

snipa
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…