Kuna aliyeiona hati ya mashtaka kwa watuhumiwa kesi ya binti wa Yombo? Kwanini haiwekwi wazi?

Kuna aliyeiona hati ya mashtaka kwa watuhumiwa kesi ya binti wa Yombo? Kwanini haiwekwi wazi?

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Wakuu salam,

Kesi ya watuhumiwa wa kesi ya Yombo imeanza kuunguruma Jumatattu baada ya watuhumiwa hao kufikishwa mahakamani. Kimtaani mtaani tunajua kilichowapeleka pale ni kumlawiti na kumbaka binti yule.

Mpaka sasa sijakutana na hati ya mashtaka ya watuhumiwa hao, na hata katika kuuliza kwa watu wa karibu ikiwemo wanasheria nao hola!

Pia soma: Yaliyojiri kesi ya Binti wa Yombo Agost 20, 2024: Shahidi mmoja asikilizwa, Watuhumiwa wamerejeshwa rumande

Kwanini document hii haijawekwa wazi? Mpaka sasa polisi hawajatoa taarifa hii, tunapata ripoti kutoka kwa vyanzo mbalimbali vya habari. Kwanini hatupewi taarifa rasmi?

Hii inaonesha fika jinsi jeshi la polisi lilivyokuwa na maslahi katika kesi hii. Tunataka uwajibikaji na hili linajumuisha pia kujua hawa wanyama wanawajabika kwa udhalimu, hii ni pamoja pia na kuwa na taarifa sahihi ili kuweka rekodi sawa.

Polisi na wahusika wote tunajua mnapita humu, wananchi tunataka hati ya mashtaka tujihakikishie uso kwa macho.
 
Wengine tufanye mambo mengine, sio yote yanayotuhusu
 
Kwa kuwema hata ya Mashtaka wazi au mitandaoni sio kosa kisheria?
Kwa taarifa nilizonazo siyo kosa Mkuu, ni document inayoonesha watuhumiwa hao wameshtakiwa kwa makosa gani, ni kama hii ambao ipo humu inayomuhusu Afande
 
Kwa taarifa nilizonazo siyo kosa Mkuu, ni document inayoonesha watuhumiwa hao wameshtakiwa kwa makosa gani, ni kama hii ambao ipo humu inayomuhusu Afande
Ooh apo mekuelewa manake watz ukiwaambia sheria wanakwambia sheria kitu gani
 
Nimeandika nikafuta nikaandika nikafuta.
Anyway
Nyaraka za serikali hazitakiwi kuwekwa mitandaoni.
Si za serikali tu hata baadhi ya nyaraka za taasisi binafsi wanakatazo ya kuziweka mitanaoni.
Kuna issue kama nne ila nakupa moja.
1. Siri
2.
3.
4.
 
Nimeandika nikafuta nikaandika nikafuta.
Anyway
Nyaraka za serikali hazitakiwi kuwekwa mitandaoni.
Si za serikali tu hata baadhi ya nyaraka za taasisi binafsi wanakatazo ya kuziweka mitanaoni.
Kuna issue kama nne ila nakupa moja.
1. Siri
2.
3.
4.
Si kila nyaraka ya serikali ni siri Mkuu
 
Ila mambo ya hii nchi ni ya ajabu sana.

Hii kesi ya jinai maana yake ni kwamba hao Watuhumiwa wameikosea Jamhuri kupitia huyo Binti. Ila cha ajabu Jamhuri ndo inaonekana kupambana kuwanasua Watuhumiwa. Inashangaza sana!
 
Dah ngoja kwanza nifuatilie ndege yetu iliyotua visiwani jana
 
Nonsense!
Kesi za ubakaji na ulawiti zipo zaidi ya elfu, kwanini ya huyo mwanamke iwe special hadi kulazimisha polisi waweke hati ya mashitaka hadharani?

Punguzeni uhanarakati UCHWARA.
 
  • Thanks
Reactions: FWC
Hivi huyo Binti ndugu zake wote masikini maana amekua kama yatima inamaana Hana ndugu wa kushugulikia hili swala kinagaubaga au ndio njaa familia nzima kama njaaa wote hapo hamna kitu wataambulia usishangae siku ya hukumu Binti akasema hajabakwa sababu Ya njaa
 
Ni mpaka dada ako afanyiwe tukio hili ndio utaona linakuhusu Mkuu?
Sina maana hiyo, hapo ndugu wa familia moja wanaamua kesi, tunapoteza mda wetu bure tu kupiga kelele,
Mramba aliibia taifa ma bilioni hukumu yake kwenda kufagia, dogo kachoma picha kala mitano.
 
ila wakiachiwa hawa watu nchi itapatwa na jambo
zito kinoma wakuu 🔥🔥🔥📌📌
 
Back
Top Bottom