Kuna aliyewahi tumia huduma za Kampuni ya Cargo Tanzania?

wegman

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2016
Posts
1,468
Reaction score
2,090
Wakuu habari ya asubuhi?

Nijikite kwenye mada moja moja kwa moja, kuna hiyo kampuni tajwa hapo juu inajihusisha na usafirishaji wa mizigo toka mataifa kama USA, UK na UAE. Hawa jamaa wanadai ofisi yao ipo Zanzibar ingawa kama kuna mzigo wa kuja Bara huwa wanautuma.

Kama tunavyojua zama hizi kuna wimbi kubwa sana la matapeli sasa nia ya kuanzisha uzi huu ni kupata feedback kwa mwanaJF yoyote aliewahi tumia huduma zao ili nijiridhishe maana gharama zao zipo fair kwa kweli.

Au kama kuna mtu anaijua kampuni inayosafirisha mizigo toka USA to Tanzania kwa gharama nafuu anisaidie kuitaja.

Ni hayo tu wakuu.
 
Kampuni inaitwaje? Ndio inaitwa Cargo Tanzania? Nakushauri waombe numbers za branches zao za ZNZ. Tutawafuatilia kwa niaba yako na kukupa feed back.
 
Kampuni inaitwaje? Ndio inaitwa Cargo Tanzania? Nakushauri waombe numbers za branches zao za ZNZ. Tutawafuatilia kwa niaba yako na kukupa feed back.
Ndio mkuu wanaitwa hivyo Cargo Tanzania hata instagram pia wanatumia jina hilo hilo namba zao ni hizi 0654111111.
 
Ndio mkuu wanaitwa hivyo Cargo Tanzania hata instagram pia wanatumia jina hilo hilo namba zao ni hizi 0654111111.
Basi tutawaangalia na kuwapa physical visit halafu tutakupa feedback
 
Itakuwa msaada sana mkuu, we upo Zanzibar?
Sipo.Zanzibar mkuu, lakini umetaka msaada ni wajibu wetu kukusaidia kwa faida yako na ndugu zetu wengine ambao kwa njia moja au nyengine watafaidika na msàada wetu huu!
 
Sipo.Zanzibar mkuu, lakini umetaka msaada ni wajibu wetu kukusaidia kwa faida yako na ndugu zetu wengine ambao kwa njia moja au nyengine watafaidika na msàada wetu huu!
Pamoja chief.
 
Pamoja chief.
Nimewafuatlia mkuu lakini naona mpaka sasa hivi sijapata muafaka na nina wasiwasi either hawako genuine au professional. The later is more likely. Kwa sababu nimejaribu kuwapigia simu siku nzima haipokewi na imefika stage nahisi wame block simu. Kwa unprofessional conduct yao hii naamini kuna uwezekano mkubwa sana ya kupoteza mzigo wako. I hope have been of some help!
 
Siku ya kwanza pia niliwapigia simu sana ilichukua muda kweli kupokelewa. Inaelekea hawapo serious na business yao ngoja nitafute njia nyingine tu mkuu. Ubarikiwe sana kwa mrejesho.
 
Siku ya kwanza pia niliwapigia simu sana ilichukua muda kweli kupokelewa. Inaelekea hawapo serious na business yao ngoja nitafute njia nyingine tu mkuu. Ubarikiwe sana kwa mrejesho.
Good luck!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…