Kuna cha Kujifunza toka Lee Kuan Yew - baba wa taifa la Singapore

Kuna cha Kujifunza toka Lee Kuan Yew - baba wa taifa la Singapore

Mondoros

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2015
Posts
629
Reaction score
474
Baba wa Taifa la Sangapore LeeKuan Yew aliposhinda uchaguzi mkuu kwa mara ya kwanza mwaka 1959 alikuta nchi ipo katika hali mbaya sana katika huduma za Afya,Elimu,Rushwa na ufisadi,ajira,viwanda,miundombinu,umaskini uliokubuhu n.k. Alipoingia madarakani bwana Lee alikuwa na kazi moja tu ya kujenga Singapore mpya yenye uchumi uliobora,huduma za jamii zilizobora pamoja na miundombinu mingine inayohitajika kwa maslahi ya taifa.

Bwana Lee alitumia mbinu mbalimbali ili kuhakikisha anasimamia serikali itakayowanufaisha wanyonge bila ya kuwaathiri matajiri huku akiongozwa na kauli ya “binadamu hawapo sawa” baadhi ya mbinu alizozitumia toka mwaka 1959 mpaka 1961 ni-:

1. Alifuta haki za binadamu kwenye katiba ya Singapore

2. Aliwaondoa wafanyakazi wote wasiokuwa waaminifu(wala rushwa) katika serikali yake na kuwapa kazi vijana wasiokuwa na uzoefu wowote na shughuli za serikali

3. Aliwafungulia mashtaka mafisadi wote nchini Singarepore na wote walipatwa na hatia walinyongwa hadharani

4. Mtu yeyote aliyekuwa anapinga au kukejeri jitihada za serikali hadharani alikamatwa na kupelekwa gerezani

5. Alihamasisha watu kufanya kazi kwa nguvu zote huku serikali yake ikitengeneza mazingira bora ya wananchi kufanya kazi

6. Alitengeneza mazingira bora ya uwekezaji na kuweka sera bora na sheria rahisi za kuwekeza Singapore na alitafuta wawekezaji ndani na nje ya nchi yake kuja kuwekeza nchini mwake

7. Alismiamia nidhamu ya watumishi wa serikali na wananchi

Katika kipindi hicho cha miaka 2 ambayo bwana Lee alikuwa anajenga mfumo mpya wa nchi ya Singapore yalitokea mambo mengi sana magumu ikiwemo ajira kushuka kwa kiasi kikubwa,baadhi ya viwanda kufungwa,huduma za jamii kuzorota ikiwa ni pamoja na huduma za afya,maji,elimu n.k. Mbali na magumu hayo yaliyoikumba nchi ndani ya kipindi kifupi ila wananchi wa Singapore bado waliendelea kuwa na imani kubwa na bwana Lee kutokana na jitihada zake za kupambana na rushwa,kubana matumizi,kuleta nidhamu serikalini,kuboresha miundombini ya umeme,barabara,reli na viwanja vya ndege n.k

Kwasasa nchi ya Singapore ipo katika nchi za dunia ya kwanza(first world country) toka nchi ya dunia ya tatu(third world contry)…….

Lee Kuan Yew aliongoza kama waziri mkuu wan chi hiyo kwa miongo mitatu mfululizo na alijiuzuru nafasi hiyo mwaka 1990 ila aliendelea kuwa kuhudumu katika serikali kama waziri na mbunge mpaka pale mauti yalipomfika mwaka 2015.

by
Ogulu
 
huyo aliitwa brilliant dictator
mwenye double first class honor kutoka chuo bora kabisa duniani. Pamoja na uwezomkubwa wa akili alizungukwa na waliomzidi akili. no Lee kuan yew no modern economic giant china. wachina walijifunza kutoka kwa mchina mwenzao huyo aliyekuwa raia wa singapole. ikumbukwe nusu ya raia wa singapole asili yao ni china na kichina ni moja ya lugha ya taifa.

ni somo la kujifunza
 
Baba wa Taifa la Sangapore LeeKuan Yew aliposhinda uchaguzi mkuu kwa mara ya kwanza mwaka 1959 alikuta nchi ipo katika hali mbaya sana katika huduma za Afya,Elimu,Rushwa na ufisadi,ajira,viwanda,miundombinu,umaskini uliokubuhu n.k. Alipoingia madarakani bwana Lee alikuwa na kazi moja tu ya kujenga Singapore mpya yenye uchumi uliobora,huduma za jamii zilizobora pamoja na miundombinu mingine inayohitajika kwa maslahi ya taifa.

Bwana Lee alitumia mbinu mbalimbali ili kuhakikisha anasimamia serikali itakayowanufaisha wanyonge bila ya kuwaathiri matajiri huku akiongozwa na kauli ya “binadamu hawapo sawa” baadhi ya mbinu alizozitumia toka mwaka 1959 mpaka 1961 ni-:

1. Alifuta haki za binadamu kwenye katiba ya Singapore

2. Aliwaondoa wafanyakazi wote wasiokuwa waaminifu(wala rushwa) katika serikali yake na kuwapa kazi vijana wasiokuwa na uzoefu wowote na shughuli za serikali

3. Aliwafungulia mashtaka mafisadi wote nchini Singarepore na wote walipatwa na hatia walinyongwa hadharani

4. Mtu yeyote aliyekuwa anapinga au kukejeri jitihada za serikali hadharani alikamatwa na kupelekwa gerezani

5. Alihamasisha watu kufanya kazi kwa nguvu zote huku serikali yake ikitengeneza mazingira bora ya wananchi kufanya kazi

6. Alitengeneza mazingira bora ya uwekezaji na kuweka sera bora na sheria rahisi za kuwekeza Singapore na alitafuta wawekezaji ndani na nje ya nchi yake kuja kuwekeza nchini mwake

7. Alismiamia nidhamu ya watumishi wa serikali na wananchi

Katika kipindi hicho cha miaka 2 ambayo bwana Lee alikuwa anajenga mfumo mpya wa nchi ya Singapore yalitokea mambo mengi sana magumu ikiwemo ajira kushuka kwa kiasi kikubwa,baadhi ya viwanda kufungwa,huduma za jamii kuzorota ikiwa ni pamoja na huduma za afya,maji,elimu n.k. Mbali na magumu hayo yaliyoikumba nchi ndani ya kipindi kifupi ila wananchi wa Singapore bado waliendelea kuwa na imani kubwa na bwana Lee kutokana na jitihada zake za kupambana na rushwa,kubana matumizi,kuleta nidhamu serikalini,kuboresha miundombini ya umeme,barabara,reli na viwanja vya ndege n.k

Kwasasa nchi ya Singapore ipo katika nchi za dunia ya kwanza(first world country) toka nchi ya dunia ya tatu(third world contry)…….

Lee Kuan Yew aliongoza kama waziri mkuu wan chi hiyo kwa miongo mitatu mfululizo na alijiuzuru nafasi hiyo mwaka 1990 ila aliendelea kuwa kuhudumu katika serikali kama waziri na mbunge mpaka pale mauti yalipomfika mwaka 2015.

by
Ogulu

maendeleo ni jasho na damu hivi lazima vimwagike
 
kwa hiyo unataka kutuambia na sisi tuko kwenye njia sahihi?
 
kwetu bado Maana kuna mkoa ukiwa unapata huduma za kiserikali ukisema unatokea huko ama ukanda ule walah! lazima yapokelewe kwanza maagizo kutoka juu yaani hali ni tifutifu kabisa Naona umoja haupo kama inavyotakiwa.
 
Namba 1 na namba 4 umeweka tu ili kuwapa moyo mashabiki wa magufuli ila ni uongo.
 
Hapa kwetu waliohusika kutufikisha hapa tulipofika wanajulikana vyema na Mh. Juma aliwaahidi kuwa atawalinda kwa gharama yoyote ile .. Hivyo tuache kuota ndoto za mchana.
 
huyo aliitwa brilliant dictator
mwenye double first class honor kutoka chuo bora kabisa duniani. Pamoja na uwezomkubwa wa akili alizungukwa na waliomzidi akili. no Lee kuan yew no modern economic giant china. wachina walijifunza kutoka kwa mchina mwenzao huyo aliyekuwa raia wa singapole. ikumbukwe nusu ya raia wa singapole asili yao ni china na kichina ni moja ya lugha ya taifa.

ni somo la kujifunza
DXP na LKY
 
huyo aliitwa brilliant dictator
mwenye double first class honor kutoka chuo bora kabisa duniani. Pamoja na uwezomkubwa wa akili alizungukwa na waliomzidi akili. no Lee kuan yew no modern economic giant china. wachina walijifunza kutoka kwa mchina mwenzao huyo aliyekuwa raia wa singapole. ikumbukwe nusu ya raia wa singapole asili yao ni china na kichina ni moja ya lugha ya taifa.

ni somo la kujifunza
Singapole kweli nusu niwa bongo hata kuandika hawajui wapo tu kwenye mijadala
 
Back
Top Bottom