Kuna haja gani kumtazama marehemu ikiwa tunamfahamu na tumeishi naye miaka mingi kabla ya kifo?

Kuna haja gani kumtazama marehemu ikiwa tunamfahamu na tumeishi naye miaka mingi kabla ya kifo?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Kuna faida gani labda ya Kimantiki Watu Kulazimisha (Kung'ang'ania) Kumuangalia Marehemu akiwa 'Jenezani' tena ameshalala Usingizi wake wa Milele na kwamba hata ukipita Kumuaga kwa kumsogelea au kumgusa na kulia kila aina ya kilio wala hawezi kukujua sana sana utakuwa ni kama vile unapaka tu Rangi upepo?

Haya Waaga 'Marehemu' hebu nijibuni.
 
Urithi wa mila na desturi kutoka magharibi, kwa wazungu vilitiathiri sana ndio maana waafrika mfumo wetu wa kuzika ilikua mtu akifa tunahama hilo eneo na kwenda mbali maana tuliamini kifo ni laana na jamii nyingine mtu akifa hakuna kuaga walikua wanaufunga mwili na wanachaguliwa wanaume wa shoka wanaubeba na kwenda nao mbali na kuchimba shimo huko na kuufukia kimila na kurudi nyumbani tena haikuepo masanduku haya ya sasa.

Tukirudi kwenye mila zetu waafrika tutaishi muda mrefu sana na tutakua na furaha.
 
kuna haja gani kuwapungia mkono wa kwa kheri watu wanaposafiri, maana hoja yako ina maana kuwa kuaga ni jambo baya kwa wale tulionao kila siku maishani mwetu..

Unamuaga anaesafiri kwa sababu nae atakuaga na mtaelewana, maiti ataelewa kama umemuaga,? Na ukumbuke pale haelewi chochote kile maana hana ufahamu na uhai sasa kuna sababu gani ya kumuaga tena?
 
Unamuaga anaesafiri kwa sababu nae atakuaga na mtaelewana, maiti ataelewa kama umemuaga,? Na ukumbuke pale haelewi chochote kile maana hana ufahamu na uhai sasa kuna sababu gani ya kumuaga tena?
Hatumuagi kwa sababu atatuona,ile ni heshima ya mwisho kwa marehemu kwa sisi ambao bado tuko hai.

Kwa hoja yako maana yake hakuna hata sababu ya kuhuzuria mazishi maana hataona kama ulienda kumzika, hakuna haja ya kwenda kumzika.

Hoja yako imekosa msingi, ni hoja dhaifu.
 
Hatumuagi kwa sababu atatuona,ile ni heshima ya mwisho kwa marehemu kwa sisi ambao bado tuko hai.

Kwa hoja yako maana yake hakuna hata sababu ya kuhuzuria mazishi maana hataona kama ulienda kumzika, hakuna haja ya kwenda kumzika.

Hoja yako imekosa msingi, ni hoja dhaifu.
Kwani Kigezo kikuu cha Wewe kwenda Msibani ni Kumzika Marehemu au unajulikana umeenda Mazikoni kwa Kumtizama akiwa 'Jenezani' ameshalala na Pamba zake Puani na Masikioni?
 
Aaisee Kuna maana nyng sn kuaga ,Kwanza kuonesha watu wa krb wa marehem kuwa nikweli mlani amekufa maana watu wanamambo mengi wanaweza sema ndugu yao hajafa ila mnazika mgomba,Kuna msiba mmoja nilihudhulia mbeya aisee kulikuwa navurugu mno marehem aligongwa na gar Sasa kukawa na iman kuwa mdogo wa marehem amemuua kaka yake kishirikiana kwakuwa mwili uliharibika vibaya mdogo wa marehem alishaur ukazikwe Bila kufunulia aisee ilitokea fujo kubwa mpk ukafunuliwa so kuaga kunaondoa hayo maswali na Kisha kutoa heshima za mwisho kwakuwa hatutamuona Tena nikama kumfanyia ubatizo mtoto na sherhe kubwa wakat hajui chchte ila ni kutanya kumbukumbu nzr tu
 
Kuna faida gani labda ya Kimantiki Watu Kulazimisha (Kung'ang'ania) Kumuangalia Marehemu akiwa 'Jenezani' tena ameshalala Usingizi wake wa Milele na kwamba hata ukipita Kumuaga kwa kumsogelea au kumgusa na kulia kila aina ya kilio wala hawezi kukujua sana sana utakuwa ni kama vile unapaka tu Rangi upepo?

Haya Waaga 'Marehemu' hebu nijibuni.
Acha kukompliketi mambo
 
Back
Top Bottom