Kuna haja ya kubadili mfumo wa ligi yetu

Kuna haja ya kubadili mfumo wa ligi yetu

Linguistic

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2021
Posts
3,669
Reaction score
8,268
Nadhani sasa tunaona umuhimu wa kuwa na ligi inayoendeshwa kwa viwango vya kisasa, professional FA inayoratibu kwa weledi mpira kwa manufaa ya nchi nzima na siyo timu mbili za Kariakoo, kuvutia uwekezaji mkubwa kwenye vilabu, uwepo wa academy nzuri, viwango bora vya makocha kwa vilabu vyetu, tupunguze uswahili na siasa kwenye mpira.

Na Shida ni Kwamba Wamiliki wa mpira hawatakubali hilo litokee kamwe. Hatutaki kukubali kuwa tunaendesha mpira wetu vibaya. Tuanzie hapo ili tuupatie tiba.

Expedience. As long as wao wanapata wanachotaka, rekodi. Nia siyo kushindana katika uwanja ulio sawa. Ukiangalia harakati za uchaguzi wa viongozi wa mpira ndiyo utajua kuwa maslahi binafsi au ya makundi ndiyo sifa ya uchaguzi

Ebu Jaribu ku propose outsourcing ya Bodi ya Ligi usikie kelele zake.

Wakuu Mpira ni mbinu Kaizer Chief walitulaghai mara oo hatujapata nafasi ya kupumzika mara wachezaji wao ni majerui uku nasi tukiangalia msimamo wa ligi yuko mbali tukajisahau yakatokea hayo.
 
Wanapunguza timu, udhamini mdogo wameridhika na udhamini wa Azam, vodacom na kcb wakati pesa haiendani na matumizi halisi ya timu.
Timu ziwe na timu za vijana kweli sio hawa wakuokoteza kwa ajili ya mashindano na pia wafundishwe na makocha wenye viwango
 
Nchi nzima kushabikia Yanga na simba tu hapo ndio penye tatizo na mbaya zaidi uweledi na ustaarabu ni sifuri kwa watoa maamuzi.

Marefa, Viongozi wa michezo na siasa wote hawa wanaweza kutanguliza ushabiki kwenye maamuzi yanayohusisha simba na yanga.

Simba na yanga hazijawahi cheza mechi za ugenini kwenye ligi maana kote wanakoenda wanakuta mashabiki wao wamejaa.
 
Mpira wa Tanzania hauwezi kukua hata siku moja kwani unaharibiwa na siasa. Leo hii ukiwa Chadema hata uwe kiongozi mzuri namna gani huwezi kuruhusiwa kuongoza timu yoyote katika nchi hii.

Hata vilabu vya mpira vimekuwa vikilazimishwa kuunga mkono juhudi, mara wachezaji wajipelekeshe bungeni nk. Tusipoacha kuchanganya siasa na mpira tutaendelea kuwa wa hovyo hivi hivi kama tulivyo.
 
Kiukwel ligi yetu ni local sana Tena sana ,angalia kama uwanja wa gwambina ,kwel tupo serious na michezo ,ifike wakat bora ligi yetu ishirikishe hata timu 10 zilizobora kabisa na zenye viwanja bora na miundo mbinu safi. Kiwepo kigezo cha uwanja wa timu husika pale inapopanda daraja ,viwanja vya mkoani vilipaswa angalau viwe kama ule wa kaitaba .

Radha ya mpira had timu zicheze dar pekee ,mikoan huko ni butua butua tu ,kiukwel hii lig inazigharimu timu zinazoshirik club bingwa ,ndio maana tumaishia hatua ya robo maana lig yetu sio kipimo sahihi cha kupambana na vilabu vya nchi zingine
 
Kwa hali ya Mambo ilivyo nchini kamwe na haitawezekana kabisa tena kabisa kubadili chochote katika ligi yetu, kwa kuwa tu bado hakuna hata njia ndogo iliyotengenezwa, inayotufanya na kutuonesha kuwa tunaweza kubadilika...
 
Back
Top Bottom