Kuna hatua hupigi kwa sababu kuna watu unawang'ang'ania, wapunguze

Kuna hatua hupigi kwa sababu kuna watu unawang'ang'ania, wapunguze

Mwanasayansi Kalivubha

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2024
Posts
344
Reaction score
926
KUNA HATUA HUPIGI KWA SABABU KUNA WATU UNAWANG'ANG'ANIA, WAACHE.

Yawezekana ikawa ni kuoa/kuolewa umekuwa kwenye mahusiano na watu ambao kihaiba ni KATAA NDOA na wewe unaona ndio aina/type yako kumbe wanakuchelewesha tu

Sio vibaya kujiuliza kwanini kila mahusiano yako hayazai ndoa? Shida ni wewe au ni aina ya watu unaochagua? Badili aina ya watu.

Yawezekana ikawa ni mafanikio ya kiuchumi hupigi hatua kwa sababu aina ya rafiki ulionao ni ile ambayo wewe unachimba shimo wao wanakuja kufukia usiku ila mchana wanakwambia mpo pamoja .

Sio vibaya kuchunguza marafiki zako na uhusiano wao katika mafanikio yako la sivyo usikubali kuwa na watu ambao wanakuzika huku wakikuaminisha kuwa bado upo hai .

Yawezekana ni mafanikio ya ki elimu umeingia kwenye mfumo wa watu ambao wao wanasema muhimu D MBILI TU 😊 na wakati malengo yako yalikuwa ni kufanya vizuri zaidi ya hapo

USIKUBALI WAKUFANYE URIDHIKE USIPOSTAHILI

#Mwanasayansi Saul kalivubha
#Fikia Ndoto Zako
 
Mimi ni pombe tu ila kuacha ndio sitaki hata kusikia huo ushauri.
20250207_111934.jpg
 
Mafanikio ya binadamu sio Mali na fedhwaa ( utajiri) pekee, hata huko duniani sio kila mtu nitajiri. Tunajibebesha mzigo mkuuuubwa kiasi cha kuanza kuzalisha imani potofu kukataa watu wetu muhimu. Komaa kwenye harakati zako kila mwanadamu Ana nafasi yake kwenye maisha yako.
 
Mafanikio ya binadamu sio Mali na fedhwaa ( utajiri) pekee, hata huko duniani sio kila mtu nitajiri. Tunajibebesha mzigo mkuuuubwa kiasi cha kuanza kuzalisha imani potofu kukataa watu wetu muhimu. Komaa kwenye harakati zako kila mwanadamu Ana nafasi yake kwenye maisha yako.
Na sio kila mtu anataka awe tajiri
 
Sijui nipige chini huyu mke wangu mi wa kujenga na kwenda kutembelea lodge yangu kama fuko la bange kisa MKE WANGU
 
Mafanikio ya binadamu sio Mali na fedhwaa ( utajiri) pekee, hata huko duniani sio kila mtu nitajiri. Tunajibebesha mzigo mkuuuubwa kiasi cha kuanza kuzalisha imani potofu kukataa watu wetu muhimu. Komaa kwenye harakati zako kila mwanadamu Ana nafasi yake kwenye maisha yako.
Hope hujaelewa somo, sidhani kama mtoa mada kataja sehemu "kuwa tajiri" tunafeli sana masomo kwa kushindwa kujua intent ya mada au swali la mtihani, unaweza kuwa na majibu mazuri sana ila nje kabisa ya topic husika
 
Mafanikio ya binadamu sio Mali na fedhwaa ( utajiri) pekee, hata huko duniani sio kila mtu nitajiri. Tunajibebesha mzigo mkuuuubwa kiasi cha kuanza kuzalisha imani potofu kukataa watu wetu muhimu. Komaa kwenye harakati zako kila mwanadamu Ana nafasi yake kwenye maisha yako.
Mbona unasema 'huko duniani' mkuu kwani wewe uko mbinguni?
 
Usipojitambuwa mapema utajichimbia shimo na hawo hawo unaowaita marafiki,ndugu na jamaa,kuna marafiki ambao wanakuita tu kwenye pombe na kununua mala.. ndiyo zao, lakini kazi na mambo ya maendeleo hamna.
 
Usipojitambuwa mapema utajichimbia shimo na hawo hawo unaowaita marafiki,ndugu na jamaa,kuna marafiki ambao wanakuita tu kwenye pombe na kununua mala.. ndiyo zao, lakini kazi na mambo ya maendeleo hamna.
Yeah, rafiki wa kweli ni yule anayekupa konekshen ya maendeleo siyo unayeambatana naye kila wakati.
 
Back
Top Bottom