Kuna hatua ugonjwa ukifika ni lazima busara itumike. Mnauza mali zote kulipia matibabu, ndugu anakufa kisha familia inabaki na umasikini wa kutupwa

Mkuu, kuna watu wanakuwa hawana pesa kipindi cha ugonjwa au hawakuwa na taarifa kwamba mtu fulani anaumwa. All in all, yote tumuachie Mungu kwa maana ndiye muweza wa yote.
 
Eeh mkuu, yani mambo haya ni mitihani ya kimaisha. Uwe na asset halafu maza anaumwa ile mbaya na anatibika eti useme siwezi kuuza tv nikamtibu bi. mkubwa. Halipo hilo!
Kama assets zipo nyingi unauza tu mkuu. Kama una nyumba 3 unauza moja ila kama unayo hiyo hiyo moja hapo ndio kasheshe.
 
Kama assets zipo nyingi unauza tu mkuu. Kama unanyumba 3 unauza moja ila kama unayo hiyo hiyo moja hapo ndio kasheshe
Ni noma sana lakini ishu ya Cancer kama hiyo ndo Nyumba pekee mnayo na una familia inaishi humo bhasi sio Busara kuiuzaa maana hata mkipata Bili 100 mgonjwa wa Cancer haponi hasa kwa Nchi kama Tanzania yani wengi wakishaanza chemotherapy bhasi jua hana Muda mkuu akiishi sana mwaka mmoja. Japo kumuacha mgonjwa afe sababu hakuna hela nayo sio sahihi.
 
Haya mambo ni mazito na hayana fikra hizo, ukiyafikiria, kwa uwezo wa kibinadamu unaishia kusema.

'Mungu atuepushe yasitufike'.
 
Je, Ungekuwa unaumwa Wewe UNGEYASEMA HAYA.

Acha nife wanangu wabaki na urithi?

Na je, kama ugonjwa unatibika lakini lazima nyumba na magari viuzwe?
 
Kuna stage ikifika daktari anasema hapa haiwezekani tena. Familia za kipato cha chini unakuta nyumba moja wanakaa watu 10
Nikweli... Lakini huyo Ni doctor mmoja
Ndo Maana wanaamini doctor mwingine anaweza kuwa na majibu tofauti..
.
Imagine mwanao anaumwa... Ungesema acha afe... Nyumba Ni urithi wa wengine
 
Hii mentality, nitawaachaje warithi.

Kuna ndugu yangu mumewe Ana kesi hataki kuuza asset za familia eti watoto watakosa urithi[emoji3][emoji3][emoji38]...watoto wa miaka 11..6.. 1

Bora mumewe afungwe kuliko watoto wakose urithi? [emoji849][emoji849][emoji849]
 
Nikweli... Lakini huyo Ni doctor mmoja
Ndo Maana wanaamini doctor mwingine anaweza kuwa na majibu tofauti..
.
Imagine mwanao anaumwa... Ungesema acha afe... Nyumba Ni urithi wa wengine
Mimi kama baba na kazi yangu ni kuuza chips na niliijenga nyumba kwa kubangaiza miaka 9 nyumba yenyewe hiyo hiyo moja tunakaa watu 10 huko Mbagala leo hii mtoto wangu anaumwa na daktari anasema hawezi kupona nitafanya nini tena zaidi ya kumuachia Mungu kwa maana ndiye muweza wa yote?
 
Haya
 
Hii ya kesi za mahakamani usilinganishe na suala la "life & death" kwa maana mtu akifungwa si mwisho wa siku atatoka tu hata kama baada ya miaka 10.

Sasa mtu akifa atafufuka tena?
 
Kama watoto ni wakubwa na wanajitegemea sawa, ila ndio una wale wa shule za msingi, secondary na kibanda ni hicho hicho na Dr kasema hapa nikumwachia Mungu nyie mnapalangana kuuza mkatafute wataalaamu wengine nadhani busara inatakiwa hapa....Tusiongee tu kuuza....tunatafuta na kujijenga kwa ajili ya future generation na sio kingine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…