DOKEZO Kuna kijiji wilaya ya Magu wageni wanaoingia kuishi kama wapangaji kulipa fedha za kiingilio kiasi cha shilingi 36,000 ndipo usajiliwe

DOKEZO Kuna kijiji wilaya ya Magu wageni wanaoingia kuishi kama wapangaji kulipa fedha za kiingilio kiasi cha shilingi 36,000 ndipo usajiliwe

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Shaksi Msovieti

New Member
Joined
Feb 2, 2025
Posts
1
Reaction score
2
Habari JamiiForums.

Naomba msaada, mimi ni mgeni katika kijiji fulani, wilayani Magu Mkoa wa Mwanza. Katika kijiji hiki kuna utaratibu kwa wageni wanaoingia kuishi kama wapangaji kulipa fedha za kiingilio kiasi cha shilingi elfu 36 ndipo usajiliwe ama ujiunge kama mwananzengo na utambulike kama mkazi rasmi.

Tofauti na hapo, kuna vitisho kwamba unaweza usitambulike au kutishiwa kufukuzwa. Je hii ni sawa.

Tunaomba Mamlaka za Wilaya situsaidie katika hilo maana imekuwa kero na usumbufu sana. Je ni halali kisheria viongozi wa mtaa/kijiji kulipisha watu ili wajiunge kwenye kijiji au mtaa?

Kama ni halali, ile haki ya Mtanzania kuishi mahali popote iko wapi? na je Serikali inatambua huu utaratibu wa baadhi ya maeneo katika wilaya zetu, maana naamini si kila sehemu kuna huu utaratibu.

 
Habari JamiiForums.

Naomba msaada, mimi ni mgeni katika kijiji fulani, wilayani Magu Mkoa wa Mwanza. Katika kijiji hiki kuna utaratibu kwa wageni wanaoingia kuishi kama wapangaji kulipa fedha za kiingilio kiasi cha shilingi elfu 36 ndipo usajiliwe ama ujiunge kama mwananzengo na utambulike kama mkazi rasmi.

Tofauti na hapo, kuna vitisho kwamba unaweza usitambulike au kutishiwa kufukuzwa. Je hii ni sawa.

Tunaomba Mamlaka za Wilaya situsaidie katika hilo maana imekuwa kero na usumbufu sana. Je ni halali kisheria viongozi wa mtaa/kijiji kulipisha watu ili wajiunge kwenye kijiji au mtaa?

Kama ni halali, ile haki ya Mtanzania kuishi mahali popote iko wapi? na je Serikali inatambua huu utaratibu wa baadhi ya maeneo katika wilaya zetu, maana naamini si kila sehemu kuna huu utaratibu.

Mkuu ungetaja kijiji ingependeza zaidi, ili mamlaka wafahamu zaidi kinachoendelea kuhusu hoja yako ulioileta
 
Habari JamiiForums.

Naomba msaada, mimi ni mgeni katika kijiji fulani, wilayani Magu Mkoa wa Mwanza. Katika kijiji hiki kuna utaratibu kwa wageni wanaoingia kuishi kama wapangaji kulipa fedha za kiingilio kiasi cha shilingi elfu 36 ndipo usajiliwe ama ujiunge kama mwananzengo na utambulike kama mkazi rasmi.

Tofauti na hapo, kuna vitisho kwamba unaweza usitambulike au kutishiwa kufukuzwa. Je hii ni sawa.

Tunaomba Mamlaka za Wilaya situsaidie katika hilo maana imekuwa kero na usumbufu sana. Je ni halali kisheria viongozi wa mtaa/kijiji kulipisha watu ili wajiunge kwenye kijiji au mtaa?

Kama ni halali, ile haki ya Mtanzania kuishi mahali popote iko wapi? na je Serikali inatambua huu utaratibu wa baadhi ya maeneo katika wilaya zetu, maana naamini si kila sehemu kuna huu utaratibu.

Pesa hizo ni bima yako kwa ulinzi, ugonjwa, kifo na uzinzi(matunzo ya mtoto endapo utampa mimba mwanafunzi kisha ukatoroka). Ukiona haikupendezi usiende kuishi hapo.
 
Habari JamiiForums.

Naomba msaada, mimi ni mgeni katika kijiji fulani, wilayani Magu Mkoa wa Mwanza. Katika kijiji hiki kuna utaratibu kwa wageni wanaoingia kuishi kama wapangaji kulipa fedha za kiingilio kiasi cha shilingi elfu 36 ndipo usajiliwe ama ujiunge kama mwananzengo na utambulike kama mkazi rasmi.

Tofauti na hapo, kuna vitisho kwamba unaweza usitambulike au kutishiwa kufukuzwa. Je hii ni sawa.

Tunaomba Mamlaka za Wilaya situsaidie katika hilo maana imekuwa kero na usumbufu sana. Je ni halali kisheria viongozi wa mtaa/kijiji kulipisha watu ili wajiunge kwenye kijiji au mtaa?

Kama ni halali, ile haki ya Mtanzania kuishi mahali popote iko wapi? na je Serikali inatambua huu utaratibu wa baadhi ya maeneo katika wilaya zetu, maana naamini si kila sehemu kuna huu utaratibu.


Hilo suala la kawaida,
Lazima ulipe kiingilio ili nzengo ikutambue ,siyo kukaa bila kutambulika.
Ukilipa unaingizwa kwenye kitabu cha nzengo maana umekuwa mwenzao sasa.
Hizo pia ni taratibu za mitaa na vitongoji + vijiji hasa kanda ya ziwa.
Ni utaratibu mzuri wa kutambuana.
 
Hilo suala la kawaida,
Lazima ulipe kiingilio ili nzengo ikutambue ,siyo kukaa bila kutambulika.
Ukilipa unaingizwa kwenye kitabu cha nzengo maana umekuwa mwenzao sasa.
Kutambulika maana yake Nini?
Hizo pia ni taratibu za mitaa na vitongoji + vijiji hasa kanda ya ziwa.
Sema usukumani sio kanda ya ziwa.
Ni utaratibu mzuri wa kutambuana.
Sio utaratibu mzuri hayo yalikuwa maisha ya kijima na hizo jamii ni uncivilized, barbaric.
 
Hiyo ipo sehemu nyingi mkuu, labda uwaulize mchanganuo wa hiyo hela yako, ila maenek mengi hata kule kijijini kwetu mpangaji ukifika tu, mwenye nyumba anakupeleka kwa balozi wa nyumba kumi. Hapo utaandikishwa jina, mahali ulipotoka, ndgu au jamaa wanaokujua mtaa huu mpya au wa jirani.

Na utatakiwa kutoa baadhi ya michango inayoendelea kwenye hiyo nzengo, na wewe unakua mmoja wa wanamtaa pia.

Hii inasaidia sana kushape mtaa, sio rahisi kukutana na uhuni au wizi wa kijingajinga.
Nenda ujisajiri kijana.
 
Sio lazima naishi mwanza sijawahi fanya huo ujinga
Unajua hata kisheria inatakiwa hivyo, ukifika mahali inabidi serikali yako ya mtaa itambue. Na kama ni mkazi wa kudumu na kuna shughuli za maendeleo maeneo hayo inabidi uchangie.
Kwa mjini in en out ni nyingi sio rahisi kumonitor ila bush hutaishi kwa amani bila kufahamika wewe ni nani.
 
Mbona huo utaratibu uko karibia usukumani pote japo kiwango cha pesa hakilingani,kuna vijiji vingine ni 10000 vingine 5000,vingine 15000 kufatana.
Hawakulazimishi kutoa ila siku ukipata tatizo usitegemee msaada wowote kutoka kwenye jamii iliyo kuzunguka.
 
Back
Top Bottom