DOKEZO Kuna kiongozi mmoja idara ya Elimu Sekondari halmashauri Masasi DC hana utu

DOKEZO Kuna kiongozi mmoja idara ya Elimu Sekondari halmashauri Masasi DC hana utu

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Zamazangu

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2015
Posts
849
Reaction score
497
Katika pitapita yangu nimekuta walimu wa Sekondari halmashauri ya wilaya ya Masasi wakibadilishana mawazo lakini katika hali ya kulalamika kuwa kuna kiongozi mmoja ndani ya idara ya Elimu Sekondari hana utu.

Nilitamani sana kujua ana matatizo gani hasa, yafuatayo yalibainishwa kuwa ndiyo matatizo yake.

1. Anapenda sana rushwa hasa inapotakiwa kulipwa malipo ya kisheria kama vile likizo uhamisho nk yale yanayotolewa ndani halmashauri. Yeye ana tabia ya kuchelewesha malipo ambayo yako tayari na ili ilipwe basi unapaswa kumpigia simu ili muongee, nadhani hapo ninaeleweka, wakati mwingine anaweza kukupigia kukuarifu kuwa kuna malipo yanaandaliwa kwa hiyo jiongeze.

Kwa muktadha huo wapo walimu hasa wale wasiopenda rushwa hawajalipwa madai yao kwa miaka kadhaa wakati wale wanaoona kutoa rushwa sio issue wanalipwa mara nyingi. Uchunguzi ukifanyika itadhihirisha hili ninalolisema.

2. Ana tabia ya kuchelewesha taarifa muhimu zinazohitajiwa kutendewa kazi na kuziomba kwa wahusika nyakati za mwisho, hii husababisha mshike mshike usio na sababu.

Viongozi wa shule na wasaidizi wao huwa na wakati mgumu sana maana utasikia anasema " hakikisha taarifa inafika kwangu by kesho saa 4 asubuhi," tena umebaki wewe tuu wenzako wote washawasilisha. Nk

Mambo haya na mengine mengi yanavunja sana moyo watumishi wa umma. Tufanye kazi kwa kupendana maana sisi sote ni ndugu na tunajenga nyumba moja.

Ahsante
 
Kuna mwaka nilikuwa naomba tenda fulan idara ya elimu KILWA MASOKO kina DEO alikuwa anaitwa KAJUSI aliogopeka Sana had na staff wenzake.
 
Tema mate chini!! Nimepiga firts class tangu chini mpaka juu.
First class yako ni bure kabisa
First class uliyofundishwa nakusahihishiwa na Walimu walio wa hovyo kabisa
Hivyo wewe ni kati ya mazao ya hovyo kabisa yaliandaliwa kihovyohovyo
Kwahiyo Walimu wako wahovyo na kada yao, wewe na first class yako ni bure kabisa
 
Ualimu ni kada ya hovyo sana!
Ila mkuu, hapa tz kuna watendaji wapumbavu sana. Mtoa mada kalenga sekta ya elimu, lakini we angalia jeshi la polisi(kwenye dhamana), baadhi maofisa mikopo benk.
 
Huko nimesikia kuna afisa utumishi mmoja kawaita ofisini kwake kesho walimu waliogoma kulipa pesa za mwenge ngoja nifanye uchunguzi
 
Kuna mwaka nilikuwa naomba tenda fulan idara ya elimu KILWA MASOKO kina DEO alikuwa anaitwa KAJUSI aliogopeka Sana had na staff wenzake
Bila shaka ni kajisi huyo, alitoka tunduru akahamia huko ni miaka ya 2010 na kuendelea.
 
Back
Top Bottom