DOKEZO Kuna kundi la Watu Kinyamwezi-Pugu linajihusisha na utapeli wa Ardhi, linatishia Watu na haliogopi Serikali

DOKEZO Kuna kundi la Watu Kinyamwezi-Pugu linajihusisha na utapeli wa Ardhi, linatishia Watu na haliogopi Serikali

  • Thread starter Thread starter Anonymous
  • Start date Start date
Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest



Huku kwetu Pugu - Kinyamwezi tuna changamoto ya kikundi cha Watu ambao wamekuwa wakifanya matukio ya utapeli wa ardhi kwa muda mrefu, hawaogopi Serikali wala Vyombo vya Usalama.

Wamekuwa wakitufanyia fujo, wakiona sehemu ipo wazi wao wanavamia wanachukua maeneo hayo kwa nguvu.

Wameshakamatwa mara kadhaa lakini baada ya muda wanatoka, wakipelekwa Polisi huko ndio hawakai kabisa, wakitoka wanawarejea wale waliowashtaki.

Wakikuona wewe ndio una kiherehere wanakwambia kabisa “watakupoteza”. Mmoja wa kiongozi wao anaitwa Shabani Mapete.

Viongozi mbalimbali wanajua akiwemo Mkuu wa Wilaya na hivi ninavyoandika hapa kuna kesi inayoendelea Mahakamani kuhusu masuala ya Ardhi, lakini wao hawajali kuhusu kesi.

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo alifika hadi maeneo yetu akaagiza Jeshi la Polisi lifuayilie malalamiko yetu na ikiwezekana matapeli hao wakamatwe.

Wakikamatwa wanapelekwa Kituo cha Polisi cha Chanika baada ya muda wanarejea Mtaani, inawezekana kituo hicho nacho kina shida.

Mapema wiki hii wamevamia shamba la mama mmoja wa hapa mtaani wakaanza kung’oa mazao yake aliyokuwa amepanda, mama huyo hana shida na kesi inayoendelea lakini jamaa wamefika na kuharibu kila kitu, alikuwa anawarekodi lakini hawakujali chochote wanasema wao hakuna wanayemuogopa Serikalini.

Tunaomba ujumbe huu ufike kwa Waziri wa Ardhi, Waziri Mkuu na Rais Samia kuwa kuna Watu huku Pugu wanadai wao hawaogopi Serikali na hawajali maamuzi ya Polisi wala Mahakama, tusaidie tunaishi kwa hofu kama vile Serikali haipo.
 
Watakuwa Wana afya ya akili,maana haya maneno ni ya kipumbavu!
 
UZOEFU UNAONYESHA KWAMBA;
-Matapeli , waporaji sugu wa maeneo ya watu ni walio kuwa wenyeviti wa serikali za mtaa.
-Ni wafuasi na mashabiki wazuri wa chama cha mapinduzi
-wako karibu ni viongozi wa chama na serikali
-wanaukaribu sana na polisi.
Hivyo hakuna wanacho ogopa

ukifika polisi huwezi pata ushirikiano wowote.
KUDAI KATIBA MPYA SI KWA SBB CHADEMA WANATAKA KUTALAWA.
 
UZOEFU UNAONYESHA KWAMBA;
-Matapeli , waporaji sugu wa maeneo ya watu ni walio kuwa wenyeviti wa serikali za mtaa.
-Ni wafuasi na mashabiki wazuri wa chama cha mapinduzi
-wako karibu ni viongozi wa chama na serikali
-wanaukaribu sana na polisi.
Hivyo hakuna wanacho ogopa

ukifika polisi huwezi pata ushirikiano wowote.
KUDAI KATIBA MPYA SI KWA SBB CHADEMA WANATAKA KUTALAWA.
Umenena vyema sana.
 
UZOEFU UNAONYESHA KWAMBA;
-Matapeli , waporaji sugu wa maeneo ya watu ni walio kuwa wenyeviti wa serikali za mtaa.
-Ni wafuasi na mashabiki wazuri wa chama cha mapinduzi
-wako karibu ni viongozi wa chama na serikali
-wanaukaribu sana na polisi.
Hivyo hakuna wanacho ogopa

ukifika polisi huwezi pata ushirikiano wowote.
KUDAI KATIBA MPYA SI KWA SBB CHADEMA WANATAKA KUTALAWA.
Kuna ukweli kwa kiasi fulani.
But all in all, Matapeli wa Ardhi wengi sana Wana urafiki mkubwa sana na Mahakimu (Wenyeviti) wa Mahakama za Ardhi hapa Tanzania, wamekuwa watu wao wakubwa wa kuwapelekea fedha za rushwa ili washinde Kesi Mahakamani.

Kushindana na Matapeli wa Ardhi ni kushindana na Serikali.
 
UZOEFU UNAONYESHA KWAMBA;
-Matapeli , waporaji sugu wa maeneo ya watu ni walio kuwa wenyeviti wa serikali za mtaa.
-Ni wafuasi na mashabiki wazuri wa chama cha mapinduzi
-wako karibu ni viongozi wa chama na serikali
-wanaukaribu sana na polisi.
Hivyo hakuna wanacho ogopa

ukifika polisi huwezi pata ushirikiano wowote.
KUDAI KATIBA MPYA SI KWA SBB CHADEMA WANATAKA KUTALAWA.
USITUINGIZIE SIASA HAPA, HII NI JINAI, WAHUSIKA WAKAMATWE WAWEKWE NDANI, NDG NDEJEMBI ANA NA HILI KWANZA ILI IWE MFANO KWA MATAPELI MENGINE!
 
Back
Top Bottom