Kuna mahala Simba SC tunakosea

demigod

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2015
Posts
8,292
Reaction score
15,250
Ukweli unaouma Simba na Yanga zinatumia muda na nguvu nyingi sana kufikiri na kufanya mambo ili kuumizana wao kwa wao; badala ya jinsi ya kufanikiwa kimataifa Kila hatua, kila kitu wanafanya wanafikiria Mtani wa Jadi! Tunajibakisha Ndondo kwa fikra hii.

Naipenda na naiheshimu timu yangu sana. Naipa muda nione matokeo ya mkakati huu. Lakini kimataifa sijaona kama tumefanya chochote mpaka sasa. Zile tano zitahusika nasi sana tu ugenini; hata kama tutashinda nyumbani Muda utaongea.
 
Hongera kwa uzalendo wako. Hakika umenena vema.
 
Well said. Kuumizana.
Sajili za Gardiel, Ajib, Beno na sasa Morrison zimelenga kuiharibia Yanga kuliko kuimprove Simba.

Tayari kwa hao watatu wa mwanzo imeonekana dhahiri.
La Morrison ni njama ya kusema kuwe na mgogoro tumkose wote.
Meanwhile, hakuna efforts za kukwepa zile tano za ugenini champions league.
 
Kulia atakimbiza Morrison, Kushoto atakimbiza Miquosone. Sub Deo Kanda, Sub Kahata. Hapo hamna hamna mpaka half time Al Ahly 0-4 Simba, Tena tuko away Misri hapo.

Nitajie sub ya safu ya ulinzi...maana ninawaona wale wale waliochezea KIGANJA.
 
Nitajie sub ya safu ya ulinzi...maana ninawaona wale wale waliochezea KIGANJA.
Simba alikuwa anagongwa tano kutokatana na approach ya kocha mkuu.....Ugenini anashambulia tu, as if wako level moja na Ahly...
Usajili bado haujafungwa...ko subiri Ukuta lazima uzingatiwe...
Wameshaanza na Ame na Kameta kama backup ya Kennedy na Kapombe......
Bado beki moja ya kimataifa hivyo unapaswa kutulia mkuu.
 
Nataka kusema kitu kuhusiana na usajili wa Simba ikiwa ni maandalizi ya Champions League lakini naona nasita kwani bado hawajamaliza usajili wao. Ngoja niwe na subira kidogo nione kama kweli wanakumbuka vizuri zile tano tano za As Vita na Al Haly.
 
Kawaida yao! Hawafiki popote, tutaishia kombe la "karia" na simba yake!
 
Wewe ni Yanga usijifiche kwenye kichaka Cha mahindi. Simba hawasajiri hovyo hovyo tu ila kwa kufata mapendekezo ya mwalimu. Na hizo tano unazosemea sisi Simba hazikutukera hata kidogo. Kiujumla kwenye mashindano yale tulifanya vizuri sana. Tulikua na Al ahly, as Vita na soura timu zote zimetupita kwa kuinvest kwenye mpira ila kocha na wachezaji walipambana mpka wakashika nafasi ya pili na kusonga robo fainali na kuwaacha as vita. Taifa likaongezewa idadi ya timu za kushiriki mashindano ya kimataifa. Kwenu nyingi Yanga mnajifanya hamuoni yote hayo mnaona tano tu za ugenini. Luc aymel alisema mashabiki wa utopolo hamjui mpira mnabweka tu Kama manyani na mbwa. Na huo ndio ukweli.

 
Nenda Instagram wameondoa post zote za Morrison akisaini zile nyaraka feki maana ni plain paper
 
Vipi mwaka jana mliishia wapi mkuu kwenye hiyo michuano? [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hua wanashangaa inakuaje sishabikii mpira wa ndani. Sababu ni kama hizi.
 

Simba mnakosea?

Umehamia Simba lini?
 
Reactions: Tui
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…