Bwana yule aliamini hakuna upinzani, aliamini anaungwa mkono na kila mtz, bara na visiwani na mpaka ulimwengu mzima, wali underestimate, otherwise wangalijua hali ingekuwa hivi, hakika TL, wangemzuia asije nchini, wangetumia mbinu zote, zilizo chini ya jua, abakie huko huko.Wachache watakuelewa kiufupi Chadema wali outsmart CCM,kutumia ushawishi wa mataifa ya magharibi.
CCM yangu ( yetu ) ina Wapiga Kura wake Milioni 22 'Kitakwimu' na 'Kiutafiti' hadi leo hii sasa Wewe 'Kisokolokwinyo' Mmoja tu una 'Athari' gani?Kama kuikataa CCM ni unafiki itabidi baraza la kiswahili wabadili maana ya neno unafiki.
Kuna clips ya Kikwete wakati huo ni Mwenyekiti na Rais wa JMT aliwaambia CCM hawezi kutumia police kujibu hoja za wapinzani.
Ni wajibu wa Kinana,Nape na Mawaziri kujibu hoja za wapinzani,utawala imekuwa ni kazi ya police,mahakama,TRA na Uhamiaji kujibu hoja kwa namna ya kutisha,kuadhibu,kupotezwa na kubambikiwa kesi za kutakatisha fedha.
Kwi Kwi KwiCCM yangu ( yetu ) ina Wapiga Kura wake Milioni 22 'Kitakwimu' na 'Kiutafiti' hadi leo hii sasa Wewe 'Kisokolokwinyo' Mmoja tu una 'Athari' gani?
Ccm uzuri wanauelewa ukweli,uchaguzi ukiwa huru na wa haki,ccm ijiandae kukabidhi nchi.Kwi Kwi Kwi
View attachment 1604423
CCM yangu ( yetu ) ina Wapiga Kura wake Milioni 22 'Kitakwimu' na 'Kiutafiti' hadi leo hii sasa Wewe 'Kisokolokwinyo' Mmoja tu una 'Athari' gani?
Hivi kadi ccm ya Bashiru ni namba ngapi ?Endelea kuamini takwimu za Polepole,CCM haina wanachama 1 million.
WanaCCM asili wanajua hali halisi ilivyo sasa huko site.
Polepole muumini wa serekali 3 na Dr Bashiru CUF damu hawakijui chama asilani hawa ni wageni baada ya uchaguzi watatimuliwa bila kuzingatia matokeo ya uchaguzi.
Hawa wamemdhalilisha Mwenyekiti,wamemfikisha mahali pagumu hadi kufikia kupiga magoti loh salaleeh watatimuliwa mapemaaa.
KweliUtawala wa jiwe umetuumiza sana, yani tunaishi kwenye nchi ambayo unaweza sema siyo yakwetu
Kutegemea dola badala ya hoja, wameitumia police kuuwa upinzani imeback fire polisi wamechangia kuimarika kwa upinzani Hadi vijijini.
Lolote baya walilowatendea watz limerudi kwao mara 7.
.wamebandika mabango nchi nzima.
.wamezuia media zote
.wametumia wasanii wote
. wanatumia police
. wametumia time
.wametumia msajili
Lkn vyoote vimebuma.
Chama mfu Ni kile kinachobebwa na dola badala ya nguvu ya umma. Anaemiliki nguvu ya umma ndie anaemiliki dola.
Namba milioni 21,laki3, elfu67, mia9 na 85Hivi kadi ccm ya Bashiru ni namba ngapi ?
Fikra chakavu za mwenyekiti,na unafiki wa wana ccm ndiyo umetufikisha hapa...Wakuu heshima sana,
Kadri siku ya uchaguzi mkuu zinapokaribia nabaki najiuliza maswali kadhaa bila majibu.
Najaribu kutafakari ni eneo gani haswa CCM ilikosea ?.
Mosi,kununua wapinzani (wabunge,madiwani na viongozi wa vyama).Wananchi au ukipenda unaweza kuwaita wapiga kura hawapendi siasa za aina hiyo.
Ukinunua wabunge au madiwani yawezekana bado haujanunua wapiga kura au sababu za kuchagua upinzani bado zinakuwa pale pale !.
Pili,Style ya kutawala au kuongoza za utawala huu si rafiki au wapiga kura hawazipendi.Hivi siasa za kutumbua tumbua fukuza fukuza mara vyeti feki bado si jawabu la kupendwa ? !.Labda tuseme kulikuwa na uonevu,kukiuka sheria na taratibu za ajira au vyote kwa pamoja.
Tatu, Matumizi ya kupiliza ya vyombo vya habari kusifiwa na majivuno.TBC chini ya Dr Ryoba ilipitiliza kusifu kila jambo mara ndege,Reli,Vyeti feki lakini Makonda hausiki na ukaguzi.Barabara hata ya Kilometer 2 mtu atasifiwa kuanzia asubuhi hadi jioni kuanzia Jumatatu hadi Jumatatu nyingine ni mwendo wa kumsifu mtu mmoja ungefikiri kujenga Daraja au Kivuko ni hisani kumbe ni wajibu wake tena kazi yenyewe kaiomba kwa kampeni na ahadi luluki.
Nne,Unasema pekee yako miaka mitano wengine wakisema shida (Kesi,Vifungo,misukosuko....)Nauliza WaTanzania wamechoka na siasa za aina hii !.
Tano,Ujenzi wa Flyover Dar una faida zipi kwa mkaazi wa Dongobesh au Tarakea mkulima wa ndizi au mkulima wa Ngogwe Lushoto.Naamini kila eneo la nchi yetu lina mahitaji yake ya msingi kutokana na mazingira yake.
Sita,Watawala wetu walifika mahali wakajiona hapo walipo walifika wenyewe si wananchi /wapiga kura.Kauli zao maamuzi yao mengi yalilenga kuwanufaisha wao wenyewe eg kupitisha sheria za kuwajengea nyumba MaRais wastaafu,Sheria za mafao yao na matibabu yao zipo vizuri kweli kweli wakati wafanyakazi sheria za mafao yao kila mara wanatengenezewa sheria za kuwakandamiza eg sheria ya kujitoa na kikokoteo.Sheria za kinga ya kutoshitakiwa hata wakifanya makosa ya aina gani !.
Mwisho nadhani watawala hawakujiandaa kukumbana na uchaguzi wenye ushindani wa kiwango hiki tunachokiona sasa.Walifikiri kumnunua Silinde,Lijualikali,Nassari ...... watakuwa wamemaliza kila kitu sasa wamekutana na uungwaji mkono wa kiwango cha kutisha kutoka kwa mgombea wa CHADEMA.
Tangu mfumo wa siasa wa vyama vingi kuanzishwa tumewaona wagombea walioleta kashi kashi za kutisha.Mwaka huu 2020 tumeanza kuona dalili mbaya kwa baadhi ya mikoa ambayo chaguzi za nyuma walikuwa wakiunga mkono CCM.Mkoa ya Rukwa,Sumbawanga,Katavi,Simiyu,Ruvuma,Lindi na Mtwara ni ngome ya CCM kwa muda mrefu lakini tumeshuhudia katika uchaguzi huu wananchi wa mikoa hiyo wakibadilika na hivyo kuiweka CCM katika wakati mgumu.
Ni butu kwerikweri....CCM walijikoroga walipomuajiri Polepole na digirii yake ya unafiki
Sasa unawaweka benchi akina Januari Makamba kwa kuwafitinisha na Mwenyekiti
Miamba ya Siasa kama kina Kinana ndio wangeiweza kasi ya Lissu sio haka ka Chawi ambako kamezeheshwa na roho mbaya ya Kichawi
Polepole ni bure kabisa ni Butu kisiasa na kijamii
Kuna Watawala 3 Duniani ambao sikuwahi kudhania wangetoka madarakani niliomba uhai niwashuhudie Wakitolewa Madarakani nao ni Sadam Hussein, Mobutu Sese Seko na Omar Al Bashir! Kweli nikashuhudia! Naamini nitashuhudia CCM ikitoka madarakani siku moja pia