Kuna mambo tuache siasa, Steve Nyerere hafai kuwa balozi wa chanjo

Kuna mambo tuache siasa, Steve Nyerere hafai kuwa balozi wa chanjo

Memento

JF-Expert Member
Joined
Jun 13, 2021
Posts
4,423
Reaction score
9,986
Kuna vitu vinashangaza sana, wizara ya afya inashangaza sana. Wote tumeshuhudia duniani kote suala la chanjo likiwa mjadala mkubwa sana ambapo kila aina ya utaalam unatumika kwa wanaokubali na wanaoipinga.

Hivyo si suala la kisiasa wala propaganda bali ni la kisanyansi, ndio maana niliona hata hapa kwetu wataalamu wa afya na madaktari bingwa wakialikwa kutolea ufafanuzi.

Ghafla bin vuu anaibuka mtu anaitwa Steve Nyerere eti anapewa ubalozi wa kuhaamasisha chanjo. Steve anajua nini kuhusu chanjo?

Akipigwa maswali mawili tu hataweza kujibu chochote kile kutokana na kutokua na elimu yoyote achilia mbali elimu ya afya ya binadamu, lakini Leo eti nae ni balozi.

Inashangaza na kusikitisha wizara kuandaa kampeni ya kutoa elimu ya chanjo alafu mtu Kama Steve nyerere anakua speaker. Nae anatoa elimu, sitaki kuamini hatuna wataalamu wa kutosha.

Waziri gwajima kuwa serious kwenye hili suala, kumbuka suala la kuhaamasisha masuala ya kitaalamu yanapaswe yaende kitaalamu maana Kuna watu wana maswali yao magumu na yasipojibiwa kitaalamu yatawafanya wakatae.
 
kama wa tz walimuamini sana magu na askofu rashidi, wakaacha kuwaamini wataalam wa Afya basi usishangae na saiv watu watachanjwa kisa ushawishi wa steve nyerere
 

Steve Nyerere analipwa Na nani hii kazi ya ubalozi wa Chanjo au pesa tayari zimemwagwa hapa Tanzania na wenye Chanjo
 
Waokoe pesa za serikali,hatuhitaji mabalozi wa chanjo.
Huyo Steve hana mvuto kabisa,pia ana sifa mbaya kule kwenye kuchangisha misiba ya wasanii.
 
Nani kasema wanataka kuulizwa au kujibu hayo maswali? ukihoji kuhusu hizo chanjo unaonekana ni mpinga chanjo na kuwekwa kwenye kundi moja na Gwajima, wao wanachojua ni kusema tu kuwa chanjo ni hiari basi.
 
Hii wizara ya Afya ni miongoni mwa wizara muhimu na nyeti katika nchi ila inaendesha mambo HOVYO sana. Wizara yenye maprofesa na wataalamu kedekede wabobezi wa afya leo hii wanatumia darasa la saba kuhamasisha wananchi kuchanja!

Uwezo wetu wa kufikiri huwa tunauweka wapi katika mambo muhimu kama haya, mlishindwa kumwamini huko kwenye chama kwenye suala la ubunge leo wizara inaona huyo ni mtu sahihi kuwa balozi wa chanjo?

Tuacheni siasa kwenye afya za watu, kuna vijana ni wazuri na vichwani mwao wamebeba mustakabali wa afya za wananchi kwanini msiwape nafasi watupe elimu na si kubeba kila mtu ili mradi akiachama kinywa chake maneno yatatoka.

Mh. Rais Samia ikikupendeza rekebisha hii wizara ni miongoni mwa wizara inayoendelea kutia doa serikali yako.
 
Kuna mstari mwembamba sana unaowatofautisha steve nyerere na dk gwajima.
 
Back
Top Bottom