Ila yule mhe. Sijawahi kumuelewa kabisa alipewa shavu la kuwa naibu waziri wa afya baada ya kupinga vikali bungeni chanjo na lockdown ila sasa yeye Tena ndio Kawa mstari wa mbele kutetea chanjo ..njaa hizi zinatudhalilisha Sana.Sasa Dr Mollel na Steve Nyerere wana tofauti gani?
Hapa hebu tutulie kidogo. Ukisema hivi, unamaanisha jamii ipi hiyo ambayo Steve hawezi kuihudumia? Ni nani huyo wa kumuuliza hayo maswali mawili? Kama Profesa tu anakunywa dawa isiyothibitishwa kitaalamu kwa lengo tu la kughilibu uma, halafu baadae tunaambiwa ile kitu alikunywa ni sampuli,inafanyiwa uchunguzi mpaka leo jii. Au unazungumzia nchi hiihii ambapo wataalamu wa tiba walijenga mtambo wa kujifukiza mahospitalini kwa nia ya kutibu Covid na leo hii wanahamasisha chanjo? Kama haitoshi, unaongelea raia ambao wanaamini kiongozi wao aliweza kuondoa Corona kimiujiza tu? Unaongelea jamii ambayo si prof, si la saba na wala si PhD wanaamini kikombe cha marehemu Ambilikile (Babu) ni tiba ya magonjwa sugu?Kuna vitu vinashangaza sana, wizara ya afya inashangaza sana. Wote tumeshuhudia duniani kote suala la chanjo likiwa mjadala mkubwa sana ambapo kila aina ya utaalam unatumika kwa wanaokubali na wanaoipinga.
Hivyo si suala la kisiasa wala propaganda bali ni la kisanyansi, ndio maana niliona hata hapa kwetu wataalamu wa afya na madaktari bingwa wakialikwa kutolea ufafanuzi.
Ghafla bin vuu anaibuka mtu anaitwa Steve Nyerere eti anapewa ubalozi wa kuhaamasisha chanjo. Steve anajua nini kuhusu chanjo?
Akipigwa maswali mawili tu hataweza kujibu chochote kile kutokana na kutokua na elimu yoyote achilia mbali elimu ya afya ya binadamu, lakini Leo eti nae ni balozi.
Inashangaza na kusikitisha wizara kuandaa kampeni ya kutoa elimu ya chanjo alafu mtu Kama Steve nyerere anakua speaker. Nae anatoa elimu, sitaki kuamini hatuna wataalamu wa kutosha.
Waziri gwajima kuwa serious kwenye hili suala, kumbuka suala la kuhaamasisha masuala ya kitaalamu yanapaswe yaende kitaalamu maana Kuna watu wana maswali yao magumu na yasipojibiwa kitaalamu yatawafanya wakatae.
We jamaa mkorof sanaSasa Dr Mollel na Steve Nyerere wana tofauti gani?
Acha maskhara kwani hatujui kama tunawaziri komedianDr Gwajima kwa hili la Steve Nyerere katia aibu ya mwaka, sielewi waziri anakuwa kama comedian