Kuna Manabii wa uongo, je Manabii wa kweli ni wepi?

Kuna Manabii wa uongo, je Manabii wa kweli ni wepi?

Donatila

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2014
Posts
7,772
Reaction score
22,598
Habari wakuu,

Husika na kichwa cha habari,

Kama kuna jambo ambalo lilikuwa likiniwazisha ni namna ya kumjua Nabii wa uongo na wa kweli.

Nilisikia habari hizi kutoka katika mahubiri kanisani tokea nilipokuwa mdogo.

Kifupi habari hizi ziliniitisha maana sikuwa najua ya kuwajua Manabii.

Nikakua bado nilisikia tu niendelea kusikia habari za kuja Manabii wa uongo.

Mpaka sasa bado nazisikia habari hizi za Manabii wa uongo.

Watu wanasema Manabii wa uongo tu, je hakuna Nabii wa kweli?

Kama yupo ni yupi?

Wamemjuaje huyo Nabii ni wa kweli?

Biblia inasema neno 1Yohana 4:1
Wapenzi msiamini Kila roho, bali zijaribuni hizo roho, bali ziketoka kwa Mungu

Mathayo 7:15
Jihadharini na Manabii wa uongo, watu wanaowajiq wamevaa ngozi ya kondoo lakini ndani ni mbwa mwitu

Mwl Mwakujonga Rabbon
 
Manabii waliopo sasa wote ni wauongo kwahiyo usidanganyike.
Na manabii WA ukweli wapo kwenye vitabu vya dini mbili hizo ukristo na uislamu na wote washatangulia Kwa mungu na MUNGU aleti tena nabii mpya.
Waliopo sasa ni viongi WA dini tu.
Naimani umenielewa
 
Mtawatambua kwa matunda yao
Mara nyingi wanatenda kinyume na neno la Mungu
Wanauza huduma za Mungu, wanapenda pesa, ni waongo, wanafiki, wabinafsi, wachoyo, wasinginziaji, wasengenyaji,
Hawakemei maovu ya watu na ya serikali ya CCM na hawalipi kodi.
 
Hakuna nabii miaka hii tofauti na wale waliopo kwenye biblia ama Quran tukufu. Ila kuna makanjanja walaghai
 
Nabii Maliyabwana au Meshack ni MMOJA wa manabii wa Kweli.

Na ametoa video nyingi U-Tube channel kuelezea na kutofautisha manabii wa Kweli na wa UONGO. Channel hiyo Inaitwa UKWELI ministries.ya Nabii/ mtume Maliyabwana.

View videos hizo na njoo uelezee ktk Uzi wako Kwa kadri Roho mtakatifu atakavyokuongoza.

Hizi ni baadhi ya sifa za manabii wa uongo.

1. Ni wazinzi, wanawake wengi hubakwa au kuingiliwa na hao., So many scandals.

2. Wengi huhubiri INJILI ya mafanikio, utajiri Mali nk nk.

3. Hawahubiri INJILI ya Utakatifu, hawakemei dhambi Ili waumini wasikimbie, hawakatazi mapambo na wigi ,suruali, UZINZI, mtu ana wake wawili na anasali na hakemewi , walevi, Mafisadi nk nk.

4. Hawalitaji Jina la YESU, utawasikia wakisema njoo Kwa Mungu wa mtume Fulani, nk nk.

5. Mwisho wa IBADA hawathubutu kuwaita watu waje kuokoka. Maana Nia Yao ni kuwapoteza watu.

6. Wanabagua maskini, mtu mwenye pesa ndo hupewa uongozi na kuthaminiwa bila kujali pesa amepata vipi.

7. Hawatumii Jina la YESU kuponya, utaona chumvi, udongo, mafuta mifagio nk nk

8. Ukiona anatoza kiingilio kumuona, ni Nabii wa uongo huyo.

Manabii wa Kweli wa Mungu.

Mwl MWAKASEGE, Mchungaji Abiudi, Askofu Mwamakula, Askofu Gwajima, Mchungaji Mbarikiwa, Mtume Maliyabwana wa UKWELI Ministries, Askofu Gamanywa na wengine wengi sijawataja, Roho MTAKATIFU akuongoze kuwatambua.

ANGALIZO: Kuwatambua manabii wa Kweli na uongo, ni vyema uombe Mungu akufunulie, maana Manabii wengi Walio wa UONGO Leo, walikuwa wa Kweli zamani, walipoona hawana pesa, wakaamua kwenda Kwa Waganga kuongeza nguvu, mwisho wakawa wa Uongo, Mfano mzuri ni Lusek.. na Mwingir....!!

Hivyo, usiweke Imani Yako Kwa Mtu, Mungu akuongoze, maana mtumishi wa Kweli pia anaweza kujaribiwa na kuingia kuwa wa uongo.

Amen
 
Manabii waliopo sasa wote ni wauongo kwahiyo usidanganyike.
Na manabii WA ukweli wapo kwenye vitabu vya dini mbili hizo ukristo na uislamu na wote washatangulia Kwa mungu na MUNGU aleti tena nabii mpya.
Waliopo sasa ni viongi WA dini tu.
Naimani umenielewa
Acha uongo.
 
Habari wakuu,

Husika na kichwa cha habari,

Kama kuna jambo ambalo lilikuwa likiniwazisha ni namna ya kumjua Nabii wa uongo na wa kweli.

Nilisikia habari hizi kutoka katika mahubiri kanisani tokea nilipokuwa mdogo.

Kifupi habari hizi ziliniitisha maana sikuwa najua ya kuwajua Manabii.

Nikakua bado nilisikia tu niendelea kusikia habari za kuja Manabii wa uongo.

Mpaka sasa bado nazisikia habari hizi za Manabii wa uongo.

Watu wanasema Manabii wa uongo tu, je hakuna Nabii wa kweli?

Kama yupo ni yupi?

Wamemjuaje huyo Nabii ni wa kweli?

Biblia inasema neno 1Yohana 4:1
Wapenzi msiamini Kila roho, bali zijaribuni hizo roho, bali ziketoka kwa Mungu

Mathayo 7:15
Jihadharini na Manabii wa uongo, watu wanaowajiq wamevaa ngozi ya kondoo lakini ndani ni mbwa mwitu

Mwl Mwakujonga Rabbon
kutambua nabii wa uongo au nabii wa ukweli ni lazima uwe na msingi mzuri wa malezi ya wazazi, kanisa na Jamii inayokuzunguka.

Na kuanzia hapo sasa,
Ufahamu na Uelewa wako kwa muongozo wa Roho mtakatifu utakua mkubwa na dhahiri kutambua na kubaini huyu nabii ni wa kutoka ufalme wa Nuru na nabii huyu ni wa kutoka ufalme Giza.

Kwa uchache sana...
 
Hakuna nabii miaka hii tofauti na wale waliopo kwenye biblia ama Quran tukufu. Ila kuna makanjanja walaghai
(Wagalatia 1:8)

Lakini ijapokuwa sisi au Malaika wa Mbinguni atawahubiri ninyi INJILI yoyote, isipokuwa hiyo tuliyowahubiri, na ALAANIWE.

Quran imeletwa baada ya Yesu kufufuka, hivyo ni nafundisho wa uongo ya kupotosha.

Nawaombea waislamu watubu, watoke kwenye nafundisho ya uongo.

Amen
 
Nabii ni mtu anaepokea ujumbe kutoka kwa Mungu na kuutangaza kwa watu.

swali la kujiuliza huyo kiumbe anaeitwa Mungu je ni kweli yupo? Utadhibitisha vipi uwepo wake ?

Mafundisho mengi ya dini yanaelezea uwepo wa kiroho wa Mungu ndani ya watu. Kwa mfano, katika Ukristo, 1 Wakorintho 3:16 (Neno: Bibilia Takatifu) inasema, "Je, hamjui ya kuwa ninyi ni hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?" Hii inaonyesha wazo la uwepo wa Mungu ndani ya waumini kwa njia ya Roho Mtakatifu.

Kama roho wa Mungu anakaa ndani yenu ya nini sasa kuwa na nabii kama msemaji wa Mungu tena katikati ya
watu wake ambao tayari yupo ndani yao?
 
Habari wakuu,

Husika na kichwa cha habari,

Kama kuna jambo ambalo lilikuwa likiniwazisha ni namna ya kumjua Nabii wa uongo na wa kweli.

Nilisikia habari hizi kutoka katika mahubiri kanisani tokea nilipokuwa mdogo.

Kifupi habari hizi ziliniitisha maana sikuwa najua ya kuwajua Manabii.

Nikakua bado nilisikia tu niendelea kusikia habari za kuja Manabii wa uongo.

Mpaka sasa bado nazisikia habari hizi za Manabii wa uongo.

Watu wanasema Manabii wa uongo tu, je hakuna Nabii wa kweli?

Kama yupo ni yupi?

Wamemjuaje huyo Nabii ni wa kweli?

Biblia inasema neno 1Yohana 4:1
Wapenzi msiamini Kila roho, bali zijaribuni hizo roho, bali ziketoka kwa Mungu

Mathayo 7:15
Jihadharini na Manabii wa uongo, watu wanaowajiq wamevaa ngozi ya kondoo lakini ndani ni mbwa mwitu

Mwl Mwakujonga Rabbon
UKIONA YAFUATAYO JUA NI DALILI LA NABII WA UONGO AU KANISA LA UONGO
1. Kanisa lolote/mchungaji anayehubiri kwamba tunahesabiwa haki kwa sheria, sio neema.

2. mtumishi yeyote ambaye ili kumuona unatoa pesa,

3. yeyote anayeoza mafuta ya upako, chumvi,maji n.k

4. yeyote anayeitisha nywele za utosi, kucha au kuosha miguu

5. yeyote anayetangaza kukomboa ardhi,kukomboa pesa,nyumba au mwili kwa sadaka

6. yeyote anayeamini unatakiwa kukomboa laana iliyoko maishani mwako wakati tunajua Yesu Kristo alibeba laana zetu pale msalabani hivyo ukimwamini anakukomboa toka kwenye laana zote, unakuwa mali yake kiumbe kipya kabisa.

7. mtumishi anayependa kujitukuza kama yule wa Kisongo Arusha.

8. mtumishi mwenye wapambe kama yule wa kimara temboni, malawi na masalia yake hapa tz. wapambe yaani mtumishi akiongea kuna kuwa na lijamaa fulani limeshika kipaza sauti linapambisha pambisha yale anayosema mtumishi. wanajaribu kuhamasisha kwa njia ya mwili kumbe maneno yeyote yenye Roho Mtakatifu hayahitaji nguvu ya mwili kuhamasisha au kuleta badiliko.

9. nabii yeyote anayetabiri mabaya tu na anasema tuombe na bado yanatokea. kama waganga wa kienyeji wanaweza kutabiri mabaya, au wakatabiri ukoo wako, au majina yako kama kale kajamaa kahaya branch ya nabii wa malawi tapeli wa south africa na wengine wa uingereza, just to mention a few.

10. wachungaji majority ambao ni masharobaro (though sio wote), ni matapeli. kwanza anapeda kuva vizuriii, gari za garamaaa, analindwa na mabodigadiiiii, ana kiburiii cha pesa...wote hao ni wa ibilisi.

11. wachungaji wote ambao ukimsikiliza akiomba, haamuru kwa JIna la Yesu, ila kwa mamlaka yake yeye mwenyewe, kama yule wa arusha, na wengine.

12. mchungaji yeyote anayepinga na kukosoa Biblia, kama yule wa Arusha na mzee wa neema. wanajiita wakristo ila wanaamin Biblia ina mapungufu, still bado wanaitumia na katika maombi yao hawatumii Jina la Yesu ila mamlaka yao binafsi.watajitahidi hawatataja JIna hilo manake linawaumiza.

13. makanisa yote ambayo hayahamasishi kumtafuta na kumpata Roho Mtakatifu awe kiongozi wako, hilo limepoa na sio kanisa la Kimungu. Roho Mtakatifu lazima umtafute ajae, kwani ndiye atakiusaidia kwenye maombi, kwenye uongozi n akutambua mabaya hata yale yasiyoandikwa kwenye Biblia, pia ni moto ulao akiwa ndani yako ni kwamba Mungu yupo ndani yako hivyo shetani hatakusogelea kirahisi. (labda umruhusu wewe mwenyewe). makanisa ya katoliki, sabato, lutheran (wasio wanafeloshipu au uamsho), mashahidi wa jehova na wengine woote wasio na mfumo wa ujazo wa Roho Mtakatifu, hao sio wa Mungu, kimbia.

14. makanisa yote yanayoruhusu unywaji wa pombe kama katoliki na mengine, wale wenye wachungaji walevi kama mzee wa bapa, kimbia.

wengine ngoja niachie wenzangu.
 
Manabii waliopo sasa wote ni wauongo kwahiyo usidanganyike.
Na manabii WA ukweli wapo kwenye vitabu vya dini mbili hizo ukristo na uislamu na wote washatangulia Kwa mungu na MUNGU aleti tena nabii mpya.
Waliopo sasa ni viongi WA dini tu.
Naimani umenielewa
Are you serious kwenye uislamu kuna manabii? Mudi ni nabii kweli
 
And the good book says.... "Mtawatambua kwa matendo yao"

Kila mtu hajapewa roho mtakatifu, ila kila mtu amepewa akili. Kuna vitu havihitaji roho kuvifahamu.
 
Simpo tu

Wa kweli ataihubiri KWELI

Wa uongo atauhubiri UONGO.

Lakini bado sio vema kumweka kundi kwamba huyu ni wa uongo huyu ni wa kweli. Nabii mmoja anaweza kisema ile kweli na huyohuyo kuna wakati akapitiwa maana naye ni binadamu akasema/hubiri au tenda uongo. Tusipende kuwahukumu kabla hawajafa na wanaweza kurekebisha makosa kama yapo.

Mfano hapo juu si nimeandika ukweli eeh: Basi Uhakika bro ni nabii wa kweli, au nasema uongo ndugu zangu?
 
Nabii ni mtu anaepokea ujumbe kutoka kwa Mungu na kuutangaza kwa watu.

swali la kujiuliza huyo kiumbe anaeitwa Mungu je ni kweli yupo? Utadhibitisha vipi uwepo wake ?

Mafundisho mengi ya dini yanaelezea uwepo wa kiroho wa Mungu ndani ya watu. Kwa mfano, katika Ukristo, 1 Wakorintho 3:16 (Neno: Bibilia Takatifu) inasema, "Je, hamjui ya kuwa ninyi ni hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?" Hii inaonyesha wazo la uwepo wa Mungu ndani ya waumini kwa njia ya Roho Mtakatifu.

Kama roho wa Mungu anakaa ndani yenu ya nini sasa kuwa na nabii kama msemaji wa Mungu tena katikati ya
watu wake ambao tayari yupo ndani yao?
Soma zaidi, kuielewa BIBLIA unahitaji ufunuo na uongozi wa Roho mtakatifu.

Ni Kweli, Roho mtakatifu anaishi ndani yetu na mwili ni HEKALU la Mungu.

Jua pia kuwa, Vipawa anagawa Roho mtakatifu, wote hawawezi kuwa wahubiri, walimu, mitume, watembelea wagonjwa, watenda miujiza Kwa wakati mmoja.

MWILI ni HEKALU, na sisi tu viungo katika mwili wa Yesu Kristo while KICHWA Cha mwili huo na Kanisa ni Yesu Kristo.

Petro na Paul walikuwa viongozi wa waamini wengine baada ya Yesu kufufuka.

Ubarikiwe.
 
Soma zaidi, kuielewa BIBLIA unahitaji ufunuo na uongozi wa Roho mtakatifu.

Ni Kweli, Roho mtakatifu anaishi ndani yetu na mwili ni HEKALU la Mungu.

Jua pia kuwa, Vipawa anagawa Roho mtakatifu, wote hawawezi kuwa wahubiri, walimu, mitume, watembelea wagonjwa, watenda miujiza Kwa wakati mmoja.

MWILI ni HEKALU, na sisi tu viungo katika mwili wa Yesu Kristo while KICHWA Cha mwili huo na Kanisa ni Yesu Kristo.

Petro na Paul walikuwa viongozi wa waamini wengine baada ya Yesu kufufuka.

Ubarikiwe
Uwepo wangu tu ni baraka tosha, roho mtakatifu ni yupoje dhibitisha apa ili niamini uwepo wa hicho kiumbe.
 
Uwepo wangu tu ni baraka tosha, roho mtakatifu ni yupoje dhibitisha apa ili niamini uwepo wa hicho kiumbe.
Mungu akusaidie.

Roho mtakatifu ni ROHO wa YESU kristo. Ukimpokea Yesu, utapokea zawadi ya Roho mtakatifu. Anaishi ndani ya WATAKATIFU.
 
Back
Top Bottom