Pre GE2025 Kuna Mawaziri wanatamba kwenye Wizara zao lakini majimboni kwao hali mbaya

Pre GE2025 Kuna Mawaziri wanatamba kwenye Wizara zao lakini majimboni kwao hali mbaya

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
Salaam Wakuu,

Kuna baadhi ya Mawaziri wamekuwa wanang'aa sana kwenye vyombo vya habari na kusifika wa kufanya kazi nzuri katika wizara zao lakini majimboni kwao hali ni mbaya sana. Miundombinu mibovu na matatizo ya msingi kwenye maeneo yao hawayafanyii kazi.

Hapa najiuliza Uwaziri umekuwa mzigo mzito sana kiasi cha wao kushindwa kutimiza majukumu ya majimboni kwao au la. Binafsi ni mkazi wa Jimbo la Ukonga. Mbunge wetu anatamba sana kwenye Wizara yake kwa sasa lakini maeneo ya huku kwetu hali ni mbaya sana barabara hazipitiki. Mbunge wetu hakai nasisi tunamuona tu anatamba na uwaziri.

Binafsi naona ipo haja tutenganishe Ubunge na Uwaziri ili tuwatendee haki Wananchi wanaomchagua kiongozi kuwawakilisha na kuwatetea.

Nawasilisha
 
Salaam Wakuu,

Kuna baadhi ya Mawaziri wamekuwa wanang'aa sana kwenye vyombo vya habari na kusifika wa kufanya kazi nzuri katika wizara zao lakini majimboni kwao hali ni mbaya sana. Miundombinu mibovu na matatizo ya msingi kwenye maeneo yao hawayafanyii kazi.

Hapa najiuliza Uwaziri umekuwa mzigo mzito sana kiasi cha wao kushindwa kutimiza majukumu ya majimboni kwao au la. Binafsi ni mkazi wa Jimbo la Ukonga. Mbunge wetu anatamba sana kwenye Wizara yake kwa sasa lakini maeneo ya huku kwetu hali ni mbaya sana barabara hazipitiki. Mbunge wetu hakai nasisi tunamuona tu anatamba na uwaziri.

Binafsi naona ipo haja tutenganishe Ubunge na Uwaziri ili tuwatengdee haki Wananchi wanaomchagua kiongozi kuwawakilisha na kuwatetea.

Nawasilisha
hakuna haja ya kutenganishwa ubunge na uwazri, kama ni mzigo mnayo fursa uchaguzi mkuu kumpeleka nyumbani 🐒
 
Taja Majina ya hao Mawaziri tuwajue vizuri

Jibu utakalopewa maendeleo ya Jimboni SIO kazi ya Mbunge bungeni Mbunge akiwa bungeni kazi yake ni kutunga Sheria utaambiwa kazi ya maendeleo Jimboni hufanywa na Baraza la Madiwani wakishirikiana na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa

Haya maelezo yaliwahi kunifanya nikapigwa Ban Ila ukweli mchungu
 
Back
Top Bottom