Kuna nafasi ya kupata Katiba Mpya bila kumwaga damu lakini viongozi wamekuwa vipofu

Kuna nafasi ya kupata Katiba Mpya bila kumwaga damu lakini viongozi wamekuwa vipofu

chotera

JF-Expert Member
Joined
May 19, 2016
Posts
6,560
Reaction score
15,864
Ifikie hatua tuseme ukweli.

Huwezi mchakato wa mzee Warioba ukaukejeli mchana kweupe ukidhani ni sawa kumbe unatafuta laana tu ya bure.

Tanzania inanafasi kubwa ya kupata katiba mpya na bora toka tume za akina jaji kisanga, jaji Nyalali, Jaji Warioba.

Nawaza jinsi mataifa mengi yaliyopata katiba mpya baada ya kumwaga damu ya wananchi wake kwa uzembe wa viongozi.

Hakuna sababu ya delay wakati nafasi na muda wa kufanya mambo kwa amani upo.

Hofu kubwa ya CCM utakuta ni muungano hawana hoja zaidi ya hiyo.

Viongozi fungukeni macho mkaangalia maslahi ya leo mkaacha maslahi ya kesho ya Mama Tanzania ni dhambi kubwa.

Mtaleta ujanjaujanja lakini utatugharimu kama taifa mbele ya safari huko baadae.

Uongozi ufanyiwe reformation ili tuweze kua na utawala bora wa dunia ya leo, mambo ya kukumbatia sera za ujamaa na uongozi wa miaka ya 1970 ni kupotezea muda wananchi ambao hata hawahitaji story za uongo na kweli.
 
Nchi ngumu huu kiukweli hatufiki popote japo mabadiliko tunayaita maendeleo ila ukichunguza ni speed Kali kuelekea shimoni.
 
Back
Top Bottom