Kuna nini clouds media?

What is happening? Ee Mungu saidia hii jamii
 
Pigo tena kwa muziki wa Bongo Fleva baada ya ripoti kusema, M To The P aliyekuwa na Mangwea jijini Johannesburg naye amefariki dunia.

Taarifa kutoka Johannesburg zinaeleza M To The P amefariki dunia baada ya kulazwa katika hospitali ya St Helen Joseph ambayo mwili wa Mangwea umehifadhiwa.

Mangwea na M To The P walisafiri pamoja hadi Afrika Kusini kwa ajili ya kufanya onesho (show) na baadaye waliendelea na maisha, lakini jana Mangwea alikutwa amefariki dunia chumbani na M To The P akiwa taabani na kulimbizwa hospitalini.

"Kweli amefariki dunia, ni yule mwenzake na Mangwea, sasa tuko kwenye pilikapilika ya kuandaa mazishi," alisema Thomas, mmoja wa Watanzania wanaoshughulikia suala la mazishi.

Source: wavuti.com - Blog
 
Majani kakoleza majini kichwani angalau amepata pa kuibukia kazi mnayo clouds ! Chezea ndumu wewe...
 
Nadhani kwa wale ambao walikuwa hawamuelewi Lady Jay Dee nadhani jibu mmeanza kuliona. Hawa Jamaa wa Clouds wanaojifanya radio ya watu wana watu wao ambao wao wanapenda wawe wanasikika tuu . na kama mnabisha fanyeni research mtagundua wasanii wa THT wanapata kiasi gani cha airtime pamoja na wale ambao wana tow the line.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…