Kuna office nimeitembelea leo,office nzima mpaka mkurugenzi hawajui kuongea Kiingereza

kyagata

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2016
Posts
10,406
Reaction score
19,892
Hii nchi ina vituko sana.

Kuna wageni kutoka marekani wametembelea Tanzania kujifunza mambo flani flani,boss wangu akaniteua mimi na wenzangu wawili tuwaongoze kwenye shughuli zao zilizowaleta.

Cha ajabu kuna office tumeenda leo,office nzima hakuna anayeweza kuongea kiingereza kizuri,hadi mkurugenzi wa office ni zero kwenye kiingereza, eti mkurugenzi akanivuta pembeni akaniambia hayuko vizuri kiafya hivyo anaomba anikabidhi kwa meneja wake ili atusaidie shida yetu,

Meneja nae akazuga eti yuko busy lkn baadae akanivuta pembeni akaniambia huwa anapata shida kuelewa accent ya kimarekani hivyo anaomba niwe namtafsria wanachoongea hawa wageni.
Nimeshangaa sana aisee.
 
Mbona kawaida tu, baada ya yote kiingereza sio kipimo cha kuwa na akili nyingi. Ni kimatumbi cha wazungu tu.

Kama mpaka wana ofisi ya hadhi ya kutembelewa basi ni wazi kiingereza hakina umuhimu kwao.
 
Kiingereza ni lugha tu kama lugha zingine mfano Kimatumbi, kisukuma kiswahili n.k
 
Wateja wao wakubwa ni wakina nani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…