Kuna sababu za kitaalamu gari ikiwa na mafuta tank limejaa inatumia mafuta kidogo?

Kuna sababu za kitaalamu gari ikiwa na mafuta tank limejaa inatumia mafuta kidogo?

mbere

JF-Expert Member
Joined
Mar 5, 2015
Posts
6,967
Reaction score
6,465
Wakuu naomba Kama kuna sababu za kitaalamu nikijaza mafuta inatumia kidogo tofauti na nikiwa na mafuta chini ya tank kwa mizunguko Ileile.
 
Unachoamini siku zote huwa ndivyo.
Amini hivyo mkuu kwa kuwa una imani hiyo itakusaidia.
Lkn kitaalamu kuna ukweli upo mi mwenyewe nina gari nikijaza full tank kwa mwezi natumia laki 1 na nikipima pima lita 5 kila yakiisha kwa mwezi natumia laki na 30
 
Sio kweli! Kinachotokea hapo ni kitu kidogo tu. Unapoweka full tank maana yake hata reserve chamber zinakuwa full. Jambo ambalo husababisha mafuta yanayotumika kufidiwa na yale ya reserve na hivyo kuifanya gage yako iendelee kusoma full...wewe hapo huona mafuta bado yamejaa, lkn inapotokea reserve imetumika, yale mafuta yanayoratibiwa na kipimo chako huanza kutumika na hapo utaanza kuona mshale unasoma kama kawaida..
Nijuavyo Mimi ni kwamba trip za hapa na pale hutumia mafuta mengi kuliko trip ndefu ama long safari, hii hasa ni kwa magari ya petrol. Sababu kubwa ni mfumo wa uchomaji wa mafuta.. Gari za petrol zina mfumo ambao ili mafuta yaingie kwenye mzunguko, ni lazima kwanza yachomwe! Sasa pale mafuta yanapokuwa yameunguzwa tayari kuingia kwenye mzunguko na wewe ukazima gari, maana yake ni kwamba mafuta hayo yatakuwa hayana kazi pindi utakapowasha tena gari kwani yatahitajika mafuta mapya yachomwe ili kuendelea na mzunguko!
Hii ni sababu ya wazi kitaalamu. Hata hivyo, zipo sababu nyingi zinazochangia mabadiliko ya ulaji wa mafuta kwenye gari, mfano njia unayopita, uzima wa gari lako na vipuri vyake, aina ya uendeshaji n.k.
 
Gari za petrol zina mfumo ambao ili mafuta yaingie kwenye mzunguko, ni lazima kwanza yachomwe!
Mkuu, kwenye hiyo aya, naomba ufafanuzi wa MAFUTA KUCHOMWA KWANZA na KUINGIA KWENYE MZUNGUKO, sijaelewa unaposema mafuta ni lazima yachomwe kwanza, yanachomewa wapi? Yanaingia kwenye mzunguko upi?
 
Wajinga mtaani unakuta wanawaambia watu kuwa jaza kabisa yatachelewa kuisha
 
Back
Top Bottom