Wadau salamu!
Naomba mwenye kujua anisaidie. Nina kampuni mbili zenye shughuli tofauti, nimeamua niziweke ktk ofisi moja ili kuepuka gharama za pango lkn pia ziwe chini ya meneja mmoja. Naomba kama kuna kosa ki sheria mniambie kabla sijafanya hivyo. Natanguliza shukrani.
Inategemea na shughuli za hizo company. Kuna baadhi kisheria hairuhusiwi na sheria mama kufanya hivo unavotaka kufanya. Kuna baadhi ya field zinakua monitored na Ethics zake.
Ila kama company zote zina deal na maswala ya business then unaruhusiwa.
Mfano, company inaojihusisha na maswala ya sheria hairuhusiwi kisheria kuwa office moja na company inayo deal na maswala yasio ya kisheria.
labda kama zinahusu aina fulani ya taaluma kama uhasibu, sheria nk, ila hakuna kosa ila kuna issue za kodi lazima ziwe wazi kwenye matumizi kwa kilia kampuni, mfano rent lazima ijulikane na tra wajue kila kampuni italipa kiasi gani
Mkuu Hilo linawezekana ili mradi tu hizo kampuni zote uzilipie kodi.
Lakini pia inategemea aina ya hizo kampuni.
Kwa mfano huwezi kuwa na hospitali halaf humo humo ukaweka mashine ya kusaga,au ukumbi wa disco.