Kuna siku mgogoro huu wa Kikatiba utaibuka na utaitingisha nchi

Kuna siku mgogoro huu wa Kikatiba utaibuka na utaitingisha nchi

Keynez

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2007
Posts
2,428
Reaction score
3,937
Katiba ya sasa ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na sheria zetu za uchaguzi zinataka mtu ukigombea nafasi yoyote ya kisiasa ni lazima uwe mwanachama wa chama cha siasa kilichosajiliwa na kinachotambulika.

Kwa msingi huu wa sheria ina maana ukipoteza unachama wako ina maana umepoteza pia sifa za uongozi wowote ulio nao ambazo msingi wake ni huo unanachama. Hapa naongelea Ubunge, Uwaziri na hadi Urais.

Kuna siku ambayo mtu tayari ni Rais wa JMT halafu ndani ya chama chake kukatokea mgogoro akafukuzwa au kusimamishwa unachama. Yatazuka maswali uhalali wake wa kuendelea kuwa Rais wa JMT.

Sikumbuki vizuri kisa cha wale Covid 19 wa CHADEMA kina Mdee na shoga zake kama walifukuzwa au kusimamishwa na chama ila ni case mojawapo ya mapungufu ya katiba na sheria tuliyonayo na jinsi ambavyo wakati mwingine tunaisigina katiba.

Tunaenda na haya mapungufu hivyo hivyo tu lakini kuna maeneo ambapo mkanganyiko ni mkubwa na kuna siku utakuwa mkubwa sana.
 
Kwa nchi hii Rais wa JMT kufukuzwa uanachama ni jambo lisilowezekana kabisa
Katiba ya sasa ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na sheria zetu za uchaguzi zinataka mtu ukigombea nafasi yoyote ya kisiasa ni lazima uwe mwanachama wa chama cha siasa kilichosajiliwa na kinachotambulika.

Kwa msingi huu wa sheria ina maana ukipoteza unachama wako ina maana umepoteza pia sifa za uongozi wowote ulio nao ambazo msingi wake ni huo unanachama. Hapa naongelea Ubunge, Uwaziri na hadi Urais.

Kuna siku ambayo mtu tayari ni Rais wa JMT halafu ndani ya chama chake kukatokea mgogoro akafukuzwa au kusimamishwa unachama. Yatazuka maswali uhalali wake wa kuendelea kuwa Rais wa JMT.

Sikumbuki vizuri kisa cha wale Covid 19 wa CHADEMA kina Mdee na shoga zake kama walifukuzwa au kusimamishwa na chama ila ni case mojawapo ya mapungufu ya katiba na sheria tuliyonayo na jinsi ambavyo wakati mwingine tunaisigina katiba.

Tunaenda na haya mapungufu hivyo hivyo tu lakini kuna maeneo ambapo mkanganyiko ni mkubwa na kuna siku utakuwa mkubwa sana.
 
Kwa kuwa hamna wenye mamlaka wanaoheshimu sheria wala katiba (hata hii mbovu) basi hamna mgogoro utatokea na ukawa serious, kwanza hamna wanachama wenye ujasiri wa kumfuta uanachama member wao akiwa ni rais, kwa sababu kwao ni chakula! Wabongo kwenye chakula wanashirikiana na kufunika kila haramu hata kwnye level ya familia acha taifa
 
CCM kwa kulijua hilo ndio maana Rais ndio mwenyekiti wa chama na ndie anateuwa Katibu mkuu wa cahama na makamu wenyeviti bara na visiwani, kwa msingi huo usiatarajie Rais wa JMT kufukuzwa uanachama hata hivi vyama vingine vikiingia madarakani sio rahisi kumfukuza uanacha Rais wa Nchi
 
Kwa kuwa hamna wenye mamlaka wanaoheshimu sheria wala katiba (hata hii mbovu) basi hamna mgogoro utatokea na ukawa serious, kwanza hamna wanachama wenye ujasiri wa kumfuta uanachama member wao akiwa ni rais, kwa sababu kwao ni chakula! Wabongo kwenye chakula wanashirikiana na kufunika kila haramu hata kwnye level ya familia acha taifa
Yule wa Zanzibar alieondolewa madarakani vp? Mtoa mada anahoja ila wewe unaiangalia kwa jicho la chini kabisa. Huyo Rais siyo kitu kama CDF na mkuu wa TISS wasipompatia back-up. Hicho ndicho mgogoro kinachosemwa, tusiishi kwa mazoea. Au hukumbi kama kuna watu wengine hawakutegemea kama Rais anaweza kufia madarakani hapa Tanzania.
Madhara yake wakawa wanachagua Bwana mkasi bora liende.
 
Yule wa Zanzibar alieondolewa madarakani vp? Mtoa mada anahoja ila wewe unaiangalia kwa jicho la chini kabisa. Huyo Rais siyo kitu kama CDF na mkuu wa TISS wasipompatia back-up. Hicho ndicho mgogoro kinachosemwa, tusiishi kwa mazoea. Au hukumbi kama kuna watu wengine hawakutegemea kama Rais anaweza kufia madarakani hapa Tanzania.
Madhara yake wakawa wanachagua Bwana mkasi bora liende.
Sikukatazi kufikiria unavyotaka ila sio kwa Tz, hizo wishful thoughts ni za kizazi kijacho sio hiki cha leo! Tuendelee kushehekea ujio wa wasira labda atapush katiba mpya maana hana cha kupoteza wakimpa energy drinks though! Kuna cdf au mkuu wa Tiss attaenda kinyume na aliyemuweka? Sio bongo
 
Unaanzaje kumfukuza uanachama mwenyekiti wa Chama na rais wa nchi mwenye majeshi yote ya ulinzi na usalama? Labda jeshi liamue hivyo tofauti na hapo haiwezekani
 
Back
Top Bottom