Kuna tatizo la kutumia feni mara ka mara?

Fmewa

JF-Expert Member
Joined
Nov 16, 2009
Posts
292
Reaction score
81
Habari za leo ndugu zangu.
Leo nimeona nije kupata ushauri kuhusu matumizi ya feni. Kila mara ninapolala usiku huwa natumia feni hiii ni kwa sababu ya hali ya joto la Dar Es Salaam ila ninasikia tetesi kuwa kuna matatizo kwa kutumia feni mara kwa mara nami nimekua na hofu kwa kua ninatumia feni kwa zaidi ya miaka mitatu sasa
Sasa naomba ushauri wa kitaalamu kuhusu jambo hili je inasababisha matatizo ya kifua? tafadhali mwenye ushauri anisaidie na kama kuna matibabu ambayo naweza kuyapata kabla matatizo hayajawa makubwa.
Asanteni sana
 
Ndiyo kuna matatizo.
Feni hukusanya vumbi laini na kulizungusha ndani ya chumba.
Ukivuta hilo vumbi linajikusanya kifuani na baada ya muda utaanza kupata tatizo la kuumwa kifua. Pia mafua huja kutokana na vumbi.
Nakushauri usitumie feni unapolala. Weka nyavu kwenye madirisha kama unaishi maeneo yenye joto.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…