Kuna timu iliadhibiwa kwa kugoma kucheza kisa kukosekana huduma za dharula uwanjani (Ambulance), sijui hili la Simba la Yanga limekaaje?

Kuna timu iliadhibiwa kwa kugoma kucheza kisa kukosekana huduma za dharula uwanjani (Ambulance), sijui hili la Simba la Yanga limekaaje?

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
11,550
Reaction score
40,697
Kuna jambo limenistua kidogo baada ya kusikia taarifa za bodi ya ligi kuhairisha mchezo kati ya Yanga na Simba kwa lengo la kwenda kufanyia uchunguzi madai ya Simba kuzuiliwa kuutumia uwanja wa Benjamini Mkapa kwa mazoezi siku moja kabla ya mechi. Tamko la Bodi ya ligi limetolewa masaa machache kabla ya mechi kuchezwa huku maandalizi yote muhimu yakiwa tayari yameshafanyika.

Hili ni tukio la pili ndani ya miaka mitatu, baada ya tukio la kwanza lilitokana na Yanga kugomea kuingiza timu uwanjani muda tofauti na uliotangazwa awali na TFF. Kipindi kile TFF ilifanya mabadiliko ya ghafla ambayo yalilalamiwa na Yanga kuwa yako kinyume na kanuni. Katika tukio lile, hakuna aliyewajibishwa na wala mchezo haukuhairishwa bali mchezo ulikuja kutangazwa tarehe nyingine ya kuchezwa.

Soma Pia: Bodi ya Ligi kuu yaahirisha Mechi ya Derby kati ya Yanga dhidi ya Simba

Kitu kilichonishtua ni namna TFF (bodi ya ligi) inavyoweza kuendesha shughuli zake kwa msukumo wa kufuata upepo wa hizi timu mbili za Simba na Yanga.

Kuna tukio liliwahi kutokea kwenye ligi yetu, ndani ya miaka miwili iliyopita, ambayo timu fulani ndogo ikiongozwa na kocha wake kugomea kuingiza timu uwanjani (pitch) ili ikaguliwe na mpira kuanza baada ya kocha wa timu husika kugundua uwanja ule haukuwa na Gari la kubeba wagonjwa (ambulance), jambo ambalo ni takwa muhimu la kikanuni kabla ya mechi yoyote kuchezwa ili kuhakikisha usalama wa afya za wachezaji uwanjani. Vyombo vya TFF vilikaa baadaye, kubariki timu husika kupokwa points na kumfungia kocha husika.
 
Simba kafanya uhuni.

Hakuwa na sababu za msingi za kukimbia mechi.

Ukizuiliwa kufanya mazoezi siku moja kabla ya mechi unakataaje kucheza mechi usika siku inayofuata?
 
Simba na Yanga wapo juu ya sheria,kanuni na Taratibu za TFF na Bodi ya Ligi
 
CCM Ndio inapenda vijana Wa Tanganyika waweke nguvu zao huko kwenye simba Na YANGA".

Great Thinker
.

Leo Tutaona Nyuzi za Simba na Yanga zaidi ya elfu 60 humu jukwaani.

TUKIWAAMBIA KUSHABIKIA SANA SIMBA NA YANGA KUNASABABISHA TUWE WA PUMBAVU HATUELEWI
 
Hiyo timu iliyofungiwa Haina uhusiano na Karia?
 
Simba kafanya uhuni.

Hakuwa na sababu za msingi za kukimbia mechi.

Ukizuiliwa kufanya mazoezi siku moja kabla ya mechi unakataaje kucheza mechi usika siku inayofuata?
Na nye mnazuiaje watu kufanya mazoezi wakati ni kitu kipo kwenye kanuni? Mna tabia za kishamba
 
Na nye mnazuiaje watu kufanya mazoezi wakati ni kitu kipo kwenye kanuni? Mna tabia za kishamba
Ulimpa nani taarifa kama unakuja kufanya mazoezi?

Au mlikulupuka tu na wazee wenu mkaja uwanjani?
 
Ulimpa nani taarifa kama unakuja kufanya mazoezi?

Au mlikulupuka tu na wazee wenu mkaja uwanjani?
Inajulikana,mda wa mazoezi unatakiwa uwe sawa na ule mda wa mechi halisi siku inayofuata, haya mmeenda uwanjani na hamjacheza imesaidia nini? Game itapangwa upya na mtacheza
 
Back
Top Bottom