Kuna tofauti gani kati ya maamuzi ya ki siasa na kisheria?

Kuna tofauti gani kati ya maamuzi ya ki siasa na kisheria?

infinix

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2018
Posts
2,096
Reaction score
2,150
Ndugu wanajukwaa la siasa,habari za jioni.

Naomba mnijuze kuhusu tofauti ya maamuzi ya kisiasa na kisheria. Mfano,wiki iliyopita,mh m bunge wa Kigoma,Zito R. Kabwe,aliita waandishi wa habari na kueleza msimamo wa chama chake kuhusu siasa,utendaji wa jeshi la polisi,hasa akizungumzia mauaji yaliyofanyika katka kijiji flani huko Kigoma hasa watu wa kabila la Wanyantuzu,alitaja idadi na pia wengine kwa mujibu wa maelezo yake waliuliwa wakiwa ndani ya hospitali.
Tunasikia polisi walimkamata,wakamhoji,na mwishowe wamempeleka mahakamani.
Kwa mawazo yangu ni kwamba,Zito ni mwanasiasa,hoja zake zimejikita kwenye siasa. Walichopaswa kufanya polisi ni kumjibu,ikiwa hayo matukio yalitokea au hayakutokea.
Hili tukio la kumkamata na kumpeleka mahakamani mimi binafsi sijaelewa msingi wake,au sababu yake ni nini..
Karibuni ndugu zangu kwa mjadala,natumaini tutatumia lugha nzuri ili kufahamishana kuhusu jambo hili.
Karibuni.
 
Mkuu sheria ni top master wa aspect zote ambazo unazijua. Siasa, uchumi, jamii, michezo na sanaa n.k

Zitto kama mwanasiasa (Mbunge) aliepewa dhamana na wananchi kuwawakilisha katika moja ya mihimili ya serikali (Bunge) anastahili kuhoji juu ya mambo fulani anayoyaona katika jamii yake (Au hata kama ni nje ya jimbo lake); katiba ya nchi inaruhusu (uhuru wa maoni na kujieleza)..

Kwa upande wa pili polisi na mahakama wao ni mhimili mwingine wa serikali ambao unasimamia na kutekeleza sheria za nchi (katiba).

Hivyo basi, kama kweli hayo matukio yalitukia na hakuna hatua zilizochukuliwa, either kwa polisi kutokuwa na taarifa n.k ni haki ya Kabwe kama mbunge/mwananchi kuhoji juu ya mambo hayo kwakuwa mauaji ni uvunjifu wa sheria. Hivyo anakuwa ametimiza wajibu wake wa kuvikumbusha vyombo vya sheria juu ya mambo fulani ambayo yanaendelea (ambayo labda wao wanayajua au 'wahayajui') *nacheka kidogo hapa* [emoji23].

Sasa kwa upande wa vyombo vya sheria ni kuwa wanapopata taarifa ya tukio fulani lazima wafuatilie kwa kufanya uchunguzi na kupata ushahidi ili wahusika wakamatwe na sheria ichukue mkondo wake.

Hivyo baada ya Zitto kuongea na wanahabari ni sawa polisi walivyomwita na kumpeleka mahakani ili akatoe maelezo ili kuisaidia polisi katika kazi ya uchunguzi maana inaonekana labda Zitto yapo anayoyajua ambayo pilisi hawayajui na ndio maana hawakuwa wanajua kuhusu hayo mauaji.

Mwisho wa yote ni kuwa, kitaratibu kabisa Zitto yupo sahihi na polisi wapo sahihi kama mambo yakiishia hapo nilipoelezea. Zaidi ya hapo ni sintofahamu nyingine.

Mwisho nimpongeze Mh. Zitto kwa kuwa kiongozi mzalendo na asieogopa kukema maovu.

Wakuu kama nimekosea nakubali kurekebishwa maana najua machache sana na najua kuna wenye kujua zaidi yangu.
 
Zito angekuwa mbunge wa Ccm asingehojiwa wala kutiwa ndani na mwishowe kupelekwa mahakamani.Polisi jukumu lao wangejibu hizo tuhuma bila kumhoji.Wanacho fanya polisi ni uendelezo wa Udikteta na ukandamizaji.Polisi wanataka watu wake kimyaa wasihoji jambo lolote.
 
Back
Top Bottom