Kuna tofauti gani kati ya maneno haya?

Kuna tofauti gani kati ya maneno haya?

MwanaFalsafa1

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2008
Posts
5,565
Reaction score
843
Napenda kuuliza kuna tofauti gani kati ya neno "marehemu" na "hayati"? Najua yote yana tumika kumtaja mtu aliye fariki ila juzi nikamsikia mtu ana sema aki taka angependwa kuitwa hayati na si marehemu. Siku weza kumuuliza pale pale ndiyo maana nimeamua kuja humu kuuliza.
 
wataalamu wa kiswahili (if I am not wrong) wanasema ni tofauti ya matumizi. ikiwa kwa mfano Nyerere unataka kutamtaja katika maongezi ya kawaida unaweza kusema marehemu, lakini ikiwa unakumbuka jambo alilotenda au usemi wake unasema hayati kwani usemi wake wawezza kuendelea kuexist.
too bad many presidents will never be hayati bali marehemu
 
Yote maneno yenye asili ya Kiarabu marehemu (Al-Marhum) kwa watu wa kawaida na Hayati (Al-Hayat) kwa watu wenye nafasi au jina katika jamii
 
Sina uhakika, ila wanasema marehemu ni asiye na kisomo, na hayati ni msomi na mwenye mchango ktk jamii.
 
Yote maneno yenye asili ya Kiarabu marehemu (Al-Marhum) kwa watu wa kawaida na Hayati (Al-Hayat) kwa watu wenye nafasi au jina katika jamii

Asante! hata mimi nilikuwa nikifahamu vivi hivi, ukiangalia kamusi ya kiswahili-English majina yote yana kuwa referred to as deceased or the late. kama alivyosema safari, hayati huwa inatumika kwa viongozi au watu wenye remarkable conbtribution kwenye jamii na marehemu ni kwa kila mtu. lakini nadhani pia si makosa mfano kusema marehemu mwal. Nyerere. Kwa ufupi ni kuwa kila Hayati ni Marehemu lakini sio kila Marehemu ni Hayati!
 
Marehemu
Tofauti ni nafasi aliyokuwa nayo huyo mtu kabla ya kifo chake. Katika hali ya kawaida kunawatu ambao tunawaita waheshimiwa. Yaani kila unapotaka kumtaja lazima uanze na Mh. Fulani, na pia wapo ambao hulazimiki kuanza na neno Mheshimiwa .... pindi unapotaka kumuita kwa jina, Hivyo basi tofauti hizi ndizo ambazo hupelekea kuwepo kwa matumizi haya ya Marehemu na Hayati katika nyakati tofautitofauti. Mtu ambaye katika uhai wake halitumiki neno Mheshimiwa basi akifa huitwa Marehemu,

Hayati
Kadhalika mtu ambaye hutumika neno Mheshimiwa ili kumuita, pindi akifa tunalazimika kutumia neno Hayati ili kuonesha kwamba bado tunaheshimu nafasi aliyokuwa nayo wakati wa uhai wake.

Tofauti katika matumizi
Kuna wakati inalazimika kuwepo kwa tofauti katika matumizi ya maneno haya. Mfano; unapotaka kumzungumzia mtu aliyekwisha kufa nje ya cheo au nafasi aliyokuwa nayo katika jamii basi litatumika neno Marehemu na si Hayati. Kwa mfano: tukimzungumzia Edward Moringe Sokoine nje ya nafasi aliyokuwa nayo wakati wa uhai wake tutasema Marehemu Moringe Sokoine ali........... Lakini tutakapokuwa tunamzungumzia katika nafasi ya uheshimiwa wake tutasema Hayati Moringe Sokoine ali.........


Ikumbuke haya yote si sheria ila ni utaratibu tu katika lugha, ambao umechukua nafasi kutokana na mazoea yaliyopo katika matumizisahihi ndani ya jamii zetu.
 
Pia Hayat linaweza likawa jina la Mtu!.. nina rafiki ya mpakistani anaitwa HAYAT
 
Asanteni nyote kwa majibu yenu. Sasa naelewa. Ila kwa kuendeleza tu mjadala.
 
Karibu tena kaka kwa kumalizia kuna kipande cha rylics nyimbo flan INTA HAYATI na hivi ndivyo walivyo tafsiri

Inta Hayati,
(You are my life)
Inta Habibi.
(You are my love)
Min awil nazra
(from the very first sight)
Wsourti nassibi.
(You became my destiny)
 
Neno Marehemu, linatokana na neno la kiarabu Al-Marhum, maana yake ni Mwenye Kurehemewa (Linatumika kwa Binadam aliye fariki au Kufa)

Neno hayati pia ni neno la kiarabu na maana yake ni Uhai, au Mwenye Uhai
 
Hivi m2 anaweza kuitwa 'hayati' siku 3 baada ya kufa au kabla hajazikwa? Hivi unaweza kusema ndugu wa hayati waje kutoa heshima za mwisho kwa hayati, hata kama alikuwa kiongozi au m2 mwenye nafasi katika jamii? Mimi navyojua, marehemu ni m2 aliyekufa na hajazikwa bado. M2 akifa hata kama itapita miaka 10 bila kuzikwa hawezi kuitwa hayati. Marehemu ni m2 aliyekufa na hajazikwa bado, na baada ya kuzikwa na kupita muda fulani ndio anaanza kuitwa hayati.
 
Pia Hayat linaweza likawa jina la Mtu!.. nina rafiki ya mpakistani anaitwa HAYAT

jf,raha kweli-kweli.
nasikia kuna mwingine anaitwa Hayat JK,yupo magogoni pale.!
 
Back
Top Bottom