Kuna tofauti kati ya Bongo Flava na Hip Hop

Sipendi kuwa shabiki kwenye huu mjadala lakini Mizozo umemwaga lekcha nzito hapo juu.

wako wapi wadu wa Bongo Flava nao waje wajitetee!!!

"Hip Hop will live Bongo Flava will perish as fast as it came"
 
Hey SUGU alikuwa mtu muhimu sana katika mapambano ya HIP HOP hapa TANZANIA tatizo ni baadhi ya MEDIA waliamua kumbania jamaa hadi akaona atimke
Nyimbo zake zilikuwa tight kwani jamaa alikuwa anapigania HAKI za watu mbalimbali
Sikiliza nyimbo kama MIKONONI MWA POLISI,MIAKA CHINI YA 18,ITIKADI,HAKI,DAR-DSM,DEIWAKA,NIKO KWENYE MIC,BARUA KWA RAIS,HALI HALISI na nyingine kibao
 
Bello thanks kwa Contribution.
Wadau wa Bongo flava nao wajitokeze kutetea upande wao unaobomoka siku baada ya siku na kuishia kuushikilia na vijigundi vya style ziso na uhai kama Baibuda!!!
Hivi kweli kwa jinsi Bongo Flava inavyoendeshwa ukiiunganisha na HIP HOP si utakua unatukana HIP HOP?
 
Sifikirii kuna kuna MSANII atasimama kuitetea BONGO FLAVIANA,hawana uhakika kwani upepo ukigeuka wote chali BIG G zimeisha utamu
 
Sipendi kuwa shabiki kwenye huu mjadala lakini Mizozo umemwaga lekcha nzito hapo juu.

wako wapi wadu wa Bongo Flava nao waje wajitetee!!!

"Hip Hop will live Bongo Flava will perish as fast as it came"

Hakuna kitu...Bado sijaona anabishana na mimi kitu gani...
what we need is massage and meaning!!!
 
......Sorry...what!! I dont get You!! unacho bisha ni nini....?
 

Tuambie kutokana na hayo maneno yako uliyoandika unasimama upande gani? Wa Bongo Flava ama Hip Hop...na ni nini kilikusukuma mpaka ukaamua M-crown Sugu ati Master wa Bongo Flava! Kwa Vigezo na misingi ipi?

Na mwisho ni kina nani wanakimbia aibu na hawataki kuonekana wamekuwa affected na other people's art?

Nakungoja.
 

Mimi ndio nilio kwambia....!! sasa nashaa unavyo react!!....
wewe ni mmoja kati ya hao wanao kimbia hiyo haibu!!
nafikiri bado hujui nini unataka kujua!!
 
Mimi ndio nilio kwambia....!! sasa nashaa unavyo react!!....
wewe ni mmoja kati ya hao wanao kimbia hiyo haibu!!
nafikiri bado hujui nini unataka kujua!!

Nimekuuliza maswali kadhaa na umeshindwa yajibu hata moja. Mjadala umekushinda nadhani ngoja tusubiri watu wengine ambao wanafahamu wanasimama upande upi watupe insights zao husiana na Mjadala wa Bongo Flava na Hip Hop ya Tanzania.

Ahsante kwa Ushiriki wako.
 

Kama maswali ulio uliza majibu unayo!!...kwanini usiwaeleze wafuasi wako!!
Kila ulicho uliza nimeshakujibu!!....ila nilicho gundua kutoka kwako..ni hujui nini unataka kujua..na unajua zaidi ya wafuasi wako tu!!
 
Nafikiri ni vyema kuweka Mbali tofauti zetu na kujenga hoja zaidi
Gigo's unetuelzea ni kwa nini unaamini hayo unayosema yako sahihi,ungetusaidia kuweza kuona mapungufu ya Mizozo
 
OK...Kuna tofauti kubwa kati ya Bongo flaver,
na Hip hop, kwasahabu Hip hop (neno na maana)ilikuwepo tangu awali!! Kumbuka hii ni www!!

Huwezi Ukaniambia Matonya anaimba R&B!! nika kuelewa!!....
au Inpetor haroon anaimba hip hop !??

Lakini wapo wanao fanya hip hop ya kiswahili...tatizo ni lugha...Labda sijui Maneno mengi ya kiswahili...hivi neno Hip hop utalitafsili vipi kwa kiswahili...
Hebu Huyo jamaa ani ambie!!...

Nili jaribu Rap Kuuita FOKAFOKA...lakini bado sijakubali...

Kati ya watu Walio Buni Jina Bongo flava-....! Bado hua nina Amini Mr2 ndie alie buni hiyo sauti...

Talatibu...tuta elewana!!
 
Nashukuru kwamba mimi na wewe kwa sasa tunaanza kuwa na mwelekeo mmoja kwa kiasi fulani. Ni tofauti cheche tu ambazo zilitufanya tuachane njia.

HIP HOP ni HIP HOP kama ambavyo imekwisha ainishwa toka mwanzao na ni kwamba hilo jambo haliwezi badilika. Na kwa Kiaswahili nadhani hilo neno litabaki kuwa hivyo hivyo kwani sidhani kama tunaweza pata Tafsiri muafaka juu ya hilo neno na kuna vichwa vingi hapa Bongo Wanafanya Hip Hop katika madhari ya hapa nyumbani ingawa kwa kiasi kikubwa bado wanakopa toka kwa waasisi wa mtindo huo wa Muziki. Bado hatujawa na true identity ya Hip Hop yetu.

Kwa Upande mwengine Bongo Flava ni mkusanyiko wa vitu vingi (Muziki aina Mbalimbali usio na dira wala mwelekeo) ambavyo kwa pamoja tuliamua kurahisisha na kuvirundika katika kundi tulilolibatiza jina la Bongo Flava. Mtazamo wangu huu ni muziki ambao unafanyika kama Bora Liende (Muziki wa Nyakati ambao unakuja katika kipindi kifupi ukilenga katika kuburudhisha na kukidhi mambo ya wakati huo). Kwa hiyo utaona ya kwamba wale wote ambao wanataka kujipenyeza katika medani ya muziki na kupata dakika yao moja on the spotlight, Bongo Flava ndo huwa Exit Route yao. Wanaingia kutoka na si vinginevyo!

Na mimi pia sidhani kama naweza kubali kama utaamua kuita Kufoka Foka maana hata Kingwendu katika Huyu Binti Mapepe anafoka vibaya mno. Pia kitu kingine ni kuhusiana na Mr. II kuwa ndo muasisi/aliebuni Bongo flava hapo ndio utata unapokuja. Kwangu mimi ni kwamba Safari za Mr II katika Medani ya Muziki wa Kitanzania ni kuhakikisha ya kwamba HIP HOP ya Bongo inasimama na hajawahi simama na 'Wabana Pua.' Ningeomba tu uniambie ni nini kimekusukuma mpaka ukawa na imani ya kwamba II ni aliyebuni hiyo Sauti.

~~Muziki ni maisha and Hip Hop is a way of Life.~~
 
mmmmh! MR II hakubuni!!!...MRII alionyesha uwezekano wa kughani kwa maana tena kwa kiswahili...nilipo anza niliona ni rahisi kughani kwa English kuliko kiswahili...na haikua na maana kwa waliokua wanasikiliza!!

Lakini MRII alionyesha ni jinsi gani Bongoflava anaipenda!!...
hata maneno yake kwenye nyimbo zake..amesha sifia neno Bongo flava...kabla hata wengine hawaja jua neno hilo...

Tatizo hapa ni majina..na kamwe tusipende kudharau hiyo bongoflava!! bado ni kitu kizuri!!.....

Ukweli ni kwamba...kazi bado ni nzuri...hakuna wabana pua...!!kama wanabana ni style tu!!...

Hebu nisaidie...hili neno bongofalva nani alilibuni?
 
Amani,

Hivi hakuna hata mtu mmoja ambaye anaweza kujitokeza na kutupatia Elimu na Ufahamu husiana na Bongo Flava ili mjadala wetu ukasimama zaidi maana naona wameamua kukimbia ama kukaa kimya sijui sasa ni lipi?

Sisi watu wa kusimamia HIP HOP ya Bongo Tunawangoja waungwana...na Majadiliano tu ya kupeana Ufahamu na Utambuzi wa Aina ya muziki wa Bongo. Tujumuike jameni!!!
 
Mizozo.
Kama vile ilivyo Bongo Flava isivyokua na Upeo na jinsi ambavyo mbali tu ya kinadharia ila hata kwa vitendo haioneshi kusimama,Ndivyo walivyo wadau wake.Wadu wa bongo flava hawafahamu Upepo wao unapoelekea kwa kuwa tu Hawana Misingi ya kusimamia the mushroom kind of music waliyonayo.

Hatutakuwa na haja ya kuwasubiri waje.Acha waje hapa wajifunze wakishatafakari na kuelewa ndipo watakapokua katika nafasi ya kungundua wapi wanakosea

Amani
 
Nami nabisha hodi katika mjadala huu,
aina hizi za muziki yaani HipHop na Bongoflava ni mkanganyiko kwa kiasi fulani hasa pale wadau[hasa wa HipHop wanapotaka kutambuliwa zaidi] hapo ndipo sekeseke linaanzia.

Kwa mtazamo wangu HipHop imekuja baada ya kucopy na kufanya marekebisho kufuatana na uhalisia wa nchini,baada ya muda songa mbele katika kile ambacho kinatafsiriwa kama makundi ndani ya HipHop[Hata ng'ambo yapo] yaani Hardcore HipHop-HipHop ngumu na Commercial HipHop ikazaa sasa tanzu ambayo imekuja kushika mizizi yaani Bongoflava[ingawa si jina zuri kwani linatoa taswira mjumuisho yaani kufunika tanzu zingine zote].

Maono yangu hii sasa inafaa iache kama aina ya muziki uliopo Tanzania na HipHop isimame pekee.Kwani Bongoflava ndani yake sasa imekuwa kwa kasi sana na kuwa na tanzu nyingi mathalani TAKEU[ile ya Mr.Nice], Bongo bangaraja[Hapa utawakuta kina Adili, zamani traki za awali za RAY C], Utamaduni [hapa kuna kina Mr.Ebbo, Msambaa, Wagosi wa Kaya].

Kwa kiasi fulani nguzo za HipHop zinafatwa hapa nyumabni na hii ieleweke kutokana na mazingira yaani unaweza kuona katika nyimbo kama za Nako2Nako watachanganya nguzo za HipHop katika upigaji wa shooting zao pia Kikosi cha Mizinga.

Ni kweli kwa sababu za kiuchumi imekuwa changamoto sana kwa wasanii hasa wa HipHop kubakia imara katika kutimiza utume wao na hii si hapa nyumbani bali hata ughaibuni mathalani Marekani ndiyo maana tunaona sasa 50 Cent anaimba Commercial HipHop wakati awali alikuwa anaimba HardCore[ambayo mara nyingi haiingizwi sokoni ama redioni] na kutumia janja nyingi kama bifu uzushi lake na wadau [sikumbuki sawia ni nani yule is it Kanye West?].

Mazingira kama haya tunaweza kuona hata hapa nyumbani watu kama AY,BINAMU,PROF JAY na baadhi wengine nao wanatumia mbinu kama hizo ili waweze kuishi.

Lakini nadhari pia ni ubunifu unahitajika sana ndiyo maana bado wakina NAKO2NAKO wanaimba Hardcore HipHop lakini bado wanauza na kuwapagawisha sawia mashabiki.Hapa ni pamoja na ujumbe na namna ya uwasilishwaji wa ujumbe huo.

Kwa sasa Bongoflava haijaweza sawia kuwa na indicators zake ama nguzo kama HipHop lakini due to time tunaweza kuja kugundua.

Nawasilisha kwa leo,
Naahidi nami kurudi tena.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…